Skip to main content

Elimisha mwanaume asibake(Rape) mwanamke....

....sio kufundisha Mwanamke jinsi ya kuzuia asibakwe!

Habari ya wewe? Nasema ahsante kwa kuichagua Blog hii.


Unategemea Nchi iliyoendelea kama UK kwamba huwezi kusikia suala la kuelimisha Wanaume kuhusu Ngono ili wasibake Wanawake via Media eti!


Wapo wachache walioelimika na wenye kumthamini Mwanamke na kumheshimu na kutomjaji kutokana na Mavazi yake. Pia Hukumu kali dhidi ya Ubakaji inasaidia kwa mbali.



Lakini bado kuna Wanawake na Wanaume ambao wanadhani kuwa Mwanamke kubakwa ni Kosa lake na hivyo kufundisha Wanawake namna ya kuzuia Kubakwa as in wasivae Mavazi yanayovutia Wanawame n.k.


Mwanamke Habaki.....sasa kwanini yeye awe responsible kuji-limit kwa ajili ya Mwanaume?


Kwanini Mwanaume asifunzwe kuji-control na kutomuona Mwanamke kama object ya kumalizia haja zake za Kimwili?



Kanini Mwanaume asifunzwe kuwa ili kufurahia Tendo ni lazima au ni vema upande wa pili ukubali kutoa ushirikiano na sio kulazimishwa?


Kwanini Mwanaume asionywe kuwa Kubaka ni Kosa? (Natambua wapo wanaosingiziwa na wapo wanawake wanaobaka Watoto ni issue inayojitegemea siku ingine).



Kwanini kwenye kila Jambo baya linalomtokea Mwanamke kwenye Maisha yake hasa ya kimahusiano na Ngono ni kosa lake....(well isipokuwa Mimba, ni kosa lako sababu ni wewe ndio unaruhusu mtu akuwekee mananilihu yake).


Kwanini baadhi ya wanawake wanapend kuwatetea wanaume kwenye suala la Kubaka sababu ya aina fulani ya Mavazi ya Mwanamke?



Usilete suala la "sio Asili yetu....Utamaduni wetu" kwa wewe unaenisoma kutoka Pande za Afrika(Wasomaji wangu wanatoka Kenya...Burundi...Rwanda)....Mavazi ya aina zote sio Utamaduni wala Asili yetu.....tuliletewa kama tulivyoletewa Imani za Dini.



Sisi zetu zilikuwa ni Majani na Magome ya Miti....Vibwaya ambavyo vilikuwa vifupi.....na vijikamba ili kushikilia Jani la mbele lisianguke na kuonyesha Nyeti.



Mzungu(well na Mchina) huyo huyo ameamua kuboresha mavazi ya Asili yetu na sasa tunavalia "flori" sketi ambazo zimechanua na  zina-move kama vibwaya.....nisizisahau Thongs ambazo ni kama vila walizovaa mabibi zetu miaka 9000 iliyopita (sina uhakika na namba hizo hihihihi but you get the idea).



Fundisheni Wanaume namna ya kuheshimu wanawake na chochote ambacho mwanamke anaamua kufanya juu ya Mwili wake....ni mwili wake hivyo anahaki na Mamlaka yakufanya chochote atakacho.



Mwanaume huna Mamlaka juu ya mwili wa Mwanamke.....unless ni mkeo in which nae pia atakuwa na Mamlaka juu ya mwili wako  kama Mumewe.

Babai.

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao