Skip to main content

Posts

Showing posts from May 11, 2014

1st time Mothers....

Za mida hii....? Enzi zile za Usichana(shuleni) kulikuwa na kipindi cha watoto "chuchuchu" kilikuwa kikiendeshwa na Marehemu Amina Chifupa(Pumzika kwa Amani). Alipojifungua basi kila wakati ilikuwa "nani huu hivi, nanihu vile" yaani ali-share excitement ya kuwa mama kwa mara ya kwanza. Mimi na wanafunzi wengine, tulikuwa tunakereka kweli na hiyo "mwanangu hivi, vile".....tukawa tunasema "Amina nae ka' yeye ndio wa kwanza kujifungua, Ulimbukeni tu!! Kumbe bana tulikuwa wadogo, hatukujua hisia anazozipata mwanamke baada ya kujifungua kwa mara ya kwanza. Niulize mimi nilipojifungua mara ya kwanza hehehehehe nilikera watu kwa picha na vijimaandishi vya kuwakilisha vitendo au pose yake kwenye Picha. Hakika niliwakera watu sana tu. Namkumbuka Marco Mwenda (nae ni marehemu alifariki kwa ajari ya Gari mwaka Jana, apumzike kwa Amani)....aliwahi kuniambia " Da' Dinah nawe unachosha, utadhani wewe ndio mama wa kwanza hapa Duniani"...

Kesi za Kubaka za Miaka ya 70s-80s....

Bari gani? Hizi Kesi na Hukumu zinazotolewa huku dhidi ya "vibabu" waliobaka au ku-abuse wasichana wadogo miaka 40 iliyopita zinaudhi eti! Unaeza sema "masikini vibabu vya watu vinafungwa bure kwa makosa ya miaka ile".....au ukajiuliza "hao wanawake walikuwa wapi tangu enzi zile kupeleka Mashtaka yao". Well! Huwezi kuelewa mpaka uwe umepitia huko au wewe ni mwanamke na unakuwa targeted kwasababu tu una Matiti na Uke. Sipendi kulinganisha lakini linapokuja suala la ku-abuse wanawake kingono hasa sehemu za kazi Tz, mimi ni mmoja kati ya wengi ambao tulitishiwa kufukuzwa (kunyimwa ajira ya Kudumu) kama tutakataa kujitoa kimwili. Wenzangu sijui, lakini mie na misimamo yangu nikamwambia "unikome ka' ziwa la mama yako na sina shida na Kazi yako".....nikatoka, mefika nyumbani nikaenda kumshitaki kwa Mama na Baba (hihihihi hapo nilikuwa Binti wa miaka 25). Sijui sheria ya Unyanyaswaji wa Kijinsia na Ubaka

Comments kwenye Gazeti la "kushika"

Jambo jambo? Sijasoma Gazeti la kushika kitambo kweli, asa nipo Trenini nasoma Gazeti la asubuhi, baada ya kusoma sinkawa natafuta "comments" ili nisome maoni ya watu....ikabidi nijicheke! Wiki ijayo kuna Uchaguzi wa Wawakilishi wa Ulaya, Hakuna chama kinachonifurahisha mpaka sasa. Nikieka majina ya Vyama hapa nitaanza kufuatiliwa kwa karibu na siku nikitereza tu narudishwa Kisarawe, so wacha wabaki "kapuni". Sijui umuhimu wa Umoja wa Ulaya kwangu binafsi zaidi ya kushikilia Bango Haki za Binadamu, hivyo nitapiga kura ili tubaki kwenye umoja huo kwa maana hiyo sitochagua yeyote anaetaka tutoke kwenye Umoja wa Ulaya. Siasa inagusa Maisha yangu, napenda Siasa ila nimeacha kufuatilia zile za Nyumbani kwani hunipa hasira alafu hazinifaidishi. Za huku zinaeza kukupa hasira (kama umekatiwa msaada wa senti hihihihi) lakini angalau unapewa nafasi ya kumtumia Mbunge wako kwa issues ambazo labda hazikutiliwa maanani na wajinga

Kila Kidume(secretly) hupenda kidume Maishani....

Hapana sio "Mikorosho" bali kupata/zalishiwa mtoto wa Kiume......Heri ya Wiki Mpya kwako! Umewahi kutana na wanaume ambao watoto wao wa kwanza ni wa Kike, na ukasikia wanavyotetea Binti zao na kuponda watoto wa kiume au hata kujifanya "hawajali" mtoto gani anazaliwa. Wengi hudai "Bora Binti Malaya kuliko Kidume Shoga"....ukielewa Sentesi hiyo kwa undani utagundua kuwa Msemaji hapendi watoto wa kike na kesha Muita Malaya kabla hata hajakua masikini. Hawana mtoto wa Kiume hivyo "ushoga" hausiki (hauna nguvu) hapo lakini tayari wamuita Binti Malaya....haa! Kisiri-siri wanatamani sana na pengine waliombea kupata mtoto wa kiume lakini haikuwa hivyo..... Wengine husema "Mheshimu Mkeo kwani kakuzalia kidume muendeleza jina la Ukoo" Mimi binafsi SIKUTAKA kabisa kuzaa mtoto wa Kike kama 1st born kitambo kabla hata sijajua kama ipo siku nitazaa. Nadhali ilitokana na hali ya kujisikia "safe" na kuheshimiwa (ogopwa) kwa vile nilikuwa na m