Skip to main content

Posts

Miaka 30 ndio mwisho wa kutaja Umri wako...

Kwa mwanamke.....habari za Masiku tele? Ahsante kwa kuichagua Blog hii. Nilipojuja Nchi hii miaka zaidi ya 10 nilikuwa kwenye my early 20s na nilikuwa nasafiri kama mtoto....sio nilifoji la hasha! Wakata Tiketi waligoma kukubali umri wangu na wakasema mie ni binti wa miaka 15yrs. Nilinilikuwa nakaa Kijijini halafu nasoma London) na Kiingilishi changu cha kudandia akuu mkidada wala sikubisha so nikakata Kibali cha Usafiri kama mwanafunzi wa Kimataifa wa Miaka 15 ambacho ni Chee. Enzi hizo (2000s) hakukuwa na mambo ya kufuatiliana kwenye Passport. FAST FOWARD....nikawa na Mume ambae anakunywa Pombe, nikienda nunua Pombe wanagoma kuniuzia eti mpaka niwe na Miaka 25 hihihihi. Nikiwaambia mie ni mama wa watoto 2 na nipo in my 30s wananicheka na kunambia a 23yr old woman can have a child too so wanaomba  niwaonyeshe kithibitisho cha umri(Driving License) nawaonyesha.....misamaha mingi ikijumuishwa na hongera kwa kuluku so yang'i. Au kwa maana nyingine am a 23yr old who look like a

Usafi na Kinyaa....

Ni vitu mbili tofauti....Natumai umeamka/shinda salama. Mtu kuwa msafi haina maana ana kinyaa na mwenye Kinyaa sio kwamba ni msafi pia....japokuwa wapo wasafi na wanakinyaa pia(mie).....hivi ni kinyaa au uoga wa kupata maambukizo? Nakumbuka nilipokuwa nakwenda Hospitali kwa matibabu au kumtembelea Mgonjwa....nilikuwa naumwa kichwa balaa. Nikitoka tu maeneo ya Hospitali napona. Natabia ya kubana Mkojo kwa muda mrefu(usijaribu hii ila kama ni mtu wa Kuendiketa poa) ili nisitumie vyoo vya wote(public)....Haja kubwa (sorry 4 TMI)huwa haiji nikiwa kwa watu au nje ya kwangu/kwetu.....hii sasa ni Saikoloji issue. Jana nimetoa siri yangu kwa Asali wa Moyo kuwa tukienda kwa watu(ndugu zake incl) huwa siogi wala kutumia vifaa vyao vya kujisafishia. Nitafungua Shower vema tu au kujaza Ndoo maji(inategemea nipo wapi) na kuacha shower iendelee au kumwaga maji as if naoga kumbe nanawa miguu...hihihihi. Badala ya kucheka akabaki kaduwaa hehehehehe well sina siri tena maana hata wewe msoma

Kiswahili Kigumu....spesho Post kwako!

Heyaaa. Ahsante kwa kuichagua Blog hii. Naona Idadi inaogezeka kila siku. Hi wa USA...How do you do wa hapa nilipo....jambo Afrika Mashariki.....Hello wengine wote popote mlipo Ughaibuni. Tambua kuwa ninathamini ugeni na ukazi wako wa muda mfupi au mrefu(unaposoma).....natumaini naweka makunyazi usoni kwako ama kwa kutabasamu au kwa kukunja sura. Umewahi kuamishwa(na Gugo) kutoka Kiinglishi kwenda Kiswahili halafu ukashindwa kuelewa....yaani unachanganyikiwa na hujui nini kina maanisha nini? Kwasababu ninablog kwa Kiswahili mara nyingi Gugo wananijaribu kutumia Blogger kwa Kiswahili ambayo siielewi. Mara chache nasoma Blog za Kiswahili kama vile http//www.tech255.com , www.bwaya.blogspot.com (simu haniruhusu kuweka link so yeah copy and paste uone waandikacho)na nyingine za Kuelimisha. Huko pia huwa nachanganyikiwa na kutokuelewa baadhi ya maneno ambayo nadhani ni mapya. Ila tofauti ni kuwa yapo kwenye sentensi hivyo inanirahisishia kuelewa Mwandishi alimaanisha au anamaanisha n