Skip to main content

Posts

Showing posts with the label kiswahili

Mind your Ughaibuni business...

 Nakumbuka miaka michache nyuma nilipokuwa Twita alijitokeza Binti mmoja nakuanza kuwaambia watu wa Ughaibuni(Nchi za Ulaya na Marekani) kuachana na Siasa za Tanzania na kufurahia maisha yako "mazuri" popote walipo Ulaya(popote nje ya Afrika)....natabua kua sio kila mtu Ulaya ana maisha mazuri(inategemea sababu yako ya kuishi huko) lakini nakubaliana nae. Wabongo wengi walimkandya/ponda kwa kudai kuwa anataka attention ya Bongo Twita sababu hakuna mtu anamfahamu, binti alijitetea na kusimamia alichokisema ambacho hakika nakubaliana nae. Watu wa Ughaibuni ambao hawaishi Tanzania  wanaguswa na Mabadiliko ya kisisa yanayoendelea Tz, hawa ni wachache sana ambao wana Biashara na pengine kumiliki ardhi(nyumba, mshamba n,k,) na wachache ambao hurudi nyumbani mara kwa mara, wengine wapo wapo tu na ndio huwa na kelele zaidi kuhusu Tanzania na Siasa zake. Unadhi utabadilisha nini  Tz na Kodi hulipi? Mind your Ughaibuni business and enjoy your High tax, cost of living and free Heathcare

Jinsi ya kujenga/kuza“character” ya mtoto wako.

Jambo wewe, Kulea Watoto Ughaibuni ambako kuna Kacha tofauti na Kacha tuliokulia nazo inaweza kuwa a bit confused, hasa kama umetoka zako Afrika (bongo as in Tz ikiwepo) na Kacha ya U-marekani mweusi. Unazaa Watoto na hujui uwalee katika kacha gani, nap engine unajiuliza hivi huku ulipo wanao wana kacha yeyote au wafuate kacha ya watu wanaofanana nao(Weusi wenzao aka Black Culture)? Unasahau kuwa kila mweusi wa Ulaya ana kacha yake aliokuzwa nao kulingana kabila lake na wapi anatokea Afrika.     Kwa kifupi nchi kama UK hakuna Black culture (wanalazimisha kuuingiza U-black Amarekan) bali kuna Culture za Afrika na Caribbean ila kwa wale wazazi waliokuja na U-black amerika kutoka Afrika basi huamini kuwa Culture ya Black amerika ndio Black culture Dunia nzima na hivyo kuindeleza. Hizo kacha   zetu za Afrika na Caribbean hazidumishwi na Taifa zaima la UK isipokuwa jamii husika ni kama ambavyo jamii nyingine ya wazungu kutodumisha Kacha zao Kitaifa kwasababu UK ina mataifa mengi hivyo k

Huge Microphones na yupo youtube...Kero zangu.

...ndio mnaita podcasts?  wameharibu youtube eti, au nimezeeka niachane nayo kama nilivyoiacha twita? Anyways, hujambo? Unaendeleaje na u-pre-menopause? Kama binadamu hakika kuna vitu vinakukera, binafsi nakwerwa na sehemu kubwa ya jamii ya online, hasa mamilionea na wamarekani weusi wanaoijua Afrika na kacha zake zote (nchi 57?) baada ya kwenda Ghana kwa wiki moja wa youtube na mi-microphone yao makubwa ka' wapo Mawingu FM. Halafu usinikumbushe wale wanajipanga kwenye vibox(zoom meetings) wanaanza kubishana oh my days.,,,ukute ni wivu wangu tu, maana  wanangu wakienda shule na Baba yako Kazini nabaki hapa sina hili wala lile. Ukiachana na hao kuna wale young single men and women wanashauri/fundisha wenzao namna ya kuishi maisha ya ndoa(Well I did that when I was younger but kama unakumbuka nilishauri kuhusu mahusino na ngono nilikuwa in one na was doing it). Najua unatambua kua sio tu Ndoa ni tofauti na maisha ya ndoa, pia Ndoa sio mahusiano japokuwa mahusiano ni sehemu ya ndoa. N

Mambo 7 Mumeo angependa umfanyie, ila...

...anaogopa kukuambia. Heri ya Mwaka mpya 2023 kwanza, leo google wamenitumia "data" bana, wanasema mwezi wa january kumekuwa na watu Laki nane na Eflu 11(8.11K) wametembelea Blog hii....nikasema Mayooo wane nimezeeka! nilikuwa napata idadi hiyo kwa Siku😅anyways, kama wewe ni mmoja wao basi nasema ahsante sana. Naendeleaje bila twita kwa Miezi 7? Vema kabisa, ahsante kwa kujali. nimegundua kuwa nina Muda mwingi sana wa kufanya mambo mengine muhimu kwa ajili ya afya ya Akili yangu. Ila baada ya kugusa miezi 4 hali ilianza kuwa ngumu nikawa nawakumbuka wote ambao tulikuwa tunabadilishana twiti mara kwa mara nikataka kushusha App, nikapata nguvu za kughaili, nikashida.  Vipi Mumeo na wanenu 3? Bado tumeshikiliana kwa mapenzi ya dhati, wanetu wanaendelea vema pia shukurani. Sema nini gharama na uhitaji wa kugawa "attention" kwa individual's umri na mahitaji yao Kiakili, Elimu, Malezi na "daily Activities" yameongezeka hyuuu!! Ila kwenye mambo mengine wan

Namna ya Kumshukuru Mumeo bila kusema "Ahsante".

Ukiachilia mbali(naipenda hii msemo) kuwa Ahsante ni "common" kitu ambacho kinaondoa uzito na maana yake, pia neno hilo ni rahisi na kila mtu anaweza kuambiwa bila kumaanisha. Mumeo sio mmoja ya hao watu, Mumeo ana umuhimu na uzito tofauti na watu wengine wote Maishani mwako(ukute ni mimi tu ndio nahisi hivyo).   Sasa kuanzia leo acha kukimbilia Ahsante kwenye kila jambo analokufanyia kama Mkewe na mlezi wa Familia(watoto wenu) yake.  Moja, Wakati mwingine mpikie/andalie chakula/kinywaji anachokipenda. Mpokee kama vile wanao wanavyompokea(bila kusema babaaa)....hiyo Pili. Shikamaneni hivi ktk Ndoa. Tatu, akikuudhi au ukiudhika na mambo mengine(unakaribia Hedhi) usimfanye alipe, hasa pale anapofika Nyumbani kutoka Kazini. Jaribu kumjulia hali, kumuacha apumzike na kisha ongea nae vizuri na kwa upendo/heshima. Nne, Ilinde Ndoa yenu pale ambapo mambo yqmegona kuendi vema, mfano Kapoteza Kazi/Tenda/Biashara imabuma, badala ya kumpa Moyo, Matumaini na Ushirikiano....we

Kwaheri Social Media(Twita)...

...hivi YouTube inahesabika kama Sosho Midia?  Kama sio basi Platform pekee naiaga kwa sasa ni Twitter. Sijawahi "kujiunga" na Instagram, Snapchat wala Tiktok. Kwanini? Ukiachilia mbali kuwa Muda unabadilisha watu(wanakua), vilevile vitu na mitazamo hubadilika kulingana na Tabia Uchumi/Nchi/Utamaduni....nadhani Twita imejaa wafanya Biashara kwa kupitia Ajenda binafsi/Harakati, Biashara ndogo ndogo na Biashara Utapeli (ulipie waliojifunza YouTube  bure), Biashara ya Miili(intimate picha/vid) oh bila kusahau Biashara ya "kuomba omba". Baada ya miaka kadhaa, nimegundua kuwa Twita hainifaidishi kwasababu sina Biashara(sikuzi Brand), hivyo sihitaji kuwa active na ku-engage na followers every few hours on daily. Kabla ya hapo nilikuwa Active sana kwenye Masuala ya Kisiasa(Naunga Mkono Upinzani Tz), baada ya Muda nikajitoa, uamuzi uliopelekea  "kurukia" zaidi issues rahisi rahisi ambazo zimejaa chuki/vita ya Wanawake vs Wanaume, hasira, kutokujiamini,

Dayaspora na Uraia Pacha...

