Skip to main content

Posts

Showing posts from March 8, 2015

MakeUps zinaharibu Ngozi ili uzitegemee?

Biashara ya Vipodozi inapamba faya mwaka hadi mwaka asante Beauty Gurus wa Youtube.....hata mie mpaka Mascara na lipgloss nimeanza kujipaka Foundation siku hizi(well nimeanza kupaka tangu 2004). Enzi hizo mie napaka ilikuwa haiitwi Faundation bana, ilikuwa inaitwa cream to powder au mimi ndio nilikuwa sijui?hihihihihi. The thing ni kwamba most Gurus (nakojifumzia kupaka make up) ngozi zao kama vile haziko sawa. Yaani kuna mmoja siku nilivyomuona bila make up (mambo ya GRWM as in get ready with me) nilaogopa kuendelea kuangalia.....sio kwamba anatisha la hasha! Niliogopa kusikitika na kulia (tangu mekuwa mama nimekuwa way too emotional). Sasa ni mpango wa make up companies kuweka Viasili vya kuharibu Ngozi asilia ili uendelee kununua bidhaa zao na kuficha uharibifu uliopo Ngozini? Najiuliza. Au ni kutokujua kwa baadhi ya watu na hivyo walikuwa hawasafishi Ngozi na kulala na makeups? Pengine ni matumizi ya Vipodozi aka Makeup wakatu ngozi bado haijakomaa? Unajua kuwa Ngozi ni

Kupenda watoto wa watu.

Mawifi na marafiki wa Kike wa mumeo ndio viongozi wa kujifanya wanapenda watoto wa watu. Utasikia "aah jamani waambie nawapenda sana"......mie najibu kimoyo-moyo, unauhakika unawapenda wanangu? Ukikaa nao wiki tu utabadilisha mawazo.....they are hard work! Mimi ni Wifi na Shemeji pia lakini sijawahi kusema nawapenda Wapwa zangu.....ninahisia nao nafurahi kuwaona na kuongea nao lakini siwezi kusema nawapenda wakati sijawahi kuishi nao. Uwazi wangu kuhusu hisia za kupenda watoto wa watu hufanya baadhi ya watu kusema kuwa nina roho mbaya kwamba nachukia watoto. Mie sijui kudanganya kuwa nawapenda wanao wakati najua wazi moyoni hawapo. Nachukulia watoto wote kama watoto na sipendi waonewe au wateseke na hilo ni muhimu zaidi kwangu kuliko kukudanganya kuwa nawapenda. Kwasababu tu ni mtoto haikufanyi automatically umpende.....nilikuambia kwenye moja yabpost zangu, baada ya kuzaa wanangu sikupata ile hisia ya kuanguka kimapenzi kwa mara ya pili na ya tatu baada ya Baba y

Malezi kwa Culture ya Ughaibuni....

Ni kawaida kwa baadhi ya watu(nilikuwa mmoja wao) kushangaa na kuwashutumu Wazazi wa kitanzania waishio Ughaibuni kuwa "wanaiga" na wanalea watoto wao "kizungu" na kusahau au kutojali Kacha yao. Unapomzaa mtoto London kwa mfano na mtoto huyo kuendelea kuishi huko maisha yake yote unategemea mtoto huyo atakuwa na Kacha ya kwenu? Mazingira, Vyakula na Mtindo wa maisha ya wanajamii yanauo mzunguuka ni ya Kacha  ya Nchi husika alikozaliwa na anakulia hivyo sio sahihi "kumpinda" afuate Kacha yako wakati yupo kwenye mazingira tofauti na yale uliyokulia wewe huko kwenu ulikotoka. Mtoto husika anakuja Tanzania mara moja kwa Mwaka na kukaa huko kwa wiki 2-3 na unategemea akue kama wewe na kufuata kacha yako? Ni vema na muhimu kuendeleza values zako na kuwaeleza watoto tofauti ya Kacha yako na Kacha yao lakiji sio kuwalea Kisarawe wakati wanaishi Kent. Just because wamezaliwa na Mtanzania na wao wanautanzania sio lazima wafuate Kacha ya Kitanzania. Jin