Umewahi kutana na wanaume ambao watoto wao wa kwanza ni wa Kike, na ukasikia wanavyotetea Binti zao na kuponda watoto wa kiume au hata kujifanya "hawajali" mtoto gani anazaliwa.
Wengi hudai "Bora Binti Malaya kuliko Kidume Shoga"....ukielewa Sentesi hiyo kwa undani utagundua kuwa Msemaji hapendi watoto wa kike na kesha Muita Malaya kabla hata hajakua masikini.
Hawana mtoto wa Kiume hivyo "ushoga" hausiki (hauna nguvu) hapo lakini tayari wamuita Binti Malaya....haa!
Kisiri-siri wanatamani sana na pengine waliombea kupata mtoto wa kiume lakini haikuwa hivyo.....
Wengine husema "Mheshimu Mkeo kwani kakuzalia kidume muendeleza jina la Ukoo"
Mimi binafsi SIKUTAKA kabisa kuzaa mtoto wa Kike kama 1st born kitambo kabla hata sijajua kama ipo siku nitazaa.
Nadhali ilitokana na hali ya kujisikia "safe" na kuheshimiwa (ogopwa) kwa vile nilikuwa na maKaka.
Nilijiamini kuwa nitatoa Kidume kwasababu kwetu Vidume ni wa kumwaga, pamoja na kujiamini bado haikunipa Guarantee ya mtoto wa kwanza kuwa Kidume.
Hivyo niliomba Mungu kila siku na nilijitahidi kwenye mambo ya "Sayansi ya Viumbe" yaani Tarehe, Mikao na kula aina fulani ya vyakula ili kuongeza "uwezekano" wa kupata Kidume.
Mdogo wangu alipojifungua Mtoto wake wa kwanza wa kiume, nilifurahi huku na natamani/ombea kimoyomoyo ingekuwa mimi.
Zamu yangu ilipofika miaka 2 baadae na Scan ikaonyesha kuwa ni Kidume, nilifurahi hadi nikatoa Sadaka...Team Vidume as 1st Born(doesn't even make sense).
Wa pili sikujali sana (kisiri-siri nilitaka awe mkidada though ili nikamilishe familia).....isingetokea basi ningeasili kabinti mahali.
Siku ya Scan tukaambiwa ni kabinti.....sikufurahi kama ilivyokuwa kwa Kidume lakini nilimwambia baba yake "I told you"(Mimba ilisumbua so nikajua nimebeba mahomono) !!!
Hakika mtoto ni mtoto tu na hatuna budi kushukuru lakini najua sote "kisiri-siri" huwa tuna "prefer" Jinsia fulani, sema guilt, uwoga, au taabu ya kushika mimba/pata mtoto inatufanya tuseme "mie sijali awe wa kike au wa kiume".
Natambua Kiasili na Kisayansi Wanaume wote hupenda kuwa na mtoto wa Kiume. Haina Mfumo Dume na wala sio Chuki ya Gender bali ni hali halisi....ni necha.
Bai kwa sasa...
Mapendo tele kwako...
Comments