Natumai unamalizia vema Mwezi huu wa 3(na Dayaspora). Suala la Uraia pacha ni zuri sana na lina faida nyingi kwa pande zote Mbili za Watanzania(Ndani na Nje), na Taifa lenyewe kwa ujumla(hasa kwenye Michezo Kimataifa, Uchumi, Afya na Elimu). Uwekezaji? Sio sana kwasababu kama Mtanzania utataka "kupendelewa" au "kupunguziwa" Masharti kutokana na Uraia wa Taifa hilo la Uzawa wako na hivyo Serikali kupoteza Mapato(Visa ya Uwekezaji na gharama nyingine) kutoka kwa Wawekezaji wa Kigeni.  Dayaspora wengi wanadhani kuwa Serikali inakwepa suala la Uraia Pacha kwa sababu ya Wivu, Chuki au Uoga wa "kupitwa" Kimapato, Ujuzi na Uzoefu. Kwaharaka haraka(uvivu wa kufikiri) inawezekana kweli ni Roho ya "kwanini wao", lakini ukiamua kutulia na kwenda ndani, utagundua kuwa  Taifa(Serikali) itapa Hasara zaidi kuliko mnavyorembesha Faida za Uraia Pacha. Hasara za Uraia Pacha zipo nyingi ila mie ninazo Nne tu. Tangu kupata Uraia wa Tanzania ni rahisi(kwa sababu ya M

Dayaspora vs Wazawa "groundini"...

Enzi Watqnzania "waishio" Twita walikuwa wakiwasimanga Diaspora kwa kujifanya wanajua kila kitu, mie nikaandika hii  kaisome tafadhali. Imekua kawaida kwa Wabongo wa Tz na wale wa Nje ya Tz kupishana mara kwa mara, huenda ni kwa Utani uliojificha kwenye yalioujaa Moyo ambayo ni ukweli au kuchangamsha Genge. Kuna wakati huwa naona "point" ya wale wa Bongo kuachwa wajadili na kuishi naisha yao na Siasa zao, lakini wakati huo huo naelewa kwanini Dayaspora wanapata hitaji la kutaka kutoa maoni/mawazo yao kuhusu Bongo kwasababu (wana Miradi, Ndugu na Jamaa...ni Kwao pia) wanaguswa kama unavyoguswa wewe. Kitu kingine ambacho Wabongo wa "Graundini" wanapaswa kujua au kujifunza kukubali kuwa,  "Dayaspora" wana-options tofauti kulingana na Muda gani ameishi huko aliko. Mtaani, Chuoni na Kazini yupo na watu wale wale wanaongea masuala tofauti kuhusu Nchi tofauti ambayo katika hali halisi ha-relate(inategemea kaishi huko nuda gani). Akija Mtandaoni anakutan

Hebu tuone Past life yako: Kuachwa/Telekezwa(2)...

Jambo, ni furaha iliyoje kukutana nawe na ahsante kws kuwa nami leo. Naendelea kukumbusha Maisha uliyopitia ulipokua angali mtoto ili kuona jinsi gani yana athiri Maisha yako hasa kwenye Mahusiano na watu wengine. Kuachwa ni jambo ambalo limezoeleka sana kwenye Jamii(hata za Ulaya ya hapa), kwamba utaachwa, utalia weeee kisha utanyamaza halafu Mzazi akirudi hautokumbuka tena(asiporudi tena baada ya miezi 2? Miaka 3?). Imani hiyo hufanya Wazazi wengi kufanya maamuzi yanayo umiza mtoto(hukumbuka ila hawajui ku-express hisia zao) bila kujua(kwa sababu hata wao walifanyiwa hivyo na they turned out just fine hivyo its okay). Kuachwa/Telekezwa na Mzazi kunafananaje? Mama ambae anamnyima mtoto Nyoyo kwasababu nyingine hana tofauti na Baba ambae hajihusishi (hayupo)kwenye maisha ya mtoto.  Mzazi aliefariki wakati kabla  hujazaliwa/angali ukiwa Mdogo....athari ni zilezile. Na je ni Matendo gani yanaashiria kuwa uliachwa/telekezwa na Mama/Baba na umeathiri? 1-Unapenda "attentuon" na ku

Hebu tuone Past life yako: Kutelekezwa/Achwa...

