Mambo?
Kama ni mfuatiliaji(mshiriki) kwenye mambo mbali mbali yanayoendelea Online iwe ni kutoa Misada kusaidia wengine, kuhamasisha juu ya Afya, kuelimisha wengine kuhusu issue mbali mbali za Kijamii na hata yale ambayo ni Binafsi.
Utagundua kuwa hayo niliyoyataja hapo juu huwaunganisha watu wote na kuwa kitu kimoja kwenye Suala husika linalofanyika kwa Wiki/Siku husika, Pamoja na kuungana huko bado hutokea kutofautiana na kutokana na "utoto" wa baadhi basi kufarakana hujitokeza na hivyo kufanya baadhi kutengwa, semwa vibaya hali inayopeleka wengi kuogopa au kukwepa "kushiriki" kwenye hayo mambo ambayo baade hutumika kusuta wengine.....hukufanya hivi tulivyo fanya vile, halafu leo kimbelembele....si unajua?
Sasa ikiwa wewe ni kama mimi(sio mtu wa Drama) na hupendi kujionyesha au hutaki watu wakujuuuuuuue, yeah naandika mengi kuhusu mimi (Kila kitu Mie...got it?)lakini bado hunijui amini nakuambia hihihihihi. Anyway kama wewe upo kama Mie utakuwa na ile tabia ya kujipa Changamoto kivyako kwa faida ya watu wengine.
Changaoto za kujipa zipo Nyingi kuanzia kuchangia Ujenzi wa Choo Kijijini kwenu, Kuajiri Vijana kadhaa Wakati wa Kilimo, Kuchimba Kisima, Kusomesha Sekondari Watoto wa Fukara kila baada ya Miaka 4 n.k. Ili kukamilisha hili hutumii Savings bali unajitahidi ku-cut back matumizi yako ili kufanikisha Changamoto uliojiwekea.
Ukiachilia Mbali hilo, kuna zile Changamoto za kila Mwaka/Mwezi/Wiki ambazo ni za kibinafsi zaidi, na mimi nimeamua kujipa Changamoto ya Mwaka ya kutonunua Tope(Foundation) mpaka nilizonazo ziishe(namna ya kuzimaliza pia ni changamoto ndani ya Changamoto ambayo naifanya weekly).
Pamoja na kuwa tayari nina Changamoto inaendelea nikaona sio mbaya "nikisafisha" Mwili na nikajipa Changamoto ya kukata/ondoa Chumvi kwenye Chakula nilacho kwa Mwezi wote wa Rent, Nilipofanikiwa nikaamua kujipa Changamoto mpya ya kunywa Maji Mengi kwa Wiki moja ili niweze kufanya unywaji wa Maji kuwa Habit. Kawaida nilikuwa nakunywa 60ml kwa siku, hii ni kutokana na hali ya hewa na unywaji mwingi wa Chai.
Leo namaliza Wiki Moja tangu nianze kunywa Maji 1200ml kwa siku, safari haikuwa rahisi na siku ya Tatu nikaongeza na hivyo nikanywa 3000ml nadhani Mwili ulishtuka na hivyo nikaumwa sana Kichwa(too much water i guess). Siku kata tamaa nikaendelea na 1200mil zangu. Unatakiwa kunywa maji kulingana na Uzito wa Wili wako, kamuone Daktari wako au Kaguge au Pakua App, weka Kilo zako na app itakuambia unatakiwa kunywa mil ngapi kwa Siku ili kuepuka Kifo, yep Majini ni Uhai lakini too much yachukua Uhai(kifo).
Nilikuwa nakunywa vipi?
Najua unatambua kuwa hupaswi kunywa Maji hayo kwa mkupuo kwani utakuwa bloted na hata kusababisha matatizo mengine ya Kiafya ikiwa ni kuvimba Ubongo, hii ni kutokana na Maji kuwa zaidi kwenye Damu kuliko Chumvi na Sodium. Pia hupaswi kunywa Maji peke yake kwa wiki kwasababu unapata vimiminika vingine kutoka kwenye Chakula na Matunda bila kusahau Chai.
-Nikiamka tu 6am-Nakunywa 600mil(bila kusafisha Kinywa....heei)
-Dakika 30 kabla ya kifungua kinywa namimina 150ml
-Baada ya kifungua Kinywa namimina 150mil
-Dakika 30 kabla ya Mlo wa mchana nachukua 150mil
-Dakika 30 kabla ya Mlo wa jioni 150mil
Natumai Post hii imekupa mwangaza kiasi kuhusu faida ya kujipa Changamoto mwenyewe, Unaweza kujiunga na watu wengine kwa support online ila mie ni Loner na Control freak, i am much happier when I do things my way and all alone.
Shukurani kwa kuichagua Blog hii, naeshimu na kuthamini Muda wako hapa.
Babai.
Kama ni mfuatiliaji(mshiriki) kwenye mambo mbali mbali yanayoendelea Online iwe ni kutoa Misada kusaidia wengine, kuhamasisha juu ya Afya, kuelimisha wengine kuhusu issue mbali mbali za Kijamii na hata yale ambayo ni Binafsi.
Utagundua kuwa hayo niliyoyataja hapo juu huwaunganisha watu wote na kuwa kitu kimoja kwenye Suala husika linalofanyika kwa Wiki/Siku husika, Pamoja na kuungana huko bado hutokea kutofautiana na kutokana na "utoto" wa baadhi basi kufarakana hujitokeza na hivyo kufanya baadhi kutengwa, semwa vibaya hali inayopeleka wengi kuogopa au kukwepa "kushiriki" kwenye hayo mambo ambayo baade hutumika kusuta wengine.....hukufanya hivi tulivyo fanya vile, halafu leo kimbelembele....si unajua?
Sasa ikiwa wewe ni kama mimi(sio mtu wa Drama) na hupendi kujionyesha au hutaki watu wakujuuuuuuue, yeah naandika mengi kuhusu mimi (Kila kitu Mie...got it?)lakini bado hunijui amini nakuambia hihihihihi. Anyway kama wewe upo kama Mie utakuwa na ile tabia ya kujipa Changamoto kivyako kwa faida ya watu wengine.
Changaoto za kujipa zipo Nyingi kuanzia kuchangia Ujenzi wa Choo Kijijini kwenu, Kuajiri Vijana kadhaa Wakati wa Kilimo, Kuchimba Kisima, Kusomesha Sekondari Watoto wa Fukara kila baada ya Miaka 4 n.k. Ili kukamilisha hili hutumii Savings bali unajitahidi ku-cut back matumizi yako ili kufanikisha Changamoto uliojiwekea.
Ukiachilia Mbali hilo, kuna zile Changamoto za kila Mwaka/Mwezi/Wiki ambazo ni za kibinafsi zaidi, na mimi nimeamua kujipa Changamoto ya Mwaka ya kutonunua Tope(Foundation) mpaka nilizonazo ziishe(namna ya kuzimaliza pia ni changamoto ndani ya Changamoto ambayo naifanya weekly).
Pamoja na kuwa tayari nina Changamoto inaendelea nikaona sio mbaya "nikisafisha" Mwili na nikajipa Changamoto ya kukata/ondoa Chumvi kwenye Chakula nilacho kwa Mwezi wote wa Rent, Nilipofanikiwa nikaamua kujipa Changamoto mpya ya kunywa Maji Mengi kwa Wiki moja ili niweze kufanya unywaji wa Maji kuwa Habit. Kawaida nilikuwa nakunywa 60ml kwa siku, hii ni kutokana na hali ya hewa na unywaji mwingi wa Chai.
Leo namaliza Wiki Moja tangu nianze kunywa Maji 1200ml kwa siku, safari haikuwa rahisi na siku ya Tatu nikaongeza na hivyo nikanywa 3000ml nadhani Mwili ulishtuka na hivyo nikaumwa sana Kichwa(too much water i guess). Siku kata tamaa nikaendelea na 1200mil zangu. Unatakiwa kunywa maji kulingana na Uzito wa Wili wako, kamuone Daktari wako au Kaguge au Pakua App, weka Kilo zako na app itakuambia unatakiwa kunywa mil ngapi kwa Siku ili kuepuka Kifo, yep Majini ni Uhai lakini too much yachukua Uhai(kifo).
Nilikuwa nakunywa vipi?
Najua unatambua kuwa hupaswi kunywa Maji hayo kwa mkupuo kwani utakuwa bloted na hata kusababisha matatizo mengine ya Kiafya ikiwa ni kuvimba Ubongo, hii ni kutokana na Maji kuwa zaidi kwenye Damu kuliko Chumvi na Sodium. Pia hupaswi kunywa Maji peke yake kwa wiki kwasababu unapata vimiminika vingine kutoka kwenye Chakula na Matunda bila kusahau Chai.
-Nikiamka tu 6am-Nakunywa 600mil(bila kusafisha Kinywa....heei)
-Dakika 30 kabla ya kifungua kinywa namimina 150ml
-Baada ya kifungua Kinywa namimina 150mil
-Dakika 30 kabla ya Mlo wa mchana nachukua 150mil
-Dakika 30 kabla ya Mlo wa jioni 150mil
Natumai Post hii imekupa mwangaza kiasi kuhusu faida ya kujipa Changamoto mwenyewe, Unaweza kujiunga na watu wengine kwa support online ila mie ni Loner na Control freak, i am much happier when I do things my way and all alone.
Shukurani kwa kuichagua Blog hii, naeshimu na kuthamini Muda wako hapa.
Babai.
Comments