Skip to main content

Diet...

Hiya....

Utaratibu wa kula kwa kila mtu ni Asubuhi, Mchana na Jioni. Baadhi yetu tunaongeza Mlo in between na wengine hatumudu Milo miwili kwa siku.



Sijawahi kujinyima ili kupungua au kukonda, nimekuwa chembamba maisha yangu yote ya Usichana mara boom nikafikia size 12(Mimba hizo).



Nikajiambia, ah nikijifungua nitakuwa nakwenda Gym ili nirudie kamwili kangu ka enzi....aiii muda si ukagoma kutokea. Nikaamua tu kupiga mazoezi yangu mwenyewe nyumbani.



Sikuweza ku-keep up na mazoezi kutokana na Uchovu (mother of two kids under 5 baibeee isn't as easy as Celebs looove to lie on our faces)....




Nkapiga mahesabu, mmh am on my 30s nikishangaa hapa nitakuwa na kitambi for life....nifanye nini sasa wajameni?




Nikapata jibu...relax Dinah Relax.....wacha Kichanga afikishe miezi 9 (atakuwa anajitegemea...kukaa peke yake na kulala vema usiku) alafu ndio uanze mambo yako.




Kusubiri mpaka afikishe miezi 9, mbali alafu sio guarantee atakuwa "anajitegemea" au kulala vizuri. Back to my hesabu!



Anhaaa!! Nitakuwa nakula Dinner (Wali/Viazi/Ndizi/Ugali + Mboga yeyote) asubuhi na Breakfast Jioni (Uji, Ndizi 1 + Chai au Mkate na Yai + Chai).




Well, sina hakika "diet" yangu imesaidia mimi kupungua au ni kunyonyesha + Mazoezi.....lakini najua kuwa imechangia kwa namna moja au nyingine.




Sijawahi kuwa Mnene hivyo kugonga size 12 hakika nilikuwa Kibonge (in my head) na hata wadogo zangu waliokuwa wakiniita "Chikonda" mara wakawa wananiita "Chibonge"....



Mambo ya kufuata Diet za so called wataalam au Watu Mashuhuri/Maarufu zinabadilika ka' software na zinaongeza stress tu....


Kula pale unapohisi njaa na kula kiasi....

Siku njema.
Mapendo tele kwako...

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao