Skip to main content

Posts

Showing posts from March, 2015

Jikubali, Jipende Jiamini so they say....

Habariiii! Baadhi huitaji support ili waweze kujikubali kujipenda na kujiamini halafu wengine tumezaliwa hivyo.....si vema kukurupuka na kumwambia mtu lazima ujiamini bwana blablabla.....sio chee kama udhaniavyo. Ni rahisi kujipenda, kujikubali na kujiamini angalau ukiwa umefikisha miaka 25(in my head umri huo ndio unaanza kujitambua na kujijua....unakuwa umekua). Mara zote Binti unapenda kuchukia baadhi ya vitu kwenye mwili wako hasa kipindi cha Kubalehe(tunabadilika). Huwa ni ngumu sana kukabiliana na mabadiliko ya ndani na nje ya mwili.....kiakili na kihisia. Kipindi hiki unaanza kujiona MZURI leo basi linapokuja suala la kuagizwa Dukani wewe ni wa kwanza kutaka kwenda ili "wakuone" si wajua kale ka atensheni ka wavulana kanakokusaidia kujua ujinsia wako? Kanakuwaga enjoyable sana......halafu kesho unakuwa MBAYA unagoma hata kwenda Shule unasingizia unaumwa er Macho (that was me). Ukifikia miaka 25 mabadiliko yanakuwa yameseto na kilichobaki ni kunenepa au kukonda. Un

Wanaume wanaopenda Natural Beauty....

Lakini bado wanavaa Nguo.....waogope sana! Kwanza ni kwanini hasa wanaume wanapenda kufuatilia masuala ya Urembo wa Wanawake au Mavazi ambayo hayawahusu? Jibu: Wanaogopa gharama au roho mbaya bin Mfumo Dume. Mwanamke anakuwa judged muda wote kwa maisha yake yote.....hata mimi nahukumu wanawake wenzangu na mimi mwenyewe lakini hapo hapo huwa najaribu kuelewa kwanini wapo hivyo walivyo(ukiachilia mbali Uwezo wa kifedha) kwasababu najua UANAMKE una issues zake ambazo mwanaume hawezi kuzielewa. Kutokana na kuwa judged muonekano wa Uso/Sura ni muhimu kuliko sehemu nyingine za mwili ambazo anaweza kuziziba kwa kuvaa nguo. Mwanamke anapendezeshwa kwa Vipodozi, Mavazi, Vito vya Thamani na Manukato. Ili mwanamke apendeze inabidi awe msafi na ili awe msafi ni lazima aitunze Ngozi yake, Kucha na Nywele......hivi vyote ni gharama. Unawajua wale wakibaba wanaopenda independent women with natural beauty?So that they can spend their money on others while you (independent woman)pay Bills na

Ile Manukato ya Kiume uitakayo...

Mambo? Miaka ya nyuma nilikuwa nina aina mbili tu za Manukato.....moja ya Jioni (Organza) na nyingine ya kutwa nzima(Eden) harufu zake zinadumu muda mrefu....huitaji kujimwagia tena. Nikaja kukutana na mdada mmoja anapenda Manukato kupita kiasi....kwamba akiwa na pesa ya ziada lazima anunue.....tena Designer ones. Nikawa namshangaa nikisema anahitaji signature kwa maana aina moja au mbili tu za harufu basi nikawa namuita perfume addict. Sasa leo hii napanga makorokocho yangu jikagundua nina Chupa kama Nane hivi za Manukato.....ama kweli hujafa hujaumbika! Kati ya hizo zote my classicO Organza haipo sababu iliniudhi nilipokuwa mjamzito kwa mara ya kwanza.....will have to revisit(kuinunua tena).....ila Eden made it! Unajua pale unapendezwa na Manukato ya Kiume sio harufu yake tu bali Chupa husika inapendeza ukiiweka pale kwenye dresser si eti? Basi unajifanya umemnunulia Asali wa Moyo kumbe kiukweli umejinunulia mwenyewe kwasababu huwezi kujipulizia Manukato ya kiume basi unamnusa

Best Umri wa kufurahia Maisha.

