Skip to main content

Kupenda watoto wa watu.


Mawifi na marafiki wa Kike wa mumeo ndio viongozi wa kujifanya wanapenda watoto wa watu.


Utasikia "aah jamani waambie nawapenda sana"......mie najibu kimoyo-moyo, unauhakika unawapenda wanangu? Ukikaa nao wiki tu utabadilisha mawazo.....they are hard work!



Mimi ni Wifi na Shemeji pia lakini sijawahi kusema nawapenda Wapwa zangu.....ninahisia nao nafurahi kuwaona na kuongea nao lakini siwezi kusema nawapenda wakati sijawahi kuishi nao.


Uwazi wangu kuhusu hisia za kupenda watoto wa watu hufanya baadhi ya watu kusema kuwa nina roho mbaya kwamba nachukia watoto.


Mie sijui kudanganya kuwa nawapenda wanao wakati najua wazi moyoni hawapo. Nachukulia watoto wote kama watoto na sipendi waonewe au wateseke na hilo ni muhimu zaidi kwangu kuliko kukudanganya kuwa nawapenda.


Kwasababu tu ni mtoto haikufanyi automatically umpende.....nilikuambia kwenye moja yabpost zangu, baada ya kuzaa wanangu sikupata ile hisia ya kuanguka kimapenzi kwa mara ya pili na ya tatu baada ya Baba yao kama wengi wanavyodai.


Kuna possibly hakuna hisia kama hiyo ila ni mchanganyiko wa furaha ya kumuona mwanao baada ya maumivu ya Uchungu na  ile hali ya wuhuuu it is over!!

Kingine ni guilt (mawifi wanqkughukia ili kuficha hilo kwa kaka yao wanakimbilia nawapenda sana wapwa zangu) au kutaka kuwa karibu na Baba yao.


....hihihihihi unawajua wale wa "jamani watoto wazuri, nawapenda natamani wangekuwa wangu".....hawa husema hivyo kwenye profile ya mumeo tu sio yako.

Eeh Babuu si katimiza miaka 4.....asubuhi yake sasa kaanza "mum is today my birthday".....nikasema ndio....babuu:yay...mum you forgot to say something.....nikasema nini? Babuu: sing happy birthday song.

Umegundua nini?

Kaniita mum na sio mummy kama kawaida ya watoto chini ya miaka 6. Aah my boy is a grown man.....sort of.

Babai.

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao