Skip to main content

Posts

Kupoteza Nywele baada ya Kujifungua....update!

Ni Mwaka na Miezi kadhaa tangu nikusimulie kuhusu Nywele zangu za kichwani ambazo ni Relaxed(bila shaka). Sasa, tangu tunamaliza Mwaka nimeona sio mbaya kama niki-share safari yangu ya kuwa na Nywele  tena zenye urefu wa kutosha kutengeneza mitindo na pia zenye afya. Halafu sio mbaya kama nikikutajia/nikionyesha Bidhaa ambazo zimenisaidia kufika hapa nilipofikia. Vilevile nitakuambia ni Bidhaa gani natumia lini na kwa nini(kwenye post nyingine) na nitaambatanisha Picha. Pamoja na kusema hayo ni vema utambue kuwa Bidhaa hizi hazikuhakikishii matokeo kama yangu, inaweza kuwa bora zaidi yangu au usione mabadiliko yeyote. Baadhi ya Bidhaa hizi nilikuwa natumia kitambo, baada ya kuhangaika na kujaribu aina nyingine na kutofanikiwa nikaamua kurudi kwenye bidhaa kutoka Vitale, Nikaamua kutumia "Steamer" na "Blow dryer". Awali nilikuwa situmii Heat kabisa kama nilivyoshauriwa na Gurus. Baadae nikagundua kuwa Nywele zangu zinapenda Heat so nikarudia utaratibu w

Single Mum/Loner Parent, Mzazi Mmoja=no Help

Hi! Sitojifanya mjuaji kwenye hili, tangu sijawahi kuwa "single mother" iwe kwa kutaka (wale wanaoamua kushika Mimba bila kuwa na hitaji la mwanaume husika) au kwa bahati mbaya, kwamba kutofautiana kwenu kumefanya mmoja wenu abaki na mtoto/Watoto(hapa siwazungumzii Wajane au wale waliobakwa, hii ni issue nyingine). Ninaowagusia hapa ni wale ambao kuwa "single mother" ni Mtindo wa Maisha,Sifa, chanzo cha kuonekana Imara/Unaweza! Wengi hapa ni wale Wasichana waliokulia miaka ya 90s na wale wa early 2000s. Ule msukumo wa kutaka kujitegemea ukikuwa na "impact" kubwa kwetu kiasi cha kuhisi hatuhitaji Wanaume ili kuwa na Familia. Tuliamini kuwa tunaweza kufanya yetu kama Wanawake na tunaweza kufanya ya Wanaume pia, "ikiwa mwanaume anaweza hata mimi naweza" sort of Imani....hakika hakuna afanyacho Mwanaume ambachoo sisi hatuwezi kufanya, lakini kuna mambo ambayo hatuwezi kuyafanya kama Wanawake kwenye malezi ya Mtoto au watoto(h

Kukosoa na Kumcheka mtu ni "interest" yako?

Nakuona! Wengi huamini kuwa ukiwa na tabia ya kukosoa au kucheka watu wengine basi wewe utakuwa na Matatizo kwenye Maisha yako, maisha yakoo hayana furaha na yamejawa na Huzuni na hivyo kukosoa na kucheka watu ndio njia pekee ya kujipatia "furaha". Nakubali kwa kiasi fulani, kwa baadhi kuwa Hasi kwenye kila kitu  ni tatizo na linaathiri maisha yao ya kila siku. wengine huamua kuwa Hasi kama sehemu ya kupata "attetion" au "Trafic" na "Views" popote walipo kwenye Sosho Midia. Kwa wale wa Ughaibuni, Maisha mitaa hii yanaweza kuwa ya Upweke sana na hivyo kumfanya mtu kutumia muda wake mwingi kwenye kutafuta "furaha" kwa kuwa Negative towards watu wengine. Upweke wa huku unatokana na utofauti wa Kitamaduni, Utaratibu wa kazi za "shift",  Majira ya Mwaka(Kiza kuingia mapema) vilevile kutumia muda mwingi kusafiri to na from work....by the time unafika nyumbani upo hoi, tayari ni Giza hivyo  hakuna muda wa kutoka au kukarib