Skip to main content

Kuzuia Mimba au Kupoteza Hamu?

Habari ya sasa!

Utasema hee Dinah mbona umeshupalia Topic hizi? Well....ninachoandika hakitobadilisha Maisha ya watu na kuwa Bora zaidi ya yalivyo sasa, lakini naweza kusaidia mtu mmoja kuelewa kwa kiasi kidogo....yule ambae ame-google "kupoteza hamu" kwa mwanamke si eti!




Kuna ulalamishi kuwa Dawa za kuzia Mimba(pamoja na matatizo mengine kwa baadhi) husababisha Mwanamke kupoteza hali ya kutaka/tamani Ngono. Hakuma chunguzi ambayo ina-support hili ila Wanawake wengi hulalamikia kuwa Hamu hupungua au hutoweka kabisa mara tu baada ya kuanza kutumia Njia za kuzuia mimba Zenye Homono(hata zisizo na Homono huingilia "hamu" ya mwanamke").

Do I look like I am busy?



Ukweli ni kwamba kama hali ya kutaka  Ngono ilikuwa juu au chini basi haitobadilika......isipokuwa utaratibu wa Mwili wako ndio utabadilika na hivyo wewe Mkimama kulazimika kuanza kujifunza upya(wengi huwa hawalijui hili) namna mwili wako unafanya kazi. Tena sio Dawa za kuzuia mimba tu ndio zinasababisha hili, bali pia kuwa Mama(Kuzaa kunabadilisha Mwili na Akili).




Unapoongeza Homono ambazo zinaenda kuingilia utaratibu wa Mayai yako ili usishike Mimba ni wazi ile siku ya Kipevuka hutojisikia Nyege sana kama ilivyokuwa awali kabla hujaanza kutumia Dawa za kuzuia Mimba. Nia na madhumuni ya Dawa  hizo ni kuzuia Uwezekano wako wa kushika Mimba.




Hivyo Yai linapokuwa "tayari" Dawa za kuzuia Mimba (aina ya Homono) ndio hufanya kazi ya ziada kuzuia na hivyo kukamata (shika/teketeza) zile "sex homono" ambazo hujitokeza kipindi hiki na hivyo kukufanya utake Ngono na kutoa Ute laini ili Mbegu zisafiri kwa "amani" na hivyo kushika Mimba.(Dhumuni la Ngono ni Mimba/Kuzaliana siunajua?)


Nimekuchanganya? Tuna Homono zaidi ya Moja lakini sasa kwa vile Mie sio Msayansi siwezi kuelezea Kisayansi na hivyo nimejaribu kuelezea kibinaadamu vile ninavyoelewa mimi ili nisikuache.



Nitajirudishiaje "Hamu" sasa?

Unahitaji uelewa na Ushirikiano wa Mumeo/Mpenzi wako(rejea topic Umuhimu wa Furaha ya Mke) pia tambua Mabadiliko na kurekebisha mambo kiakili(jifunze upya kona zako za Utamu/raha) na kimwili(kula kiafya, fanya mazoezi, jipende)....umewahi kujiremba (paka vipodozi) na ukafikia kwenye kupaka Lipstic/Lipgloss ukahisi hamu ya Kuneng'enuka(au ni mie tu? Najitamani hihihihihihi).





Anyway kabla hujakimbilia kukubali kuwa umepoteza Hamu, jaribu kubadilisha utaratibu wa maisha yako ya kila siku (kama nilivyogusia hapo juu) na kufanya jambo ambalo unaamini na kujua kuwa unalipenda na unalifurahia. Unapofurahia siku yako na kupata muda wako peke yako kama "mwanamke" hata kama ni Nusu hakika siku yako itakuwa Njema sana na akili yako itatulia na hivyo kupata muda wa kufikiria mambo ya kufanya na Mumeo kama wapenzi. Unapokuwa na huzuni au hasira/mawazo/hofu siku itakuwa mbaya na hakika hutotaka/tamani kufanya Mapenzi au kuwa karibu na Asali wa Moyo wako.




Kama siku imekuwa na Mishughuliko mingi  kama Mama basi jaribu kutulia na kufanya yanayohitajika kufanyika.....kamwe usijipe presha ya kuwahi kumaliza ili kupata muda wako na hivyo kumfurahisha Mumeo....kumbuka Wewe kwanza, watoto halafu ndio Baba yao. Usiwafuate wale Mume wangu kwanza, Kids halafu ndio wao...(hawajui Thamani yao).




Ukipata muda(watoto wakilala), jipatie Dakika chache za kucheza na mwili wako ili ujue wapi panafanya nini na wapi hapako kama enzi kabla hujazaa. Mfano mie.....mmh itakuwa Too much Info....achana na hili.




Ukishajijua inakuwa rahisi kumuongoza Mpenzio/Mumeo na hivyo yeye kuachana na ile Kanuni ya "paji, midomo...shingo....matiti...kiuno...nyuma yabmagoti...ingia kati".Baada ya Kuzaa mwili wa mwanamke hubadilika na kilichokuwa kinamhemesha enzi.....sasa kinaweza m-put off.



Na ninyi wanawake mnaoshupaa kuwasukumia Wanawake  wenzenu Mpira wa "Wanawake ni kosa letu"....."Wanawake tunajitakia wenyewe"...."Wanawake hatujitumi". Mnapaswa kujifunza namna mwili wa Mwanamke unafanya kazi na wakati unajifunza tambua kuwa Wanawake tunatofautiana na hivyo mabadiliko unayokabiliana nayo wewe mwingine hana. Tuanze kujiheshimu na kutumia Muda zaidi ili kujijua badala ya kulaumiana hasa linapokuja suala la Ngono na Mahusiano baada ya Kuzaa.




Mwanamke  haitaji Mwanaume kufika Kileleni(kama anaujua mwili wake), lakini ili afike Kileleni akiwa na Mwanaume.....atahitaji Mapenzi na ushirikiano  wa Mwanaume  kimwili na kiakili. The moment mwanamke ana mawazo(akili haijatulia) hakutakuwa na Kilele wala kutaka/kufurahia Tendo.



Naheshimu na kuthamini Muda wako hapa, Ahsante kwa kuichagua Blog hii.


Babai.

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao