Skip to main content

Posts

Showing posts from March 29, 2015

Kumfulia nguo sio wajibu ni msaada.

Heri ya Ijumaa! Najua umewahi kukutana au kusikia watu wakisema wanataka kufunga ndoa ili wapate watu wa kuwafulia nguo na kuwapikia er futari? Pia umewahi kuona wanaume wakimsifia mwanamke kwasababu akienda kwake lazima atamfulia nguo na hivyo mwanamke huyo anafaa kuwa mke au bado? Unakuta mtu anakasirika kabisa kwasababu nguo zake hazijafuliwa na kunyooshwa tayari kwa ajili yake akidhani kuwa hiyo shughuli ni wajibu au kazi ya Mpenzi wake(wanasahau kuwa kuna Dobi kila Mtaa). Kwa wale wanaofanya kazi nyumbani(mama wa nyumbani) kazi zao ni nyingi kuliko kazi yako nje ya nyumbani hivyo anapokufulia nguo ni msaada.....kwamba anakusaidia so usizoee ukadhani kuwa ni wajibu wake kukufuli. Kunyoosha Nguo aka kupiga Pasi huku Ughaibuni inachukuliwa kama kazi ngumu kwamba inaweka presha kwenye Miguu na uti wa Mgogo sasa imagine mkimama anaefua(kwa kuinamisha mgogo pia).....! Nina sifa nyingi kama mwanamke kwenye "shughuli" za nyumbani lakini sifa kuu ni kunyoosha Mashati na Sur

Jikubali, Jipende Jiamini so they say....

Habariiii! Baadhi huitaji support ili waweze kujikubali kujipenda na kujiamini halafu wengine tumezaliwa hivyo.....si vema kukurupuka na kumwambia mtu lazima ujiamini bwana blablabla.....sio chee kama udhaniavyo. Ni rahisi kujipenda, kujikubali na kujiamini angalau ukiwa umefikisha miaka 25(in my head umri huo ndio unaanza kujitambua na kujijua....unakuwa umekua). Mara zote Binti unapenda kuchukia baadhi ya vitu kwenye mwili wako hasa kipindi cha Kubalehe(tunabadilika). Huwa ni ngumu sana kukabiliana na mabadiliko ya ndani na nje ya mwili.....kiakili na kihisia. Kipindi hiki unaanza kujiona MZURI leo basi linapokuja suala la kuagizwa Dukani wewe ni wa kwanza kutaka kwenda ili "wakuone" si wajua kale ka atensheni ka wavulana kanakokusaidia kujua ujinsia wako? Kanakuwaga enjoyable sana......halafu kesho unakuwa MBAYA unagoma hata kwenda Shule unasingizia unaumwa er Macho (that was me). Ukifikia miaka 25 mabadiliko yanakuwa yameseto na kilichobaki ni kunenepa au kukonda. Un

Wanaume wanaopenda Natural Beauty....

Lakini bado wanavaa Nguo.....waogope sana! Kwanza ni kwanini hasa wanaume wanapenda kufuatilia masuala ya Urembo wa Wanawake au Mavazi ambayo hayawahusu? Jibu: Wanaogopa gharama au roho mbaya bin Mfumo Dume. Mwanamke anakuwa judged muda wote kwa maisha yake yote.....hata mimi nahukumu wanawake wenzangu na mimi mwenyewe lakini hapo hapo huwa najaribu kuelewa kwanini wapo hivyo walivyo(ukiachilia mbali Uwezo wa kifedha) kwasababu najua UANAMKE una issues zake ambazo mwanaume hawezi kuzielewa. Kutokana na kuwa judged muonekano wa Uso/Sura ni muhimu kuliko sehemu nyingine za mwili ambazo anaweza kuziziba kwa kuvaa nguo. Mwanamke anapendezeshwa kwa Vipodozi, Mavazi, Vito vya Thamani na Manukato. Ili mwanamke apendeze inabidi awe msafi na ili awe msafi ni lazima aitunze Ngozi yake, Kucha na Nywele......hivi vyote ni gharama. Unawajua wale wakibaba wanaopenda independent women with natural beauty?So that they can spend their money on others while you (independent woman)pay Bills na