Skip to main content

Kufanya Mapenzi(Ngono) Hakujengi Ndoa yenye Furaha......


....lakini ni "Madhara" ya Ndoa yenye Furaha! Nimekuchanganya si eti? hata mie sielewe nilichoanza kuandika ila endelea kusoma na mimi niendelee kuandika na kwa pamoja tunakuwa kwenye Mstari na hivyo sote kuelewa. Hujambo lakini?



Ngono au Kufanya Mapenzi(kama tunavyopenda kuita sie tulio Ndoani ili kuhisi "Utakatifu" wa Ndoa zetu) sio Muhimu kiviiiiiile, Muhimu ni kutunza au kuendelea kuwa na  ile hali ya kuvutia/vutiwa na Mwenza wako. Kwamba, sasa ni Miaka 8 ya Ndoa yenu lakini bado unapata misisimko uleule uliokuwa ukiupata pale anaposema "kesho nakuja"....tofauti sasa unajua anarudi saa ngapi nyumbani kwenu....Sauku ya kumuona inakupa tabasamu kuu.



Wakati mwingine Unajiambia/jisemea ni jinsi gani unampenda Mume/Mkeo bila yeye kukusikia. Wakati mwingine wala huamini kuwa unaishi na Mwenza umpendae hivi(japo huwa anakuudhi na unamnunia)....Ukimuona Mkibaba unahisi "kunyetukanyetuka" na yeye akisikia sauti yako  Mkimama basi tena hana Hali. True Story!! turudi kwenye Topic...



...Ngono (Kufanya Mapenzi) ni Madhara ya Ndoa yenye furaha.....unajua, kila kitu kina Faida na Madhara yake si ndio? Sasa faida za Ndoa zipo nyingi lakini Ngono(kufanya Mapenzi) sio moja wapo. Kufanya Ngono(Mapenzi) ni Madhara ya kuwa na Ndoa yenye furaha. (Hiki kipengere kimejirudia....Usijali, kuandika na kueleweka sio kazi rahisi kama udhaniavyo)!


Kwamba, ni lazima Madhara hayo yakupate ikiwa Ndoa yako imesimama Imara na imejawa/egemea Upendo, Furaha na yale yote Mema mlioelekezwa, funzwa, jifunza n.k. Pamoja na kusema hivyo bado Ngono(kufanya Mapenzi) haipaswi kufanywa Kila siku. Ikifanyika kila siku inapoteza "Mngaro"? hihihihi mnapoteza "ubunifu" a.k.a mnaishiwa!....



......ndio hiyo inatoka kwangu Mie yule wa Enzi pale Dinahicious, ambae nilikuwa nawashanga sana Watu wanalala vipi Kitanda kimoja bila kupandana kila siku angalau Mara 3. Achana na hili. Mnapokuwa kwenye Ndoa mambo mengi hutokea, kumbuka mmeunganisha Familia mbili tofauti. Kila familia hukutwa na issues zake ambazo huwahusisha ninyi pia kwa pamoja. Kwamba likija kutoka kwenu ni lake  na likija kutoka kwa Mumeo pia ni lako. Ukiachilia hayo kuna Malezi ya Watoto na Majukumu Mengine kibao ya Kimaisha.



Sasa mnapoishiwa "Mngaro" au Ubunifu ni wazi kuwa mtakuwa na kazi ya ziada ya kutafuta mambo Mapya ambayo katika hali halisi ni yale yale tu sema hamjayafanya kwa muda Mrefu, but Muda wa kufikiria on how to actually do it tena unagharimu kwani tayari Masaa 24  yapo full....ni kama vile hayatoshi.



Hivyo ni Muhimu kufurahi pamoja bila kukutanisha Miili nakufanya Mapenzi Daily(mara 3-4 kwa Wiki inatosha), kama bado au  ulikuwa hujui basi jaribu kujifunza  kuwa karibu nae:-

1)-kuonyesha Mapenzi kwa Vitendo popote mlipo bila kuingiliana, Busu, shika/gusa kwa Huba, Mahaba yaani kuwa "Intimate".

2)-Kiroho-kujadili Imani yenu/zenu na Kusali pamoja.

3)- Kiakili-Kufanya Mazungumzo ambayo hayahusiani na Watoto/Kazi/Ndugu.

4)-Ongezea as you go.....



Mpaka umefika hapa ni matumaini yangu kuwa umenielewa au tumeelewana. Kama bado basi usisite kuni-Tweet nami nitafanya Blog Post ingine Spesho kwa ajili yako.


Nathamini Muda wako mahali hapa na Ahsante sana kwa kuichagua Blog hii.

Babai.

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao