Skip to main content

Posts

Showing posts from May 18, 2014

Kujiremba....

Kipajiiii....heri ya Alhamisi! Nilipokuwa Msichana 10-17 sikuwa najali mambo ya kujiremba....Mama hakuturuhusu kupaka Rangi ya Kucha Ijumaa kisha tuondoe J'pili jioni. Eti tulikuwa tunaharibu Rangi zake... Basi tukawa tunapaka Wino mwekundu(Pen nyekundu) au ukitaka Rangi "clear" au kucha zing'ae basi unachukua Marumaru au Vipande vya China (sahani, vikombe n.k vilivyovunjika) unasugua kwenye Sakafu ya Sementi kisha ile vumbi yake unaisugua kuchani. Nilipofikia Miaka 18 nikaanza kupaka Wanja na Lip gloss. Nimeanza kujipangusa Poda usoni, kutinda Nyusi na kupaka Mascara nilipokuwa na miaka 28....anyways! Baada ya kuwa addicted na Beauty Vlogger nikaamua kujitutumua kwenye kujiremba bana....basi siku ambayo najua sitoki nje mwenyewe napanga nitakavyo vyaa the next day na Vipodozi gani vya kujipaka....(Ninavyo kibao kwani kila Birthday napewa zawadi ya Vipodozi....watu wachokozi)! Naamka mapema, nafanya shughuli zangu za ndan

Mti/Ua Shamba....

Yenye viwango na Uchunguzi wake umefanywa kisasa.....(Wataalam wa Sayansi) sio wale wa "Maono"....The wezi. Oh! Heri ya Juma Nne....Hongera na ahsante kwa kuichagua Blog hii. Ile Nywele issue (bado ninayo) bana inanifanya nijifunze mengi kuhusiana na vitu asilia ambavyo vinamanufaa mazuri kwa mwili wa Binadamu ikiwa ni pamoja na nywele. Kunywa maji ni muhimu kwa ajili ya ngozi, nywele na kupunguza Mafuta Mwilini kwani inakuzuia kula chakula kingi/kupita kiasi.....ila ukiwa ulibeba mtu mbili Tumboni eh bwana lazima uwe mwangalifu na maji unywayo. Unakunywa "Fundo" ndogo mbili na sio kumimina robo/nusu Lita kwa wakati mmoja....unaeza pata Mimba atifisho a.k.a Kitambi....(Hata sijui kwanini nakuambia hili)! Oooh! Back to Miti shamba, ninayotaka kuizungumzia hapa ni Chai.....huyoo ulidhani mizizi na Magome? Hehehehe....Chai ya Kijani na ile ya Maua aina ya Chamomile. Come to think of it, Mizizi na Magome hutumiwa kama

Mabadiliko ya Ngozi

Naamini au niseme kuwa nadhani nina ngozi nzuri, kwamba si nyeusi na si nyeupe. Ila tatizo linakuja kwenye mabadiliko yake kutokana na Hali ya hewa inavyobadilika. Awali wakati naishi Tanzania ngozi yangu ilikuwa inachukia Mafuta Mazito, hivyo nikawa napaka mafuta ya "maji" ya asilia ambayo ni ya Nazi. Baadae nikagundua aina fulani ya "Lotion" nikawa nachanganya Mafuta ya Nazi na kupaka mwilini (usoni incl). Kipindi chote hicho sikuwa naona mabadiliko ya Rangi ya Ngozi yangu kama ninavyoiona huku Ulayani. Yaani wakati wa Baridi na kipupwe Ngozi yangu inakuwa Nyeupe (napauka)....alafu wakati wa Kiangazi naiva (Rangi inakolea).... Nikadhani labda macho yangu yanaumizwa kutokana na Mwanga wa jua wakati wa Kiangazi ndio maana najiona "nimeiva). Siku nikaenda kwa Daktari kumueleza tatizo langu hehehehehe I know(am so stupid....not really mie muoga wa Magonjwa bana)....nilidhani labda ni dalili ya Ugonjwa wa Michael Jac