Mawifi na marafiki wa Kike wa mumeo ndio viongozi wa kujifanya wanapenda watoto wa watu.
Utasikia "aah jamani waambie nawapenda sana"......mie najibu kimoyo-moyo, unauhakika unawapenda wanangu? Ukikaa nao wiki tu utabadilisha mawazo.....they are hard work!
Mimi ni Wifi na Shemeji pia lakini sijawahi kusema nawapenda Wapwa zangu.....ninahisia nao nafurahi kuwaona na kuongea nao lakini siwezi kusema nawapenda wakati sijawahi kuishi nao.
Uwazi wangu kuhusu hisia za kupenda watoto wa watu hufanya baadhi ya watu kusema kuwa nina roho mbaya kwamba nachukia watoto.
Mie sijui kudanganya kuwa nawapenda wanao wakati najua wazi moyoni hawapo. Nachukulia watoto wote kama watoto na sipendi waonewe au wateseke na hilo ni muhimu zaidi kwangu kuliko kukudanganya kuwa nawapenda.
Kwasababu tu ni mtoto haikufanyi automatically umpende.....nilikuambia kwenye moja yabpost zangu, baada ya kuzaa wanangu sikupata ile hisia ya kuanguka kimapenzi kwa mara ya pili na ya tatu baada ya Baba yao kama wengi wanavyodai.
Kuna possibly hakuna hisia kama hiyo ila ni mchanganyiko wa furaha ya kumuona mwanao baada ya maumivu ya Uchungu na ile hali ya wuhuuu it is over!!
Kingine ni guilt (mawifi wanqkughukia ili kuficha hilo kwa kaka yao wanakimbilia nawapenda sana wapwa zangu) au kutaka kuwa karibu na Baba yao.
....hihihihihi unawajua wale wa "jamani watoto wazuri, nawapenda natamani wangekuwa wangu".....hawa husema hivyo kwenye profile ya mumeo tu sio yako.
Eeh Babuu si katimiza miaka 4.....asubuhi yake sasa kaanza "mum is today my birthday".....nikasema ndio....babuu:yay...mum you forgot to say something.....nikasema nini? Babuu: sing happy birthday song.
Umegundua nini?
Kaniita mum na sio mummy kama kawaida ya watoto chini ya miaka 6. Aah my boy is a grown man.....sort of.
Babai.
Comments