Skip to main content

Rudisha Heshima Ya Ndoa: Mwenza hana Jema, kila siku Kukosoa...



Kukosoana ni jambo jema na muhimu ili kusaidia kurekebisha Tabia ndogo-ndogo ambazo ni mbaya lakini kumkosoa  Mwenza wako mara kwa mara (kupitiliza) bila wewe mwenyewe kujali kuwa unakasoro zako ambazo anazivumilia ni wazi utakuwa Mnyanyasaji. Unyanyasaji huo utamfanya mwenzio kujisikia vibaya na hivyo kusababisha:-

-Maumivu ya Hisia na Akili.
-Kumfanya Mwenzio ajione hana thamani au Umuhimu kwenye Ndoa yenu.
-Uoga/Hofu  kwenye Ndoa yenu
-Kuondoa Furaha na hivyo kujitenga kihisia
-Kukosa Amani
-Msongo wa Mawazo


Kwasababu Mwenza wako sio Mlalamishi au Mkosoaji wa mara kwa mara haina maana kuwa wewe ni Mungu na hukosei, kwamba wewe ni next to perfect(hakuna binadamu asie na Kasoro) ndio maana Mkeo/Mumeo hajawahi kukukosoa au kulalamika.


Ukweli ni kuwa, baadhi ya Weza huwa "wanakurekebisha" kwa vitendo, kwamba anafanya exactly vile unapaswa kufanya au kwa kukupa "hints" bila kuumiza Hisia zako wala kusababisha ujisikie vibaya. Asipo pata matokeo ndio anaweza kukuambia.

Ni vigumu sana kuishi na Mwenza wa hivyo kutokana na maumivu anayokupa. Sasa kabla hujaanza kupanga namna ya kuikimbia Ndoa yako, tulia kwanza nikuambie nini cha kufanya, Jinsi ya kuepuka....ila kabla tuanze na sababu zinazoweza kupelekea Mwenza kukukosoa kupita Kiasi(kuku nyanyasa Kihisia/Kiakili).


Nini hasa huwa kinasababisha Mkosoaji kupitiliza?

-Hawana raha/furaha na jinsi walivyo na hivyo wanataka na wewe uwe kama wao bila kujua.

-Majuto; inawezekana kutokana na Makosa yao ya Maisha huko nyuma kabla yako.

-Fainali Uzeeni, hajafanikiwa kukamilisha Ndoto zake na hivyo anatupia "Mpira wa lawama" kwako kama sababu ya yeye kufeli/kutofanikiwa(Wakati hukuwepo wakati wa Ujana wake).

-Malezi/Makuzi  mabovu aliyopitia....ama hakulelewa na Wazazi moja kwa moja  bali Ndugu kama vile Dada/Kaka/Bibi/Babu n.k. kwa zamu,  kwamba hakuwa na "Stable family" utotoni mpaka utu Uzima.


Nini cha kufanya:-

-Usiwe Hasi kwake wala kumkosoa(rudishia). Mwache atiririke na wewe Msikilize kwa makini ili upate materials/points za kutumia Moto wake ukipoa. Usisababishe Mabishano hasa kama mna Watoto.

-Utakuwa umeumia sana kihisia(kwa kawaida kama Mwanamke utakuwa umemchunia), pamoja na maumivu hayo jitahidi kufikiria yote anayokukosoa/lalamikia kila siku. je yanajirudia? je kuna mabadiliko umefanya(jirekebisha)? je haoni jema pamoja na kuwa umejirekebisha? je alikuwa amekunywa kidogo?( ona point ifuatayo hapo chini)

-Baada ya Maumivu/Mnuno/Chunio kuisha, Mwambie ungependa mzungumze. Utakapo anza kuzungumza nae mwambie wazi kuwa ungependa mzungumze na sio mbishane, kwamba akusikilize.

-Ongea nae kwa Upole lakini kwa kumaanisha tena kwa kumuangalia Usoni moja kwa moja. Mwambie tabia yake ya kulalama/kosoa kila akipata nafasi inavyokufana ujisikie. Weka wazi kuwa huna furaha tena kwenye Ndoa yenu kutokana na Tabia yake hiyo mbaya(nafasi yako kumkosoa hii, itumie vizuri. Simamia kwenye yeye kukukosoa kupita kiasi na alivyokufanya ujisikie, mengine save ili usimuumize).

-Mwambie ni sawa kukukosoa lakini sio sahihi kurudia yaleyale kila mara bila kuangalia kama umefanya mabadiliko, pia sio vema kila mnapokuwa pamoja yeye ni kukosoa tu. Mwambie hudhani kuwa hakuna jema hata Dogo ufanyalo na kustahili kukusifia/shukuriwa. Mpe mfano wa Mema unayodhani unafanya kwenye Ndoa  yenu au kwenye Malezi ya Watoto wenu.

-Malizia kwa kusema, nisingependa Ndoa yetu iishie pabaya na nisingependa watoto wetu wawe wanakusikia ukilalamika kila siku kwa mambo yale yale au pengine kusingizia ili upate nafasi ya kukosoa.


Una nyongeza? swali je? tupia humu dinahicious@gmail.com
Sijibu Email moja kwa moja bali nitaweka hapa kwa faida ya wengine.
Nathamini na kujali Muda wako hapa, ahsante.

ooh Post ijayo itakuwa Jisni ya Kuepuka Ukosoaji wa Mara  kwa mara, Usikose
Bai

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao