Za mida hii....?
Enzi zile za Usichana(shuleni) kulikuwa na kipindi cha watoto "chuchuchu" kilikuwa kikiendeshwa na Marehemu Amina Chifupa(Pumzika kwa Amani).
Alipojifungua basi kila wakati ilikuwa "nani huu hivi, nanihu vile" yaani ali-share excitement ya kuwa mama kwa mara ya kwanza.
Mimi na wanafunzi wengine, tulikuwa tunakereka kweli na hiyo "mwanangu hivi, vile".....tukawa tunasema "Amina nae ka' yeye ndio wa kwanza kujifungua, Ulimbukeni tu!!
Kumbe bana tulikuwa wadogo, hatukujua hisia anazozipata mwanamke baada ya kujifungua kwa mara ya kwanza.
Niulize mimi nilipojifungua mara ya kwanza hehehehehe nilikera watu kwa picha na vijimaandishi vya kuwakilisha vitendo au pose yake kwenye Picha.
Hakika niliwakera watu sana tu. Namkumbuka Marco Mwenda (nae ni marehemu alifariki kwa ajari ya Gari mwaka Jana, apumzike kwa Amani)....aliwahi kuniambia " Da' Dinah nawe unachosha, utadhani wewe ndio mama wa kwanza hapa Duniani"....
.....nikacheka nkamwambia wee ni Mkibaba hujui Mkimama anavyojisikia baada ya kumaliza Miezi Tisa salama na mwishowe kusukuma nje Kilo Tatu za mtu mdogo mwenye afya njema.
Sasa kutokana na Techolojia ilivyokuwa watu wanapitiliza wana-share mpaka Scan ya kwanza(18weeks).....kikwetu hupaswi kusema chochote kuhusu Mimba yako hasa kama haijajitokeza(haionekani) na ukiulizwa unakana...."akuuu sina Mimba mie, Ndoa tu ndio inaninenepeshaa".
Ile hali ya kujifunza na kushuhudia kila hatua ya ukuaji wa mwanao na kuirekodi (asante Teknolojia) ni vere....veri Fascinating.
Kuwa mama sio Kazi rahisi, inachosha inakupa stress na wakati mwingine depression lakini kama una "support system" (ndugu, jamaa na rafiki) nzuri na ya uhakika mambo yanakuwa mazuri sana.
Sasa namuelewa Mama yeyote aliezaa mtoto wake wa kwanza naku-share furaha na yote anayojifunza, shangaa kuhusu mwanae.
Ni hisia maalum ambazo hakuna mwanamke atazielewa mpaka atakapopata uzoefu, na kwa wanaume....well ni wanaume hamtokaa mzijue hisia hizo....hata mkibadilisha Jinsia via Cosmetics Surgery.....hihihihi!
Uanamke ni zaidi ya kupenda mavazi ya Kike, kujiremba, Matiti na Uke....(Nafikiria kwa sauti).
Nikuache kwa sasa eti....babai!
Mapendo tele kwako...
Enzi zile za Usichana(shuleni) kulikuwa na kipindi cha watoto "chuchuchu" kilikuwa kikiendeshwa na Marehemu Amina Chifupa(Pumzika kwa Amani).
Alipojifungua basi kila wakati ilikuwa "nani huu hivi, nanihu vile" yaani ali-share excitement ya kuwa mama kwa mara ya kwanza.
Mimi na wanafunzi wengine, tulikuwa tunakereka kweli na hiyo "mwanangu hivi, vile".....tukawa tunasema "Amina nae ka' yeye ndio wa kwanza kujifungua, Ulimbukeni tu!!
Kumbe bana tulikuwa wadogo, hatukujua hisia anazozipata mwanamke baada ya kujifungua kwa mara ya kwanza.
Niulize mimi nilipojifungua mara ya kwanza hehehehehe nilikera watu kwa picha na vijimaandishi vya kuwakilisha vitendo au pose yake kwenye Picha.
Hakika niliwakera watu sana tu. Namkumbuka Marco Mwenda (nae ni marehemu alifariki kwa ajari ya Gari mwaka Jana, apumzike kwa Amani)....aliwahi kuniambia " Da' Dinah nawe unachosha, utadhani wewe ndio mama wa kwanza hapa Duniani"....
.....nikacheka nkamwambia wee ni Mkibaba hujui Mkimama anavyojisikia baada ya kumaliza Miezi Tisa salama na mwishowe kusukuma nje Kilo Tatu za mtu mdogo mwenye afya njema.
Sasa kutokana na Techolojia ilivyokuwa watu wanapitiliza wana-share mpaka Scan ya kwanza(18weeks).....kikwetu hupaswi kusema chochote kuhusu Mimba yako hasa kama haijajitokeza(haionekani) na ukiulizwa unakana...."akuuu sina Mimba mie, Ndoa tu ndio inaninenepeshaa".
Ile hali ya kujifunza na kushuhudia kila hatua ya ukuaji wa mwanao na kuirekodi (asante Teknolojia) ni vere....veri Fascinating.
Kuwa mama sio Kazi rahisi, inachosha inakupa stress na wakati mwingine depression lakini kama una "support system" (ndugu, jamaa na rafiki) nzuri na ya uhakika mambo yanakuwa mazuri sana.
Sasa namuelewa Mama yeyote aliezaa mtoto wake wa kwanza naku-share furaha na yote anayojifunza, shangaa kuhusu mwanae.
Ni hisia maalum ambazo hakuna mwanamke atazielewa mpaka atakapopata uzoefu, na kwa wanaume....well ni wanaume hamtokaa mzijue hisia hizo....hata mkibadilisha Jinsia via Cosmetics Surgery.....hihihihi!
Uanamke ni zaidi ya kupenda mavazi ya Kike, kujiremba, Matiti na Uke....(Nafikiria kwa sauti).
Nikuache kwa sasa eti....babai!
Mapendo tele kwako...
Comments