Skip to main content

Posts

Showing posts from March 1, 2015

Stop....Africa is NOT a Country.

Mtukome...... Wamarekani ndio zao....sijui hawakuwa na waalimu wa Jiografia. Wakija UK wanasema wanakuja EU.....wakienda Tanzania wanasema wapo Afrika. Mbona Canada hamuirifai kama America au Marekani ya Kaskazini? Humkuti mtu kutoka Bara la Ulaya anarifaa Nchi yake kama Ulaya....atakuambia moja kwa moja yeye anatoka wapi. Afrika ni Bara sio Nchi. Halafu waafrika wenyewe ndio mamwehu kabisa yanaona raha au sijui sifa au aibu ku reffer Nchi zao walikotoka na kuishia kusema Afrika....."back home in Africa nlanlanlaaaa". Sema Nchi yako kama hawaijui waambie wakaGUGE......acheni kutufanya as if Waafrika wote tupo sawa. Nchi yeyote iliyotawaliwa na Muingereza inafuata mambo fulani ya Kiingereza.....kuna Tamaduni tume-adopt na kufanya zetu....mfano Ukristo, uvaaji wa nguo na baadhi ya Uendeshaji wa shughuli za Kimahakama bila kusahau sheria. Hii ndio faida pekee ya Jumuiya ya Madola(in my head). Halikadhalika waliotawaliwa na Mreno....Mwarabu....Mjerumani au Mfaransa

Kwanini___haonyeshi mtoto wake?

Hujawahi kujiuliza kwanini huyu fulani anapenda kuzungumzia mwanae lakini hajawahi kuweka picha ili na mimi angalau nipate picha ya alivyo kila anapomzungumzia. Well shauri yako ila najua mie nimeisha jiuliza to the point napata hasira(hihihihi sio hasira bali whys lundo). Kuna dada mmoja (enzi zile bado nipo kwenye social media) alikuwa ana-share mengi wakati wa Mimba....alimalizia na baby shower na habari ya mtoto kuzaliwa halafu ndio ukawa mwisho.....akawa anamzungumzia tu na kushare zawadi alizompatia kwenye Siku ya kuzaliwa n.k....mapaka leo sijui sura wala rangi ya mwanae......sio muhimu kihivyo lakini muhimu. So kama mimi enzi nilikuwa nahisi hivyo hakika hata wewe ungependa kuona sura za wananhu si eti eeeh. Nili-share picha kiasi nilipokuwa kwenye Sosho media so walionifuata wengi wanakumbukumbu kwa mbali ya wanangu walivyo japo sasa wamekua mmno. Kuna sababu nyingi zinazofanya watu kuzuia picha za watoto wao kuzagaa mitandaoni hasa kama wazazi ni maCeleb..... .....maana