Skip to main content

Posts

Showing posts from May 25, 2014

Dave na Jamaly

Hawa walikuwa "my best friends" wangu yaani walifanya lolote kwa ajili yangu....baadhi ya watu walidhani jamaa walikuwa wapenzi wangu. Naelewana vema na Wanaume kuliko Wanawake, naturally, wanawake hawanipendi (I think like man most of the time) hihihihihi natania, I just don't click kirahisi na watu wa jinsia yangu. Jamaly nilisoma nae Msingi na wote tukafaulu yeye akaenda Tambaza na mie nikaenda shule moja hivi pale Mjini kati.....Bado urafiki wetu uliendelea Mpaka Chuo. Tulikuwa tunakaa Dawati Moja (yeah nilikuwa nakaa na Wavulana), tulikuwa tunapishana nafasi ya kuongoza darasa. Tulikuwa tukisoma pamoja lakini hatukuwa tukikaa pamoja kwenye Mitihani sio wajua ile kupangwa kwa herufi.....still tulikuwa tukibishana ni maswali gani yatatoka kwenye Mtihani usika. Urafiki na Dave ulianza Kidato cha Pili, na ukaendelea Mpaka naondoka Tanzania karibu miaka 17 iliyopita. Tulikuwa tukisoma pamoja kila tunapotarajia Mitihani japoku

Addicted to Dini....

Jiadhari, inaua! Wataalamu wanaamini kuwa kila Mwanadamu anaumwa Akili(anaugonjwa fulani wa Akili) na huwa triggered na aina ya Maisha anayoishi mhusika. Sasa kuna wale watu wako so dedicated na Imani zao mpaka unahisi akili zao hazipo sawa....hizo mtu zipo Addicted (Dini imetriga Gonjwa la Akili). Kama zilivyo addictions nyingine Imani ya Dini inaharibu Mahusiano, Inasababisha Mfarakano kati ya familia na familia na hatimae kupoteza Maisha au kumfanya Muathirika kuishi Maisha yale yale wakati Mkuu wa Dini (Zungu) anafurahia the High life + attention ya Jamii. Nakumbuka enzi, Mtu (kwenye familia yangu) alikuwa yupo radhi kupeleke "fungu la Kumi" kanisani kila Mwezi kuliko kuwanunua watoto wake mahitaji muhimu. Ilifikia mahali anasomesha watoto wa Waumini wengine wakati Elimu ya watoto wake haieleweki. Addiction ilinoga akaamua kuacha kazi ili "afanye kazi ya Bwana"....akawa anaamka asubuhi kwenda Kanisani na kurud

Nafurahia kuwa Mama...

Lazima umeisikia hii kwa Wanawake wengi wa kileo....Mimi sifurahii kuwa Mama (way too hard) ila najivunia kuwa Mama kwa wanangu. Kuna wale wanawake ambao wakikua tu wanatamani kuwa Mama (kuzaa) yaani kuwa mama ni muhimu kwenye "list" ya mambo wayatakayo Maishani. Mimi sikuwa hivyo, yaani kuzaa haikuwemo kabisa akilini mwangu....nilijua siku moja nitazaa, lakini sikuwa na haraka au niseme urge/desire ya kuwa na Mtoto. Hata nilipojifungua Wanangu sikupata ile hisia wanazopata wanawake wote(wengi waongo hehehehe) "falling in love like never before" au "falling in love all over again"....nilijipa "hi5" in my head nikafurahi na kuwa-proud huku nikujiuliza "kapitapitaje pale"? Haina maana siwapendi Wanangu la hasha! Nawapenda sana na siwezi kuishi bila uwepo wao....hata kwa masaa machache yaani SIWEZI. Ila Mapenzi kwa wanangu hayakuhitaji mimi ku-fall in love na Mapenzi kwa Mtu baki ndio huita

Nafurahia kuwa Mama...

Lazima umeisikia hii kwa Wanawake wengi wa kileo....Mimi sifurahii kuwa Mama (way too hard) ila najivunia kuwa Mama kwa wanangu. Kuna wale wanawake ambao wakikua tu wanatamani kuwa Mama (kuzaa) yaani kuwa mama ni muhimu kwenye "list" ya mambo wayatakayo Maishani. Mimi sikuwa hivyo, yaani kuzaa haikuwemo kabisa akilini mwangu....nilijua siku moja nitazaa, lakini sikuwa na haraka au niseme urge/desire ya kuwa na Mtoto. Hata nilipojifungua Wanagu sikupata ile hisia wanazopata wanawake wote(wengi waogo hehehehe) "falling in love like never before" au "falling in love all over again"....nilijipa "hi5" in my head nikafurahi na kuwa-proud huku nikujiuliza "kapitapitaje pale"? Haina maana siwapendi Wanangu la hasha! Nawapenda sana na siwezi kuishi bila uwepo wao....hata kwa masaa machache yaani SIWEZI. Ila Mapenzi kwa wanangu hayakuhitaji mimi ku-fall in love na Mapenzi kwa Mtu baki ndio huitaji

Rafiki wa kweli...

Haitaji kuku-support kwenye kila jambo hata kama ni baya! Kama ukikosea atakuambia ukweli hata kama unauma....akiku-support kwenye kila kitu ujue ni MNAFIKI. Ndio maana Mimi sina Rafiki bali nafahamiana na watu....oh wait! Actually ninarafiki Mfamasia nilikuwa nae Chuo in olden days....labda kwavile ni Mghana so tofauti ya Kacha imefanya Urafiki Udumu. Sijui wenzangu mlilelewa vipi lakini kukosolewa ni muhimu kama kusifiwa. Ilikuwa unakosolewa kwa kinachokosoleka (ujinga/upuuzi ulioufanya) mbele ya wenzio so that usirudie tena upuuzi wako. Usiogope kuitwa "double standard" akienda ovyo mpe cheupe ajirekebishe. Babai... Mapendo tele kwako...