Skip to main content

Posts

Showing posts from November 1, 2015

Bora alama ya Mstari kuliko F.....Miaka 20 Tangu Secondary

Mambo! Ijumaa Mpya(ya Kwanza Mwezi huu) na Maalum kabisa kwani ni Wiki ya Kwanza tangu kuanza kwa Mitihani ya Kumaliza Kidato cha Nne Tanzania, na ndio Mwanzo wa Mwisho wa Series hii(inaonekana kupedwa/somwa zaidi), inapendeza! Utakuwa unajua by now kuwa Mie na Hisabati sio marafiki, Biology niliipenda kwenye kuandika Essay kuhusu Maambukizo au Magonjwa(niliyajua haya kutokana na Somo la Sayansikimu kutoka Msingi), mengineyo nilikuwa sielewi(nilikuwa nasinzia). Mwalimu wetu wa Biology Kidato cha Tatu-Nne alikuwa a bit Boring au alikuwa  na Mapepo(hihihi). Yule mama alipokuwa akiingia na kufungua Mdomo "Good afternoon" mie yuleeeee Uzaramoni.....yaani macho yanakuwa mazito halafu nalala ule usingizi Mzito m paka Udenda! Nikaona aah isiwe shida bana, nikawa siingii kwenye Kipindi chake unless kuna Essay hehehehe. Sikufanya Mitihani Miwili  nayo Hisabati na Biology, kwasababu nilijua wazi sitofanikiwa kufanya vizuri na matokeo yake nikaamua ni Bora nipate alam

Kuzuia Mimba au Kupoteza Hamu?

Habari ya sasa! Utasema hee Dinah mbona umeshupalia Topic hizi? Well....ninachoandika hakitobadilisha Maisha ya watu na kuwa Bora zaidi ya yalivyo sasa, lakini naweza kusaidia mtu mmoja kuelewa kwa kiasi kidogo....yule ambae ame-google "kupoteza hamu" kwa mwanamke si eti! Kuna ulalamishi kuwa Dawa za kuzia Mimba(pamoja na matatizo mengine kwa baadhi) husababisha Mwanamke kupoteza hali ya kutaka/tamani Ngono. Hakuma chunguzi ambayo ina-support hili ila Wanawake wengi hulalamikia kuwa Hamu hupungua au hutoweka kabisa mara tu baada ya kuanza kutumia Njia za kuzuia mimba Zenye Homono(hata zisizo na Homono huingilia "hamu" ya mwanamke"). Do I look like I am busy? Ukweli ni kwamba kama hali ya kutaka  Ngono ilikuwa juu au chini basi haitobadilika......isipokuwa utaratibu wa Mwili wako ndio utabadilika na hivyo wewe Mkimama kulazimika kuanza kujifunza upya(wengi huwa hawalijui hili) namna mwili wako unafanya kazi. Tena sio Dawa za kuzuia m

Umuhimu wa Furaha ya Mke....

....wengi huchukulia suala hili juu juu tu, labda hushindwa kuelewa kwasababu Jamii (ikiongozwa na wanawake wenyewe) huwa  hailizungumzii sana kama wazungumziavyo Furaha ya Mume. Furaha ni hitaji la wote lakini nadhani kwa mwanamke ni muhimu zaidi kwasababu bila furaha kwake ni wazi watoto  na baba mtu hatokuwa na furaha. Pia furaha kwa mwanamke inahusika sana kwenye masuala ya kufanya mapenzi.....kama mwanamke hana furaha ni ama hakutakuwa na Tendo au Tendo halitokuwa la kufurahia na badala yake litakuwa ni la kumaliza haja tu kwa Mwanaume(maliza nilale arrg hihihihi). Wanaume wachache ambao wameshuhudia baba zao wakihakikisha Mama zao wanafuraha mara zote iwezekenavyo, hujitahidi na kuwa hivyo au zaidi kwa wake zao. Hawa hujua namna ya kujali  na kuheshimu hisia za mwanamke. Kwabahati mbaya sehemu kubwa ya Wanaume wamelelewa kwenye Mazingira ya kumuona Mama  ni mtu mmoja mvumilivu, mpole na muelevu.....wakati Baba Mkali na Bingwa wa kudharau. Kwamba Mama anapochoshwa n