Umekuwa na mama yako kwa Miezi 9 mpaka 11 kama ulikuwa na bahati, wengine ni miezi 6 na wengine karibu Mwaka(Miezi 12). Ni mtu pekee unaemfahamu, na unahisi kuwa upo salama na unapendwa, sababu Mtu huyu sio tu amehatarisha maisha yake ili kukubeba na kukuleta Duniani. Mtu huyu ataendelea "kuteseka" sababu unataka ule x4 usiku wa manane, ataendelea kukupenda, kukulinda, kukufunza na kukujali.  Hayo yote hutokea kwa Miezi 3 ya mwanzo, baada ya hapo unamuona mtu huyo Nusu siku, kila unapoachwa unalia sana. Siku zinavyozidi kwenda ukaribu wako na mtu huyo unapungua na kilio chako kinapungua. Kitendo cha Mtu huyo ambae sasa unamtambua kama Mama(au Anty, Dada wa Kazi ndio Mama yako) kukutelekeza/kukuacha huwa kinaumiza sana. Sasa umekua na unajitegemea kwenye mambo mengi kama vile kucheza peke yako, kujivisha viatu/nguo nk. Lakini bado ni Mtoto na bado unamuhitaji Mama yako. Jana la leo Mama amekua nyumbani siku zima, unahisi furaha, upendo na kujaaliwa.....Mama anaamua kutaka kuto

Heri kwa Mwaka 2022, hebu tuone Past life yako...

Ni kawaida kuamini kuwa ulipigwa, tishwa, telekezwa/achwa kwa masaa kadhaa au miaka na Mama/Baba na umekua vema tu, huna shida yeyote Kisaikolojia/Kimwili/Kihisia. Unaendelea kuwapenda Wazazi wako despite the mateso walikupatia ilipokuwa kichanga, Mdogo na Kijana. Unaamini kuwa walichokifanya wazazi wako ndio kimesaidia kukufanya wewe uwe hivyo ulivyo sasa. Hakika bila wazazi wako kukulea walivyokulea usingekuwa hivi ulivyo ambavyo wewe unadhani ni "kawaida". Kukubali kuwa uliteswa/na kutengwa(rejea kipengele cha kwanza) na kuwa malezo hayo yamefabya uwe ulivyo sasa lakini una kutaa kuwa huna tatizo, tayari ni tatizo.  Nikukumbushe....Kupigwa, Kutelekezwa/achwa na kutishwa kwa awamu tofauti. Kupigwa : Ikiwa Mama/Baba kukupa maumivu ya mwili ambayo uliyachukia na kuogopa kwanini unatumia mbinu hiyo hiyo kuumiza mtoto wako? Mtoto anapofanya kosa(bado anajifunza), kwanini huchukui hatua na kumfunza/elewesha na kisha kumpa adhabu kulingana na umli wake ambayo sio kipigo.  Kwanini

Nguzo 5 za Mahusiano bora(Masikilizano/Maelewano).

Masikilizano/elewano huja wakati/baada ya mawasiliano japo ni Nguzo inayoweza kusimama peke yake kutegemea na tukio....mf:- wakati wa manunuzi makubwa(gari, nyumba), familia yenu iwe na watu wangapi?, Shule/Malezi ya watoto na pengine “career”. Unapowakilisha jambo/kero kwa mwenza wako ni vema kuwa katika hali ya utulivu(sio mara zote hufanya kazi hasa kama mwenzio sio msikilizaji mzuri). Utulivu wako husaidia kutoongea kwa sauti ya kushambulia na hivyo kuepeuka yeye kujitetea(bila shambulio hakuna pa kurudisha shambulio). Unapoibua suala ili lizungumzwe/jadiliwe nia ni kufikisha Ujumbe/kero na kupata muafaka(maelewano) na sio kung'aka na kuanza kugombana....hii hupoteza muda(kusumbua watoto kihisia/akili) na tatizo kuzimishwa badala ya kumalizwa. Kuzima/acha tatizo bila muafaka/maelwano kwa muda mrefu hupelekea mwanzilishi wa “mazungumzo" kuhisi kuwa hasikilizwi na hisia zake hazithaminiwi na mwenza wake. Hisia hizo hupelekea hasira(jitahidi kujizuia ili usifanye jambo mbaya)

Nguzo 5 za Mahusoano/Ndoa Bora...

Nguzo 5 za Mahusiano bora ya Kimapenzi ilikuwa topic maarufu sana 2007. Unakumbuka? Nilizielezea kwa kirefu kama utambulisho, wakati ule wengi walikuwa hawafahamu na baadhi hawakuwa wameziishi. Sasa tangu umeziishi nineona sio mbaya kama nikizirudia tena kwa pembe tofauti kidogi na ile ya 2007. Kabla sijaenda huko hebu nikukumbushe Nguzo hizo ambazo ni... 1) Mawasiliano. 2) Maelewano/sikilizano 3) Ushirikiano 4) Heshima 5) Kujali Ni rahisi kudhani kuwa wewe na Mwenza wako mnafanya yote hayo na kuamini kuwa Uhusiano wenu upo Imara. Utajuaje kuwa Mawasiliano ni mabovu? Mara ya mwisho kukaa chini na kuzungumza masuala yenu binafsi na yale ya kimaendeleo? Je, mwenzako anapokuja na hoja, huwa unasikiliza, jadili inapobidi na kufikia maelewano?  Ikiwa Mara zote mnaishia kubishana badala ya kujadili sababu mmoja wenu kapandisha sauti(foka) basi ujue uhusiano wenu hauna mawasiliano. Ni muhimu kutafuta namna ya kurekebisha na kuboresha kona hiyo. Njoo tena tuseme kuhusu Masikilizano kwa pembe t

Kama Mumeo anakupenda hatoruhusu ufanye haya...

Kutokana na wakati tuliopo ambapo  kuna "informations" nyingi kuhusu nini hasa Mwanamke anapaswa kufanya au kuwa na hivyo kuibua kukanganyana na kudanganyana kuliko wakati wowote ule wa maisha ya Mwanadamu(nimeongeza chumvi, sijui historia ya Mwanamke kabla ya 1900). Hata hivyo bado haiondoi  ukweli kuwa kuwa Mwanamke  mbele ya Wanawake wa kisasa ni Kazi ya Ziada. Mara nyingi sie(wewe na wenzio) wa Kisasa huwa tunaambiana kuwa mwanaume hana haki juu ya mwili wako au uamuzi wako wa nini unataka kufanya na mwili wako(mavazi/Urembo) which it is true  kama ni Mpitaji(boyfriend) lakini ukiwa  kwenye Ndoa/Uhusiano Mwanaume kuonyesha kuwa anajali nini unaweka juu ya mwili wako ni dalili kuwa mwanaume huyo anakupenda na sio kwamba hajiamini au anahofua kuibiwa. Wengi mnadanganyana kuwa Mume(au Mume mtarajiwa) akikukataza usifanye mambo kadhaa ni kuwa anaku-control, Nyanyasa au ni Dikteta kwenye uhusiano wenu. Tunasahau kuwa yeye ni mwanaume na hivyo anajua ni namna gani Wana

Muendelezo wa Twiti yangu ya "if he is hot, don't let yourself go"...

Miaka mitatu iliyopita niliandika kuhusu Wanaume wapenda nachuro byuti, kama ilikupta isome hapa  kisha tuendelee. Kwanza habari za leo? mie nipo Likizo, aina ya Likizo ambapo unafanya yote uyafanyayo unapokuwa nyumbani isipokuwa haupo nyumbani. Achana na hili. Kuwa shabiki wa "natural beauty" wakati unavaa Nguo, unaoga maji Safi ya Bomba(yana Kemikali), unavuta hewa kila siku(imejaa toxic), unakula vyakula vinavyotunzwa kwa kutumia Kemikali ili kuepusha magonjwa/wadudu, Ukiugua unatumia Tiba ya Kisasa, Unatumia Simu kuwasiliana  n.k. sio rahisi. Hakuna tatizo la mtu kupenda Urembo wa Asili na hakuna tatizo kwa yeyote anaependa Urembo wa kununua/jiongezea ailimradi tu hambadilishi na kukufanya uonekane mtu mwingine. Imekuwa ni kawaida kwa baadhi ya wanaume kusakama Wanawake wanaopenda kujiremba(usually wasio kuwa na pesa, maana makeups sio chee). Kutokana na maisha yalivyo  hivi sasa (Wanawake tunafanya yaliyokuwa yakifanywa na Wanaume pekee) na mabadiliko ya Hali

Dini inaweza kuyumbisha Ndoa/Uhusiano wako....

