Skip to main content

Jikubali, Jipende Jiamini so they say....

Habariiii!

Baadhi huitaji support ili waweze kujikubali kujipenda na kujiamini halafu wengine tumezaliwa hivyo.....si vema kukurupuka na kumwambia mtu lazima ujiamini bwana blablabla.....sio chee kama udhaniavyo.

Ni rahisi kujipenda, kujikubali na kujiamini angalau ukiwa umefikisha miaka 25(in my head umri huo ndio unaanza kujitambua na kujijua....unakuwa umekua).

Mara zote Binti unapenda kuchukia baadhi ya vitu kwenye mwili wako hasa kipindi cha Kubalehe(tunabadilika). Huwa ni ngumu sana kukabiliana na mabadiliko ya ndani na nje ya mwili.....kiakili na kihisia.

Kipindi hiki unaanza kujiona MZURI leo basi linapokuja suala la kuagizwa Dukani wewe ni wa kwanza kutaka kwenda ili "wakuone" si wajua kale ka atensheni ka wavulana kanakokusaidia kujua ujinsia wako? Kanakuwaga enjoyable sana......halafu kesho unakuwa MBAYA unagoma hata kwenda Shule unasingizia unaumwa er Macho (that was me).

Ukifikia miaka 25 mabadiliko yanakuwa yameseto na kilichobaki ni kunenepa au kukonda. Unaanza kugundua your best bits mwilini mwako na kuzipenda zaidi ili kuficha zile usizozipenda.

Ukifika miaka 30 na upo tayari kuwa Mama na ukashika Mimba na ukafanikiwa kuzaa aiiiiii unaanza upya au unarudia ile miaka ileeee ulipobalehe......wakati huu ni mgumu sababu mwili umekomaa hivyo hata mazoezi huchukua Muda kutoa matokeo mazuri na ya haraka.

My best bits ni Mwili wangu wote na Macho.....sipendi Kucha zangu za Miguuni pia Mikono kwa nyuma(ya kukamatia sio arms) inaniudhiiiii lakini ndio yangu sina budi kuitunza japo imejikunja oh my Meno too hihihihihi.

Sasa nimegundua kuwa watu wanatumia Vipodozi ili kufungua Macho na pengine kuyafanya yawe makubwa.....kwa kifupi hawapendi macho yao yalivyo bila make up.


Mie ninamajicho makubwa (in my head) na ninayapenda sana tu ila tatizo ni kuwa kila mtu anajaribu kuwa na macho kama yangu(natania) ili niwe tofauti na mimi natumia vipodozi kuyapunguza.

Babai.

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao