Heri ya Mwezi mpya wa May. Mungu abariki kila jema upangalo kufanya(na-sound kama Pastor sasa eti?)!
Umewahi kujiuliza kwanini Mwanao/Wanao huwa na Homa au Vikohozi visivyokwisha? Ukimpeleka Hospitali na kupima Damu na kila kitu majibu ni kuwa hana Malaria wala Typhoid (hatuna huku ila inawezekana ulipo haya Magonjwa yapo) na magonjwa Mengine ya Utotoni. Wahenga...well Bibi yangu alisema "Mwanangu kuwa Uyaone", mie nasema kuwa na Watoto ujifunze!
Wazazi wengi huamini kuwa Soda husababisha Watoto kuchangamka kupita kiasi na pengine kukosa usingizi, baadhi huamini kuwa hufanya Watoto kuwa na tabia za ajabu(wabishi,wakahidi, hawakusikilizi, wananguvu kupita kiasi) kutokana na Soda ambayo huwafanya kuwa "high". Sasa hizo ni Soda na zina some sort of "hewa" sio, kwamaana hivyo Juice za kawaida ambazo hazina Sukari ni salama(nilidhani) tena zile ambazo unachanganya na Maji(squash) ndio Bora zaidi(nilijidanganya).
Kuna wakati tulikuwa tukinunua aina Juice ya Matunda"asilia"bila kuongezewa Sukari, maalum kwa Watoto. Matokeo yake (bilakujua) Babuu akawa na Homa zisizokwisha, yaani karibu kila siku Anachemka. Siku moja tulipoenda "Manunuzini" ile Juice haikuwepo in Stock hivyo tukanunua Brand nyingine ambayo ilisema kuwa ni jutoka kwenye Matunda Halisi aka "Natural" hakuna addictives. Babuu hakuwa na Homa tena. Ziporudi zile zilizokuwa out of stock tukanunua tele(maana alikuwa akizipenda), Homa zikarudi, hapo ndio nikagundua kuwa Zile Juice zina kitu ambacho sio Salama!
Kama Kacha(kawaida, Utamaduni) nikaenda Gugo, na kuuliza sababu ya juice "husika" kusababisha Mtoto kuchemka/Homa. Nikakutana na "Aspartame" ambayo ni Sweetner wanayoweka kwenye Juice kuongeza Utamu badala ya kutumia Sukari ya Kawaida. Na huu ndio ukawa Mwazo wa mimi kuwa "Mlevi"wa Kusoma Ingredient(Vitu walivyotumia kutengeneza Bidhaa husika). Natumia muda mwingi kusoma "ingredient" zaidi ya kulinganisha Bei.
Nia ya Post hii ni kukupa mwanga kuwa sio Soda tu zinazoweza kufanya Mtoto "achangamke" sana hata zile Juice laini zinazosema "no Sugar added" zinamadhara kwa Watoto kwa namna tofauti. Mwanangu Homa(naturally ni very active), Wengine wanakuwa too High/Over active
Baada ya Muda nikaja gundua lingine, Mwanangu Hapatani(Allergic) na Karanga au anything Nuts....kuwa na Watoto ujifunze eeh! Tulipiga sana Misele kwa Dermatologist nikaja kugundua Mwenyewe kuwa tatizo ni Karanga(nilizila sana nilipokuwa Mjamzito) na Ngozi yake ni Sensitive na hivyo haitaji Hash Soaps,Lotion etc....hii ni Topic ingine(nikumbushe nikusimulie na nikuambie tunatumia nini ku-keep ngozi safi na yenye afya, no miwasho wala ukavu).
Pamoja na kusema hivyo, usitumie Post hii kama Ushauri wa Daktari, Ikiwa Mwanaoa anaugua Homa mara kwa mara nenda kwa Daktari kwa Ushauri wa kitibabu na Vipimo/Tiba. Lakini pia ondoa vinjwaji ambavyo sio "Asilia".
Unaweza kutengeneza Juice mwenyewe kutokana kwenye Tunda Fresh. Natambua kuwa kila tulacho siku hizi kina Kemikali(sio natural), lakini mpaka sasa hakuna Issue kiafya inayotokana na Maji ya Matunda kutoka Tunda asilia.
Ahsante sana kwa kuichagua Blog hii, tambua kuwa na heshimu na kuthamini Muda wako hapa!
Babai.
Comments