Ni kawaida kwa baadhi ya watu(nilikuwa mmoja wao) kushangaa na kuwashutumu Wazazi wa kitanzania waishio Ughaibuni kuwa "wanaiga" na wanalea watoto wao "kizungu" na kusahau au kutojali Kacha yao.
Unapomzaa mtoto London kwa mfano na mtoto huyo kuendelea kuishi huko maisha yake yote unategemea mtoto huyo atakuwa na Kacha ya kwenu?
Mazingira, Vyakula na Mtindo wa maisha ya wanajamii yanauo mzunguuka ni ya Kacha ya Nchi husika alikozaliwa na anakulia hivyo sio sahihi "kumpinda" afuate Kacha yako wakati yupo kwenye mazingira tofauti na yale uliyokulia wewe huko kwenu ulikotoka.
Mtoto husika anakuja Tanzania mara moja kwa Mwaka na kukaa huko kwa wiki 2-3 na unategemea akue kama wewe na kufuata kacha yako?
Ni vema na muhimu kuendeleza values zako na kuwaeleza watoto tofauti ya Kacha yako na Kacha yao lakiji sio kuwalea Kisarawe wakati wanaishi Kent.
Just because wamezaliwa na Mtanzania na wao wanautanzania sio lazima wafuate Kacha ya Kitanzania.
Jinsi wanavyokuwa na bidii yako ya kuwaelisha kuhusu asili yao, Historia ya Nchi yako TANZANIA na Utamaduni wenu ndivyo itakavyowasaidia na pengine kuamua kuishi KisaraweAN au Kibritain.
Mbona nyie hamuishi Ughaibuni na baadhi hamjawahi kufika lakini mnalea wanawenu kiughaihuni bila hata kuwa na Mazingira ya Kiughaibuni?
Mtuache.
Babai.
Comments