...hivi YouTube inahesabika kama Sosho Midia? Kama sio basi Platform pekee naiaga kwa sasa ni Twitter. Sijawahi "kujiunga" na Instagram, Snapchat wala Tiktok. Kwanini? Ukiachilia mbali kuwa Muda unabadilisha watu(wanakua), vilevile vitu na mitazamo hubadilika kulingana na Tabia Uchumi/Nchi/Utamaduni....nadhani Twita imejaa wafanya Biashara kwa kupitia Ajenda binafsi/Harakati, Biashara ndogo ndogo na Biashara Utapeli (ulipie waliojifunza YouTube bure), Biashara ya Miili(intimate picha/vid) oh bila kusahau Biashara ya "kuomba omba". Baada ya miaka kadhaa, nimegundua kuwa Twita hainifaidishi kwasababu sina Biashara(sikuzi Brand), hivyo sihitaji kuwa active na ku-engage na followers few hours on daily. Kabla ya hapo nilikuwa Active sana kwenye Masuala ya Kisiasa(Naunga Mkono Upinzani Tz), baada ya Muda nikajitoa, uamuzi uliopelekea "kurukia" zaidi issues rahisi rahisi ambazo zimejaa chuki/vita ya Wanawake vs Wanaume, hasira, kutokujiamini, kukat
Kila Mwanamke ni Imara hiyo inajilikana na wala huitaji kujitanganza(kuwa chini ya Kundi fulani kuthibitisha hilo), pamoja nakusema hivyo wewe kama Mke bado ni Dhaifu/laini(Kimwili) na hakuna kosa mkimama kuwa mlaini(jivunie udhaifu wako). Kazi yako kubwa Duniani ni kuwa msaidizi wa Mumeo, kuleta uhai(kubeba Mimba na Kuzaa), kulea, kufundisha na kutunza Familia. Ili uweze kufanya hayo(niliyoyatajabhapo juu) unatakiwa kuwa umejitolesha kwenye nyanja nyingine ili kurahisisha Maisha yako kama Wewe, Mama na Mke. Unapaswa kuwa na uwezo wa kufanya baadhi ya vitu haraka na kwa ukamilifu bila uwepo wa mtu wa pili iwe Mumeo au Muuza Huduma. Je ni nyanja gani hizo? Dharura; Unaweza kujituliza, kutafakari kwa haraka na kufanya uamuzi kwa faida yako na familia badala ya kusubiri mpaka Mumeo apokee Simu/arudi. Uchumi; kuwa na Akiba ya Senti kwa mahitaji madogo madogo(ya ghafla) nje ya Bajeti ya Familia(kutoka kwenye zile anazokupa Mumeo), sio kila akikupa Pesa unatumia zote kwa wa