Habari yako? Je kuna umri uliopita na ukadhani ulifaidi sana na kufurahia maisha kuliko sasa au miaka michache kati kabla ya umri ulionao sasa? Sijawahi kufanyiwa au kufanya sherehe ya siku ya Kuzaliwa sio tu kwa sababu za Kikacha kuwa hatuna hizi mambo (unaiga tu) lakini pia binafsi sipendi mikusanyiko ya watu na ikiwa naeza kuepuka kwa kutokuwa na Party basi na iwe hivyo....so yeah. Naishi kwenye Nchi ambayo kutimiza miaka fulani ni big deal na hivyo mhusika kutaka ku-share siku yake maalum na watu wengine. Hiyo ni Kacha yao na hivyo inawafanya (Kazini wanajua DoB na anuani yako so huna jinsi)baadhi wanipatie zawadi na hapo ndio suala la "am too old for the party ila zawadi napokea" linakuja  badala ya kuzikataa. Kuna umri ambao nahisi nilifurahia zaidi maisha yangu na hivyo kuzipenda namba au umri huo uliopita. Sikuwa chini ya Wazazi na sikuwa na majukumu. Nilifanya maamuzi bila kujali watu wengine....Baada ya hapo nikawa busy  na maisha. Tangu Kibibi(princess) ameac

Mwanao anapoleta the Ex Factor

Kwa wale ambao Uhusiano wa bf na gf uliharibika na kuvunjika kwa sababu zozote na kwa bahati mbaya mlizaa (ukizaa na mtu halafu ni X mwenzangu ni bahati mbaya). Sasa imagine kila unapowakorofisha watoto......watoto hukasirika tu hata kwa yale mema kwao.....mf unawakataza wasicheze Jikoni ni hatari au unahimiza wafanye home work badala ya kutazama Tv. Kila unapokwenda kinyume na watakavyo kama mzazi kwa faida yao wanaanza kulia au kununa na kumtaja mama au baba yao......"Baba angekuwepo ingekuwa hivi au vile" au "mama angekuwepo asingenikataza hili au lile" na hiyo huwaongezea huzuni na hata kilia kwa Uchungu bila wewe kuwaona. Mara chache unaweza kusikia wakimtaja mzazi mwenzio ambae ni mama au baba yao lakini umeachana nae na sasa unamchukia. Nimesema hayo yote kutokana na tabia ya Babuu pale unapomuudhi(ukimkataza kufanya kitu).....ananuna halafu anasema "I want my dad to come and cheer me up". Maneno hayo hunifanya nimuonee huruma (ndio atak

Nakupa mapenzi alionipa Mama....

Unless hujui Elimu ya Viumbe Hai hasa kuhusu Mwanadamu utabisha na pengine kuwa offended. Unaeza kudhani kuwa Ali Kiba amemkosea adabu Mama yake na pengine ulajiiliza utampaje mpenzi wako Mapenzi aliyokupa mama obviously hayato tosh......halafu ukawaza ni mapenzi gani hasa mwenzetu alipewa eeeh! Well uhusiano wa kwanza wa mtouo yeyote ni ule wa yeye na Wazazi wake.....mtoto hajui kupenda mtu yeyote zaidi ya wazazi wake hivyo lolote analopata kuyoka kwa wazazi hao ni mapenzi. Linapokuja penzi la mama kwa mtoto wale wa Kiume au Baba kwa Binti yake kidogo kuna mkanganyiko na wengi hushindwa kuelewa lakini kama nilivyosema ikiwa kama unalijua vema Somo la Viumbe Hai baada ya High school(ambayo mie sikuipata hii ni another sitori ya siku ingine) utaelewa. Vitendo vya kimapenzi au upendo ambavyo Mama alitupatia baada ya Kuzaliwa na kipindi tunakua ndivyo ambavyo tunavifanya au tunapenda kufanyiwa na Wapenzi wetu tukiwa watu wazima kwa......mf kunyonyana Chuchu, kukumbatiana, kupeana mab

Kuangalia na kujaji matako ya watu...!

Well sio watu wote bali Wanawake....halafu unacheka....i do! Sidhani kama ni tatizo au tabia hii inanifanya nionekane Msagaji hihiiihihi.....(ngoja nijihami kabla hujaendelea kunijaji).....hapana sina hisia na wanawake wenzangu na wala siwatamani. Nikiwa natembea kwa miguu lazima nitakuwa naangalia makalio ya yeyote aliembele yangu na kulijaji tako lake halafu kama linachekesha basi nacheka. Tena matako ya Wazungu ndio yapo ya sampuli nyingi tofauti.....ujue sisi Waafrika(well Watanzania as sijawahi nzunguuka Bara zima la Afrika)...matako yetu ni ama yapo kwamba makubwa au ya wastani na yamejitokeza au hayapo yaani bapa.....hakuna ile eneo la tako kubwaa na bapa halafu kijitako kinajitokeza kiduchu kwa chini. Au ni kwasababu Tanzania wengi hawavai Leggings sijui jeggins na viblauzi vifupi? Mmmh ukijifunga Khanga shape ya tako inaonekana so sidhani. Hao ni wanawake. Linapokuja suala la Wanaume binafsi napendezwa na wanaume ambao ni Bapa. Mambo ya kukamata tako kubwa la mumeo n

MakeUps zinaharibu Ngozi ili uzitegemee?

Biashara ya Vipodozi inapamba faya mwaka hadi mwaka asante Beauty Gurus wa Youtube.....hata mie mpaka Mascara na lipgloss nimeanza kujipaka Foundation siku hizi(well nimeanza kupaka tangu 2004). Enzi hizo mie napaka ilikuwa haiitwi Faundation bana, ilikuwa inaitwa cream to powder au mimi ndio nilikuwa sijui?hihihihihi. The thing ni kwamba most Gurus (nakojifumzia kupaka make up) ngozi zao kama vile haziko sawa. Yaani kuna mmoja siku nilivyomuona bila make up (mambo ya GRWM as in get ready with me) nilaogopa kuendelea kuangalia.....sio kwamba anatisha la hasha! Niliogopa kusikitika na kulia (tangu mekuwa mama nimekuwa way too emotional). Sasa ni mpango wa make up companies kuweka Viasili vya kuharibu Ngozi asilia ili uendelee kununua bidhaa zao na kuficha uharibifu uliopo Ngozini? Najiuliza. Au ni kutokujua kwa baadhi ya watu na hivyo walikuwa hawasafishi Ngozi na kulala na makeups? Pengine ni matumizi ya Vipodozi aka Makeup wakatu ngozi bado haijakomaa? Unajua kuwa Ngozi ni

Kupenda watoto wa watu.

Mawifi na marafiki wa Kike wa mumeo ndio viongozi wa kujifanya wanapenda watoto wa watu. Utasikia "aah jamani waambie nawapenda sana"......mie najibu kimoyo-moyo, unauhakika unawapenda wanangu? Ukikaa nao wiki tu utabadilisha mawazo.....they are hard work! Mimi ni Wifi na Shemeji pia lakini sijawahi kusema nawapenda Wapwa zangu.....ninahisia nao nafurahi kuwaona na kuongea nao lakini siwezi kusema nawapenda wakati sijawahi kuishi nao. Uwazi wangu kuhusu hisia za kupenda watoto wa watu hufanya baadhi ya watu kusema kuwa nina roho mbaya kwamba nachukia watoto. Mie sijui kudanganya kuwa nawapenda wanao wakati najua wazi moyoni hawapo. Nachukulia watoto wote kama watoto na sipendi waonewe au wateseke na hilo ni muhimu zaidi kwangu kuliko kukudanganya kuwa nawapenda. Kwasababu tu ni mtoto haikufanyi automatically umpende.....nilikuambia kwenye moja yabpost zangu, baada ya kuzaa wanangu sikupata ile hisia ya kuanguka kimapenzi kwa mara ya pili na ya tatu baada ya Baba y

Malezi kwa Culture ya Ughaibuni....

Ni kawaida kwa baadhi ya watu(nilikuwa mmoja wao) kushangaa na kuwashutumu Wazazi wa kitanzania waishio Ughaibuni kuwa "wanaiga" na wanalea watoto wao "kizungu" na kusahau au kutojali Kacha yao. Unapomzaa mtoto London kwa mfano na mtoto huyo kuendelea kuishi huko maisha yake yote unategemea mtoto huyo atakuwa na Kacha ya kwenu? Mazingira, Vyakula na Mtindo wa maisha ya wanajamii yanauo mzunguuka ni ya Kacha  ya Nchi husika alikozaliwa na anakulia hivyo sio sahihi "kumpinda" afuate Kacha yako wakati yupo kwenye mazingira tofauti na yale uliyokulia wewe huko kwenu ulikotoka. Mtoto husika anakuja Tanzania mara moja kwa Mwaka na kukaa huko kwa wiki 2-3 na unategemea akue kama wewe na kufuata kacha yako? Ni vema na muhimu kuendeleza values zako na kuwaeleza watoto tofauti ya Kacha yako na Kacha yao lakiji sio kuwalea Kisarawe wakati wanaishi Kent. Just because wamezaliwa na Mtanzania na wao wanautanzania sio lazima wafuate Kacha ya Kitanzania. Jin

Stop....Africa is NOT a Country.

Mtukome...... Wamarekani ndio zao....sijui hawakuwa na waalimu wa Jiografia. Wakija UK wanasema wanakuja EU.....wakienda Tanzania wanasema wapo Afrika. Mbona Canada hamuirifai kama America au Marekani ya Kaskazini? Humkuti mtu kutoka Bara la Ulaya anarifaa Nchi yake kama Ulaya....atakuambia moja kwa moja yeye anatoka wapi. Afrika ni Bara sio Nchi. Halafu waafrika wenyewe ndio mamwehu kabisa yanaona raha au sijui sifa au aibu ku reffer Nchi zao walikotoka na kuishia kusema Afrika....."back home in Africa nlanlanlaaaa". Sema Nchi yako kama hawaijui waambie wakaGUGE......acheni kutufanya as if Waafrika wote tupo sawa. Nchi yeyote iliyotawaliwa na Muingereza inafuata mambo fulani ya Kiingereza.....kuna Tamaduni tume-adopt na kufanya zetu....mfano Ukristo, uvaaji wa nguo na baadhi ya Uendeshaji wa shughuli za Kimahakama bila kusahau sheria. Hii ndio faida pekee ya Jumuiya ya Madola(in my head). Halikadhalika waliotawaliwa na Mreno....Mwarabu....Mjerumani au Mfaransa

Kwanini___haonyeshi mtoto wake?

Hujawahi kujiuliza kwanini huyu fulani anapenda kuzungumzia mwanae lakini hajawahi kuweka picha ili na mimi angalau nipate picha ya alivyo kila anapomzungumzia. Well shauri yako ila najua mie nimeisha jiuliza to the point napata hasira(hihihihi sio hasira bali whys lundo). Kuna dada mmoja (enzi zile bado nipo kwenye social media) alikuwa ana-share mengi wakati wa Mimba....alimalizia na baby shower na habari ya mtoto kuzaliwa halafu ndio ukawa mwisho.....akawa anamzungumzia tu na kushare zawadi alizompatia kwenye Siku ya kuzaliwa n.k....mapaka leo sijui sura wala rangi ya mwanae......sio muhimu kihivyo lakini muhimu. So kama mimi enzi nilikuwa nahisi hivyo hakika hata wewe ungependa kuona sura za wananhu si eti eeeh. Nili-share picha kiasi nilipokuwa kwenye Sosho media so walionifuata wengi wanakumbukumbu kwa mbali ya wanangu walivyo japo sasa wamekua mmno. Kuna sababu nyingi zinazofanya watu kuzuia picha za watoto wao kuzagaa mitandaoni hasa kama wazazi ni maCeleb..... .....maana