Biashara ya Vipodozi inapamba faya mwaka hadi mwaka asante Beauty Gurus wa Youtube.....hata mie mpaka Mascara na lipgloss nimeanza kujipaka Foundation siku hizi(well nimeanza kupaka tangu 2004).
Enzi hizo mie napaka ilikuwa haiitwi Faundation bana, ilikuwa inaitwa cream to powder au mimi ndio nilikuwa sijui?hihihihihi.
The thing ni kwamba most Gurus (nakojifumzia kupaka make up) ngozi zao kama vile haziko sawa. Yaani kuna mmoja siku nilivyomuona bila make up (mambo ya GRWM as in get ready with me) nilaogopa kuendelea kuangalia.....sio kwamba anatisha la hasha! Niliogopa kusikitika na kulia (tangu mekuwa mama nimekuwa way too emotional).
Sasa ni mpango wa make up companies kuweka Viasili vya kuharibu Ngozi asilia ili uendelee kununua bidhaa zao na kuficha uharibifu uliopo Ngozini? Najiuliza.
Au ni kutokujua kwa baadhi ya watu na hivyo walikuwa hawasafishi Ngozi na kulala na makeups?
Pengine ni matumizi ya Vipodozi aka Makeup wakatu ngozi bado haijakomaa? Unajua kuwa Ngozi ni moja ya Ogani kama ilivyo Moyo na inakua kulingana na ukuaji wako...sidhani hii ilikuwepo kwenye Biology niliyosoma au kwa vile nilikuwa nasinzia(Mwalimu alikuwa so boring....akianza tu mie yuleee Kisarawe).
Au hali ya hewabya Baridi haipendi Ngozi nyeusi.....kwamba naturally inakinga ya kutosha kupigana na Jua sasa kama Jua halitoshi ngozi inasahau sijui masikini matokeo yake inapigana na Vipodozi(Doesnt even make sense I know).
Anyway.....kila biashara ina namna yake ya kuendelea....mf biashara ya software na Virus.....wanaotengeneza softwares ndio wanaotengeneza Virus ili biashara ya software iendelee kuwepo na wewe mtumiaji kuwa tegemezi.
Ngozi yangu inabadilika kulingana na hali ya hewa. Baridi napauka(a bit lighter)na wakati wa joto naiva(a bit darker).....lakini ile cream to powder haikunibadilisha....kwanza hata nilipaka Foundation hujui.
Ama sijui kujipaka au kwa ujumla sirembeki hihihihi sura gumu mpaka Make ups zinadunda.
Napenda makeup sababu inanipa kale ka muda ka mimi kuwa peke yangu bila adha ya watoto na baba yao. Ila hiyo issue ya Ngozi kuwa mbaya ndio inanikatisha tamaa.
Leo ni siku ya Mikosi UK.....kila Ijumaa 13. Happy 1st Mikosi day of 2015.
Babai.
Comments