Skip to main content

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case.


Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo!

Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie!


Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*.


Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi Mazoezi, Haipati Hewa wala Mwanga wa Jua + unapenda sana kukaa chini*.


Sasa mwanamke(na mwanaume) fanya yote ambayo ni kinyume ya nilichosema hapo juu. Najua unajiuliza utapataje Jua makalioni eti?!!


Sio lazima ukayaanike makalio yako Juani kila mtu ayaone bali vaa Khanga bila Chupi(mwanamke) na Msuli/Pensi nyepesi bila kitu ndani (mwanaume) kisha simama Juani kwa muda kiasi.


Rangi tofauti Kwapani: Inasemekana Weusi huo hutokana na "kinga" ya Ngozi ya sehemu hiyo ku-over work ili kuzuia. Madhara ya Mionzi ya Jua....ndio maana hata ukiichubua inaendelea kuwa Nyeusi mpaka "kinga" ya Ngozi yote iishe ndio Kwapa litatakata.....so unfair and expensive kwa wapaka Mkorogo khaa!

Kwa baadhi yetu hata tukipaka "Sun cream" ili "kinga" "isiOve weki" bado Kwapa linabaki jeusi kuliko sehemu nyingine ya Mwili....so annoying!


Sasa ukitaka kuikomesha "kinga" inakupasa uiachie Kwapa yako nje ili ipate mwanga wa jua wa mara kwa mara ili "kinga" isi-react kwa hasira dhidi ya Mionzi ya jua mahali hapo!


Wengine Kwapa lawa juesi kwasababu ya kutokumalizika kwa Nywele baada ya kunyoa, Maambukizi ya ngozi na wengine ni kuinyoa sehemu hiyo kwa hasira....ni kwapa tu jamani, kwanini utumie nguvu na hasira kulisugua au kulinyoa?


Nguvu zako ndio zinasababisha "majeraha" usiyoyaona na hivyo kushambuliwa na Bacteria na kuweka "rangi" tofauti hapo kwapani.

Stori time: Jana Usiku nimeamua kunyoa Kwapa (you are welcome hihihihihi I mean sorry for TMI)....bila kutumia Cream....yaani nimeenda "chukuchuku" na Wembe baada ya Miaka zaidi ya 15.

Heee!Mwanamke najiangalia kwapa jeupee na laini halina hata baki la nywele.....Hair removal cream day time bai bai....umeni-cheat for nearly 15yrs....bai bai sikutaki tena!

Sasa ni hivi! Ngozi ni Mkao makuu ya Bacteria (Wanasayansi hawajui kwanini)....sasa unaponyoa Asubuhi ni wazi kuwa umewapa Bacteria Makao masafi ya kushambulia....ndio maana unapata mapele kwapani sometimes!


Hivyo ni vema kufanya "tretment" yeyote ya ngozi kama vile scrub, kutumbua/kamua chunusi, nini na nini...(kunyoa nayo ni treatment na Kwapa ni Ngozi bana wacha ubishi eeh)...mida ya Usiku ili kuipa ngozi nafasi ya kujijenga upya bila muingiliano wa wadudu wa huko Nje.

Kidokezo: Usichukue maelezo haya ukayatumia ukijifanya Mtaalam au umefanya Utafiti, maana Wambongo nanyie nao mmeendelea kweli.....mnaweka na Picha kabisa ili ionekane kuwa wewe ndio Umeandika wakati maelezo ni yangu kwa Uzoefu wangu Binafsi, Ulaaniwe wewe na jamii yako....HUH!!...(Calm down Dinah...Calm down).

Hii imefidia siku 2 ambazo siku-Blog! Ile "kupenda kukaa chini" haina ukweli ndio maana nimeweka *.

Babai.
Mapendo tele kwako...

Comments

Christian Bwaya said…
Dada unaandika. Ah! Hongera sana. Unajua nasoma najikuta kicheko hiko!! Hongera sana. Unajua namna ya kuwasilisha ujumbe wako kwa lugha rafiki, hadi raha. Aisee, lugha tamu asikwambie mtu. Najisikitikia tu sijui lugha uzuri kama wewe.
KKMie said…
Si eti! Kaka Bwaya, nashukuru sana na nafurahi kuwa nakufanya ucheke. Uwepo wako ni muhimu kwenye Blog hii. Ahsante.
Unknown said…
Asante mmno,ur so charming like
Ariano said…
Mtiririko wako umenikumbusha enzi za Dinahicious, nyakati zimeenda sana.
Charismatra said…
Nimekupata snaaa...ngoj nianze kuyafanyia kazi uloyasema..nakupenda buree
.. said…
Ndoa yangu ilikuwa karibu kufikia mwisho nilipoona maoni juu ya mtu anayeitwa Dr DAWN ambaye husaidia watu kuwarudisha wenzi wao na niliwasiliana naye kwa bahati nzuri kwangu aliniroga baada ya masaa 24 mpenzi wangu alirudi kwangu tangu wakati huo ndoa yangu imekuwa. amekuwa mtulivu asante kwa yote aliyonifanyia naweza kukuhakikishia kuwasiliana naye,
yeye ni mjuzi wa maneno yafuatayo:
* maneno ya mapenzi
*miujiza ya ndoa
* uchawi wa pesa
* bahati nzuri
* Vivutio vya ngono inaelezea
* UKIMWI Tiba Uchawi
* Pango la Casino
* Mapango Yamelaaniwa Yameondolewa
* Ulinzi Spell
* Uchawi wa bahati nasibu
* Maneno ya Bahati
* Tahajia ya Uzazi
* Pete ya Telekinesis
WhatsApp: +2349046229159

Barua pepe: dawnacuna314@gmail.com

Topic hizi tamba...

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao