Skip to main content

Posts

Showing posts from May 3, 2015

Tuepushie Bunge la Kuheng'i....

...na tuepushie huyu wa sasa....amen!  Natumai Kura yangu itaongeza palipopungua 2010. Heyaaa! Kuna wiki moja huwa inakuwa busy sana na appointments kuliko.....Dentist....Chanjo kwa Kibibi....kuongezea Chanjo kwa Babuu....manunuzi ya viwalo vyao vya summer. Wengine (mimi) tunanunua nguo Sikukuu to sikukuu. Unafanya kubadilisha Makoti na Majaketi ya Miaka 2 iliyopita.....sio kila Majira ya mwaka yanavyobadilika mweee. Halafu mtu anakuambia "hutaki kuzaa kwasababu unaogopa maisha".....no dear naogopa gharama. Well ukiachilia habari ya kukujulisha kwanini sijapost kwa muda kiasi, ni kwamba huu uchaguzi wa Leo unanipa Presha kimtindo. Naenda kulala ili niweze kufuatilia matokeo kuanzia saa Tatu(Tano tz). Ahsante kwa kuichagua blog hii. Babai.

The Online Support....kwa Celebs!

Hata kwa sie ambao sio maCeleb is real.....unajua pale unapoungwa mkono na kupewa ushirikiano wa "kisaiba"(cyber) na kukufanya ujihisi umebebwa....unapendwa...unakubalika. Unahisi furaha na pengine kujiona Mashuhuri(mtu wa kawaida) au kuhisi Umashuhuri wako (kwako Celeb) umeongezeka na kupata Konfisensi ya ajabu ya kufanya lolote au chochote. Unajua ile umeweka Picha halafu unapata followers zaidi na wanakumwagia masifa.....wanaomba kuona zaidi na wewe unazimwaga picha za mapozi tafauti hihihihihi baada ya siku mbili wanakuja followers wapya(wale wale kwa account tofauti via device tofauti) na kuanza kukuponda.....unabaki kulia na kuita watu "fake friends". Inategemea ni nini hasa kimefanya upate support ya "Fanzi" aka followers wako Online.....kuna wakati unahisi kutaka kusema ukweli wako ulivyo na sio uongo wausikiao au ku-justfy na ku-share zaidi ya unachopaswa kusema/ku-share. Bila kuomba ushauri kutoka kwa "inner self" au bila kumsikili