Skip to main content

Posts

Showing posts from April 13, 2014

Kazi za watu...

Maoni ya Mhariri...siku hizi sote tunatoa Maoni on particular or similar issues....Teknolojia na Uhuru wa kujieleza/Changia utakacho au ulichokiona/shuhudia unaharibu kazi za watu. Mfano, kazi ya Uandishi wa Habari wa Magazeti na Radio....imeingiliwa na Blogs, Online Radios, Social Media na YouTube(is YouTube sosho Media pia?). Jamaa wanatumia Sosho Midia kama "chanzo cha uhakika" na wale Waandishi wavivu wa kukopi na kupesti ndio wamerahisishiwa kazi. Habari zenye Uzito ni zile za Uchunguzi....labda na mahojiano magumu ya Wanasiasa! Jana nipo YouTube (napenda Fashion Haul na beauty review....how sad!!?) nikakutana na Matangazo kutoka Kampuni moja kubwa ya Urembo....alietumiwa ni Vlogger na sio Model/Celeb kama nilivyozoea. Nkajisemea eeh Teknolojia imeharibu na kazi za Celebs na Model pia.....sio haki kabisa! ....Hebu ngoja kwanza! Hawa Vlogger ni real people wanatumia bidhaa na kuzi-review hivyo wao kutangaza bidhaa husika wana

Diet...

Hiya.... Utaratibu wa kula kwa kila mtu ni Asubuhi, Mchana na Jioni. Baadhi yetu tunaongeza Mlo in between na wengine hatumudu Milo miwili kwa siku. Sijawahi kujinyima ili kupungua au kukonda, nimekuwa chembamba maisha yangu yote ya Usichana mara boom nikafikia size 12(Mimba hizo). Nikajiambia, ah nikijifungua nitakuwa nakwenda Gym ili nirudie kamwili kangu ka enzi....aiii muda si ukagoma kutokea. Nikaamua tu kupiga mazoezi yangu mwenyewe nyumbani. Sikuweza ku-keep up na mazoezi kutokana na Uchovu (mother of two kids under 5 baibeee isn't as easy as Celebs looove to lie on our faces).... Nkapiga mahesabu, mmh am on my 30s nikishangaa hapa nitakuwa na kitambi for life....nifanye nini sasa wajameni? Nikapata jibu...relax Dinah Relax.....wacha Kichanga afikishe miezi 9 (atakuwa anajitegemea...kukaa peke yake na kulala vema usiku) alafu ndio uanze mambo yako. Kusubiri mpaka afikishe miezi 9, mbali alafu sio guarantee atakuwa "a

Nywele zako ni 2a au 4z?

Wenzetu ambao wamezaliwa na Mzazi mmoja Mwenye asili ya "Nywele kunyooka" wanapenda kutupeleka mbio sana sisi wenye kipilipili. Hata kama Bibi yake Bibi wa Baba yake ndio alikuwa "nywele kunyooka" na mweupe bado mtu ana-claim yeye ni asili hiyo which is Okay ila msitupeleke mbio sasa eti! Juzi nimesoma mahali, Binti mmoja anasema anamshukuru Baba yake kwa kutokuoa Mwafrika mwenzie maana angezaliwa mbaya na mwenye nywele mbaya za 4b....anampenda sana mama yake ambae ni Mzungu. Nkakimbilia ku-google ili nijue maana ya hizi namba na herufi "Nyweleni"....well nilitaka kujua namba ya Nywele zangu, aiiii nadhani ni 5z...the higher the number the Mbayest the hair. Tunanyoosha nywele sio kwasababu hatuzipendi tulizozaliwa nazo au tunataka kufanana na nyie bali ni kutaka kuzi-manage kiurahisi... Ni kipilipili cha haja lakini kuna wakati kilikua na kufika katikati ya Mgongo....HAPANA!! am not that short...am 5'4 nadhan