Skip to main content

Kuoga Usiku Vs Asubuhi/Mchana!


Haiyaaa!

Kiangazi Kimeisha na Mvua ime-cotton fire, hii sio sababu ya wewe kuacha kuoga. Usafi wa Mwili ni muhimu kama vilivyo vitu vingine Maishani. Lakini je wewe unaoga mara ngapi kwa Siku? na je kuna ulazima wa kuoga zaidi ya mara moja kwa Siku?






Wanawake tunapewa/peana PRESHA kuoga-oga  mara nyingi na tunaambiwa tusipooga tunatoa harufu kwa sababu ya Maumbile yetu, lakini wanasahau kuwa kunakosababisha harufu sio mwili as in Ngozi, bali kwapa na kunako(Nyeti) ambazo hata wanaume wanazo na zinatema harufu pia ikiwa hazitaoshwa.






Sasa nikianzia mwisho, hakika kuna ulazima wa kuoga zaidi ya mara Moja kwa siku, Inategemea unafanya kazi gani na wapi, unatumia Usafiri gani(kubanana  kwenye daladala/train hakika unabeba wadudu) na bila kusahau hali ya hewa. Ikiwa unafanya kazi Hospitali(una deal na maambukizo), unaishi mahali penye joto sana au kazi yako inakufanya utoke jasho sana mpaka unanata basi wewe oga mara zote unazohitaji.





Kitibabu tunapaswa kuoga angalau mara Nne kwa Wiki, hii ni kuisaidia Ngozi kutunza Mafuta yake asili na hivyo kuwa na afya njema. Pia inasemekana kuwa Kuoga mara nyingi kwa siku kwa kutumia Sabuni kunaongeza uharibifu wa Ngozi kutokana na matumizi ya Sabuni(Kemikali).





Nikijibu swali la pili, Mimi naoga Mara moja kwa siku(siku saba za Wiki), na ni  Usiku tu (nitakuambia kwanini as we go along)......nimezaliwa na Kukulia Dar es Salaam hivyo kuoga mara TATU/Nne kwasiku  ilikuwa ni kawaida(baada ya Kubalehe). Kabla ya hapo nilikuwa naoga/ogeshwa Jioni tu.






Nimeamua kuoga Mara moja kwa Siku baada ya Kuwa mama(sina Muda)......unakumbuka Enzi zile(au ni mie tu) ukiamka asubuhi unasafisha Kinywa, Uso, kwapa na Sirini(kuchamba) halafu unamalizia kulowesha Miguu ili kuwezesha Mafuta ya Rays ku-apply vema? Hii ilisaidia kuokoa Muda wa Baba/Mama (hasa kama mmpo wengi) na wote mnatakiwa kutoka kwenda Shule pale Baba/Mama anapotoka kwenda Kazini au kabla.



Sababu za Mimi kuoga Usiku tu(kama unajali):-

1)-Ni muhimu kuosha matatizo na vumbi/mioshi(hali ya hewa Chafu) yote ya siku nzima kabla ya kwenda kulala.

2)-Ngozi inajitengeneza/tibu vizuri ikiwa safi na unapokuwa umelala.

3)-Ni muhimu kuneng'enuka mwili ukiwa msafi/fresh(una harufu yake asilia).



Mara zote mwili (weka pembeni Uso, Kwapa na Nyeti) huwa hauchafuki kama unavyofikiria, hata unapokuwa Hedhini(mwanamke) au umefanya Ngono(wake kwa waume) huitaji kuoga Mwili mzima isipokuwa unasafisha pale panapohitaji kusafishwa.



Tambua nathamini ushirikiano wako, ahsante kwa kuichagua Blog hii.

Nikuache sasa, Babai.

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao