Skip to main content

Posts

Showing posts from April 6, 2014

Ugomvi wa Ndugu...

Sie tuliozaliwa wengi (zaidi ya wawili) huwa hatuoni umuhimu wa attention ya wazazi wetu....labda kwavile hatukupewa au tulipokuwa tukihitaji kwa vile kulikuwa na Kichanga. Tuliihsia kuambiwa "acha kudeka" na kofi juu. Na baadhi yetu tuliishia kulea wadogo zetu ambao walihitaji attention zaidi yetu wakati Mama na Baba wako busy na mambo yao mengine kama sio kutengeneza mtoto mwingine. Tunapenda kuwamwagia sifa kutokana na malezi yao mema kwetu na kutangaza ni namna gani tunawapenda na baadhi hudai wazazi wao ni mifano mizuri kwao (good role model)! Wakati mwingine ni kweli ni "good role model" lakini mara nyingi ni Hatia moyoni inakufanya udhani kuwa walikuwa wazazi bora na wanafaa kuigwa....si unajua the "bila wao nisingezaliwa au kusomeshwa" sort of guilt..... Well (1)-Uamuzi wao kukuzaa (hukuomba kuzaliwa) + (2)- ;ukumu lao kuhakikisha unaishi vizuri na unapata Elimu hivyo wacha kuhisi hatia. Kuna mahali w

Pale 40something anaposhindana na 20something....

Kwa hamu nasubiri siku nitakayofikia miaka 40(God willing) ili namie nijisikie kama wanavyojisikia waliogonga hiyo namba. Natumaini Botox itakuwa imeshuka bei by then, maana Viganja kwa nyuma vinamakunyanzi ka' Bibi yangu wa miaka 90. Wengi huamini kuwa miaka 40 ndio Uzee ila nadhani Tz mwanamke akifikisha miaka 30 huitwa Mzee.....Mtukome....Mzee Mama yako (hii imetoka mchicha ka tusi eti?) Well, namaanisha mwanamke aliekuzaa ndio Mzee. Celebs waliofika Umri huo wa miaka 40 hujisifia kuwa wanajisikia kama walivyokuwa kwenye umri wa miaka 20s ila tofauti ni kwamba sasa wanajijua, wanajiamini, wanajua watakacho nakadhalika.... .....well inawezekana kabisa sio kweli ila ni mikakati ya kutaka kuendelea "kuonwa" kijana. Hakuna haja ya kuendelea kufanya uliyoshindwa kuyafanya enzi zako za Yahoo na Hotmail, relax na uwaache watoto wa 20something wafurahie Era yao. Tunafanikiwa sana kuficha au kudanganya Umri lakini sura siku zo

Tunapenda kufanana...

Heri ya Alhamisi.... Katika kupitia Vlogs (nilikuwa nanfanya uchunguzi kuhusu nywele) nikagundua kila chumba au Vanity room (where they film) vinafanana....Nikatafuta ukweli kwanini wote wanafanya hivyo? Nikagundua chanzo ni Kadashianzi. Mara nikakumbuka watu wa kawaida tu kwenye jamii pia hupenda kuigana kuanzia Nyusi, Fashion mpaka mapambo ya nyumba/ndani....Blogs na Sauti (bwahahahaha) Najua kwa baadhi ya watu ni muhimu kufuata "trends" na hivyo kufanya kama wanavyofanya wengine.....kama inakupa furaha maishani why not eti? Dressing table yangu ni ile ya kizamani, kabati upande mmoja, chini na juu droo katikati kioo chenye kijisehemu cha kuweka Manukato, Wanja n.k!...Vanity/Dressing Room? Aii only in Amerika na Kanada (majumba yao makubwa) or Mamilionea wa Bongo na Ulaya.... Tangu nilipokuwa Mdogo nilikuwa sipendi kufanana na watu wengine, si unajua midosho nini na nini....Dar combine...hihihihihi. Ndani kwangu hakuna Picha ukutani k

Changudoa...

Kwa kawaida jamii hushupalia ikiwa mhusika au wahusika ni Wanawake. Tena wanawake wenyewe ndio wanaongoza kuwakandamiza Machangudoa. Katika hali halisi Machagudoa hasa kwenye maisha ya Chuoni ni kitu cha kawaida, haina maana mimi nimewahi kufanya hivyo bali kuna wake kwa waume niliosoma nao walikuwa wakifanya kazi hiyo ili kujimudu. Siungi mkono kazi yao na wala sipingi kwasababu sijui ni circumstances gani(ukitoa tamaa ya high life) zimepelekea wao kufanya uamuzi huo huko Nchi za watu.... Tambua tu kuwa wanaume pia wanafanya Uchangudoa Nchi za nje na sio Wanawake pekee. UK ya leo sio ile ya Tony Blair na kama UK maisha magumu huko kwingine si ndio basi tena (in my head). Kwenda "Majuu" is not as cool as it used to be....ndio maana watoto wa Vigogo siku hizi hawaendi Nje (hawaishi Nje), wanafungua mabiashara makubwa au wanakuwa Wanasiasa..... Uanasiasa na kumiliki Biashara yenye mafanikio is new Cool. Kwaheri kwa sasa.

Uchungu wa Kuzaa + Kujizuia usi-Push = Near Death

Mimba ya mwanangu ya Pili Iman haikuwa enjoyable + alipitiliza. Mkunga kanaipangia siku ya kuwa "induced" ili nipate Uchungu. Binafsi sipendi vitu ambavyo sio asili kwenye mwili wangu na hakika sio Uchungu, pia ni Mpinzani wa kuzaa kwa. C-section. Kwabahati nzuri (Mungu alijibu maombi) Asubuhi ya kuwa induced "chupa" imepasuka, nikawapigia simu wakunga wakasema wanajiandaa kunipokea wakati wowote. Mimi being mimi, nikasema nitavumilia mpaka maumivu yachanganye ili nikifika tu Hospitali nijifungue....maana kwa Barack ushamba/kutokujua tulienda Hospitali mapema....uchungu ukachanganya Saa saba....Lol! Anyway, nikapata uzoefu mpya sasa....kama unadhani Uchungu wa Kuzaa ni kamambe!!....Usiombe Kuumwa uchungu huo + juhudi za kuzuia mtoto asitoke. Mambo yakaenda vizuri, Uchungu unakuja unarudi....ikafika saa Kumi na mbili Jioni, mara booom! Mtoto namhisi huyu hapa....naita baba mtu, kusanya Barack....hao garini. Najisemea &q

Nywele....

Baada ya kujifungua Barack na kupoteza nywele za kutosha, nikavumilia mpaka nilipomaliza kunyonyesha. Niliposhika Mimba ya Iman nikaamua kukata nywele hivyo nimekuwa na nywele fupi kwa miaka 2. Siku moja nika-google kujua "Tiba" ya nywele zangu "kumwagika" kutokana na kunyonyesha(mabadiliko ya Homono). Nikakutana na Vlogs za hair journey bana...hee! Nikagundua mafuta yanaitwa Castor (mafuta ya Nyonyo) mwanamke si nikakurupuka....nikawa naosha nywele kila siku na kupaka Mafuta ya nyoyo + leave in + hair cream za kutosha, Wacha nywele ziendelee kukatika mpaka nikawa kipara hihihihihi (I was crying actually). Nikaendelea kufanya Uchunguzi kwa kusoma na kusikiliza Shuhuda za watu nikagundua kuwa nakosea na nywele zangu zilikuwa zinalainika zaidi(too much moisture) bila kupata nguvu kutoka kwenye Protein (nywele zinahitaji balance ya vyote). Ndio nikakutana na wadada wakitoa shuhuda kuhusu Aphoghee Step 2 treatment ambayo unatu

Matumizi ya Tablets kwa watoto....

Mambo! Nitakuwa naandika chochote kinachonijia kichwani kwa wakati huo.....kuanzia malezi ya wanangu, habari itakayogusa Mtima wangu (usijali sio habari za Tz) na siku husika kwa ujumla. Hali ya hewa leo ni ya Unyevu na Mvua kwa mbali, Wataalam na wachunguzi wa huku wanalalama kuwa watoto wasitumie Tablets kwa vile zinawafanya wasiweze kutumia mikono kuandika au kuchora kama ilivyokua kwetu enzi zile. Lakini Enzi zetu si zimepita? hizi enzi zao waacheni ila tuwe responsible na wanachokifanya kwenye Tables, Fundisha mwanao....usitegemee mtu mwingine (Yaya/Mwalimu) akufundishie just because you pay them to do so. kwaheri kwa sasa.