Mtukome......
Wamarekani ndio zao....sijui hawakuwa na waalimu wa Jiografia. Wakija UK wanasema wanakuja EU.....wakienda Tanzania wanasema wapo Afrika.
Mbona Canada hamuirifai kama America au Marekani ya Kaskazini?
Humkuti mtu kutoka Bara la Ulaya anarifaa Nchi yake kama Ulaya....atakuambia moja kwa moja yeye anatoka wapi.
Afrika ni Bara sio Nchi. Halafu waafrika wenyewe ndio mamwehu kabisa yanaona raha au sijui sifa au aibu ku reffer Nchi zao walikotoka na kuishia kusema Afrika....."back home in Africa nlanlanlaaaa".
Sema Nchi yako kama hawaijui waambie wakaGUGE......acheni kutufanya as if Waafrika wote tupo sawa.
Nchi yeyote iliyotawaliwa na Muingereza inafuata mambo fulani ya Kiingereza.....kuna Tamaduni tume-adopt na kufanya zetu....mfano Ukristo, uvaaji wa nguo na baadhi ya Uendeshaji wa shughuli za Kimahakama bila kusahau sheria. Hii ndio faida pekee ya Jumuiya ya Madola(in my head).
Halikadhalika waliotawaliwa na Mreno....Mwarabu....Mjerumani au Mfaransa wanafuata Tamaduni za Nchi Tawala.
Pamoja na kuwa tuna baadhi ya vyakula sawa....utagundua upikaji na Ulaji wetu unatofautiana.
Pia maumbile yetu ni tofauti....tabia zetu ni tofauti....uchangamfu na wepesi wa akili na utendaji ni tofauti.
Wenyewe tu ndani ya Tanzania tumetofautiana depends na Kabila....Mf Wapemba na Wachaga wazuri sana kwenye Biashara kuliko wale wa Kagera ambao ni wazuri kwenye Kitabu na majivuno.
Tabora wapo vizuri kwenye nanilihu....Academically lakini wavivu kimaendeleo.....majungu....misifa na wanapenda kukimbia Mkoa wao (wahamiaji wazuri) kuliko Wazaramo ambao sio wazuri sana Academically lakini wazuri kwenye suala la kuendeleza ardhi.....Mzaramo bana kumiliki Kibanda ni muhimu. Umewahi sikia msemo kuwa "mzaramo halali njaa"?
Wale wa Sinza (is Mkoa now au)ama wanalelewa na KugaZ au ni Vimada (hihihihihi)....no offence intended.....niliipata hii nilipokuwa Morogoro(siku nikikumbuka ntashea).
Sasa ikiwa ndani ya Tanzania tunatofautiana mpaka Desturi iweje muirifae Afrika kama nchi wakati tunatofautiana kidesturi n.k?
Kesho basi au vipi?
Comments