....sio kiviile ila close(I promise)....Jello!
Kama Jojoba ni Hohoba kwanini Hello isiwe Jello?
Ni kawaida kwa wengi kutafuta "namna ya" kupenda, kuridhisha, kuonyesha mapenzi, kujali n.k. Kuna siku Mtu aliniuliza afanye nini ili Mumewe amuombe radhi? nikashangaa...kuna watu hawajui kuomba Radhi Wenza wao?
Hakika hakuna Kanuni kwenye Maisha ya Ndoa lakini kuna yale mambo "basic" ambayo ni lazima kila mtu ayajue na kuyafanya/tenda. Mambo hayo huwa tunafunzwa tukiwa angali wadogo, tukianza Shule na kuendelea kuona Wazazi na watu wetu wa karibu wakiyatenda/fanya . Bila kusahau kutukumbusha pale tunaposahau kuyafuata/tenda/fanya.
Ndio maana siku zote huwa nasema kuwa Mwenza ulienae hivi sasa ni Matokeo ya Malezi/Makuzi yake bila kusahau Mazingira aliyokulia. Kiongozi kwenye Malezi hayo mambo huwa ni Mama (au Msaidizi mwenye Values kama wewe au bora Zaidi) kwavile ndio huwa anakaa na Mtoto kwa muda mrefu kuliko Baba.
Sasa pamoja na kuwa wengi wetu hutegemea/dhania kuwa Kila Mwanaume ni lazima awe "loving" kama "Romeo" kwa Juliet, kwamba anakuambia anakipenda mara kadhaa kwa siku kwa aina tofauti ya Maneno, mkiwa mtaani anapachika Mkono kiunoni, anakupandisha garini kabla yeye hajapanda, anakubusu mara kibao kwa siku, anafanya Ngono Kiromansi mara zote mnapohitajiana...Romeo huyo hakulelewa kwenye Mazingira yale yale aliyolelewa Mumeo. Romeo ni yeye na Mumeo ni Mumeo.
Suala muhimu hapo ni kwako wewe kumjua vema Mumeo kabla hajawa Mumeo, vilevile ni kwako wewe kuwa wazi kwake(usi-settle for less ila usiende overboard)....kama kuna mambo hawezi/hajui kuyafanya na sio muhimu sana kwako basi achana nayo. Mf;- Kutolewa nje kwa jili ya Mlo, Yeye kuosha Vyombo, Kukuimbia, kusema "honey i am hooooome" hihihihi.
Kuna yale muhimu/basic ambayo ni lazima ajifunze kuyafanya hata kama hawezi, nayo ni Heshima, Ukweli, Thamini, Shukurani na Kuomba Msamaha/radhi. Ikiwa Mumeo kabla hajawa Mumeo na hujamuweka sawa kwenye hayo basi Ndoa yako itakuwa Chungu...utahisi kuwa Ndoa yenu ni ya Mtu mmoja na utakuwa Mpweke Ndoani. Utahisi kumpenda Mumeo lakini hutopendezwa nae Siku 305 kati ya zile 365 za Mwaka!....je unaweza kuishi na Mtu anaekuudhi kwa Muda huo wote wa Maisha yako?
Sie wa "kizamani" tulifundwa kuwa Mke anaweza kuchukua nafasi ya "Mama" kwenye kumuweka sawa Mumewe, ila sasa unapomfunza Mumeo yale muhimu ambayo Mama yake labda hakutilia maanani hupaswi kuwa kama Mama yake kweli na yeye kuwa Mtoto wako bali unapaswa kufikisha "Somo" kivingine ukijitumia wewe kama mwenye hitaji la "tabia njema" kutoka kwake Mumeo Mpenzi.
Ninachojaribu kusema hapa ni kuwa Wanaume hawafanyi mambo yale yale ambayo wewe unadhani ndio Kupendwa na kwamba kila Mwanamke anapata "Tamu" ya "Romeo" kwa Juliet. Kuna Wanaume ni Wapenzi wazuri sana lakini hawajui kusema "Nakupenda" kila siku, hawajui kusema "samahani/nisamehe" kila wanapokukosea, hawajui kuwa Romantiki.....wana namna zao tofauti-tofauti za kufikisha ujumbe kuwa wanakupenda, wanaomba msamaha na kuromantika.
Siwajui Wanaume wote Duniani ila "I lived" hihihihi so nitakupa Uzoefu wangu. Tafadhali usikose kunitembelea tena ili ujue ni namna gani hasa baadhi ya Wanaume hufikisha ujumbe uleule wa kiRomeo bila kuwa kama Romeo.
Nathamini na kuheshimu Muda wako hapa, ahsante kwa kuichagua Blog hii.
Babai.
Comments