Jambo jambo?
Sijasoma Gazeti la kushika kitambo kweli, asa nipo Trenini nasoma Gazeti la asubuhi, baada ya kusoma sinkawa natafuta "comments" ili nisome maoni ya watu....ikabidi nijicheke!
Wiki ijayo kuna Uchaguzi wa Wawakilishi wa Ulaya, Hakuna chama kinachonifurahisha mpaka sasa.
Nikieka majina ya Vyama hapa nitaanza kufuatiliwa kwa karibu na siku nikitereza tu narudishwa Kisarawe, so wacha wabaki "kapuni".
Sijui umuhimu wa Umoja wa Ulaya kwangu binafsi zaidi ya kushikilia Bango Haki za Binadamu, hivyo nitapiga kura ili tubaki kwenye umoja huo kwa maana hiyo sitochagua yeyote anaetaka tutoke kwenye Umoja wa Ulaya.
Siasa inagusa Maisha yangu, napenda Siasa ila nimeacha kufuatilia zile za Nyumbani kwani hunipa hasira alafu hazinifaidishi.
Za huku zinaeza kukupa hasira (kama umekatiwa msaada wa senti hihihihi) lakini angalau unapewa nafasi ya kumtumia Mbunge wako kwa issues ambazo labda hazikutiliwa maanani na wajinga-wajinga na yeye kufuatilia kwa karibu.
Kila sehemu ya Kazi (hasa za Serikali) kuna wajinga wajinga ambao hawataki kufanya kazi zao au wanakuwa wazembe, hapo ndio Mbunge huingilia kati.
Nikutakie siku njema.
Mapendo tele kwako...
Sijasoma Gazeti la kushika kitambo kweli, asa nipo Trenini nasoma Gazeti la asubuhi, baada ya kusoma sinkawa natafuta "comments" ili nisome maoni ya watu....ikabidi nijicheke!
Wiki ijayo kuna Uchaguzi wa Wawakilishi wa Ulaya, Hakuna chama kinachonifurahisha mpaka sasa.
Nikieka majina ya Vyama hapa nitaanza kufuatiliwa kwa karibu na siku nikitereza tu narudishwa Kisarawe, so wacha wabaki "kapuni".
Sijui umuhimu wa Umoja wa Ulaya kwangu binafsi zaidi ya kushikilia Bango Haki za Binadamu, hivyo nitapiga kura ili tubaki kwenye umoja huo kwa maana hiyo sitochagua yeyote anaetaka tutoke kwenye Umoja wa Ulaya.
Siasa inagusa Maisha yangu, napenda Siasa ila nimeacha kufuatilia zile za Nyumbani kwani hunipa hasira alafu hazinifaidishi.
Za huku zinaeza kukupa hasira (kama umekatiwa msaada wa senti hihihihi) lakini angalau unapewa nafasi ya kumtumia Mbunge wako kwa issues ambazo labda hazikutiliwa maanani na wajinga-wajinga na yeye kufuatilia kwa karibu.
Kila sehemu ya Kazi (hasa za Serikali) kuna wajinga wajinga ambao hawataki kufanya kazi zao au wanakuwa wazembe, hapo ndio Mbunge huingilia kati.
Nikutakie siku njema.
Mapendo tele kwako...
Comments