Heri ya J'Nne, Kama nilivyokuahidi Wiki (mbili na Siku Moja) iliyopita (bonyeza hapa kama ulipitwa) kuwa nitakuja nikukumbushe tu ni kwa namna gani Imani yako ya Dini inaweza kuyumbisha Ndoa au Uhusiano wako. Kwa kawaida wengi hudhani kuwa mtu anapokuwa Mumini Mzuri wa Dini au "anamuogopa" Mungu ndio atakuwa muaminifu, atampenda kwa dhati, atakuwa  mkweli, hatomuumiza na mengineyo mazuri mazuri. Ukweli ni kuwa Mtu wenye Dini mara nyingi huwa mwepesi kutenda "dhambi" au yale ambayo hayaruhusiwi na Dini zao akijua kuwa atasamehewa, sio tu na Mungu bali wewe Mwenza wake unapaswa kumsamehe. "Ikiwa Mungu aliemuumba anatuambia tusamehe iweje wewe ushindwe kunisamehe". Mazoea hayo ya kutegemea kusamehewa kila unapofanya makosa ya makusudi hupelekea upande mmoja kuhisi upweke na kuondoa Amani na Furaha kwenye Uhusiano /Ndoa. Hii inaweza kupelekea kujitenga na pengine kutafuta furaha Nje ya Muungano wenu. Hilo moja. Pili, Imani yako ya Dini inak

Social Media, kama ilivyo kwa Dini ni chanzo cha Ndoa/Uhusiano wako kuyumba.

Jambo! Siku kadhaa niliuliza "kiutani" kuwa Tatizo la Upungufu wa Nguvu za Kiume  kwa Vijana(chini ya Miaka 60)Nchini Tanzania au pengine Afrika linasababishwa na nini? Wawili watatu walidai kuwa Vijana siku hizi wanapiga Mkono(kujichua) kupitiliza, binafsi nilidhani kuwa ni Mawazo kutokana na Ukosefu wa Ajira(Kipato). Hivi majuzi nikakutana na Majadiliano ya Vijana (huku niliko) wakijadili ni namna gani Instagram inawafanya washindwe kuwa watendaji wazuri Kitandani. Sio tu kwamba hawawezi ku-perform bali pia wakifanikiwa kuinuka basi mwenzo huwa mreeeefu na hawafikii mwisho. Kwa kawaida(kiuzoefu) Mzunguuko wa kwanza unaenda kwa Dakika 45 bila Mwanamke kuhisi kuchoka na bila kubadilisha Mikao(unabadili movements za Kiuno/Nyonga), na hii ni kwa Mwanamke mwenye uwezo wa "kukojoa" zaidi ya  mara moja ndani ya Mzunguuko Mmoja(Hisabati nazo zinanifuata kila mahali...I don't like them huh!). Kumbuka baada ya Mwanamke(wa kawaida, sio sie special wa Goli 3 p

Jinsi ya kukabiliana na Mwanaume apendae kununa/susa/chuna...

Sio kwamba anapenda (hakuna mtu anapenda kununa)isipokuwa anatabia ya kununa(Kislani/Gubu). Kama ilivyo kwa sisi Wanawake , wenzetu pia huwa wananua ila kununa huko huwa wanakupa Jina lingine tofauti kabisa na Kisilani/Gubu ili wasihusishwe na "Uanamke"(wakiamini ni udhaifu na Mwanadamu pekee dhaifu Akilini mwao ni Sisi). Utamsikia anang'aka na kusema hana gubu/hajanuna/hajajitenga isipokuwa "siku yangu imeharibika/imeanza vibaya", "usinisumbue nina Mawazo", "Nahitaji muda wa peke yangu kutuliza akili", "Najisikia vibaya" na ikiwa alipoteza Mzazi au Wazazi wote basi hiyo itatumika zaidi..."nimewakumbuka Wazee" nakadhalika. Tabia hiyo inakera na inaumiza sana, inakupa wewe Mke mtu upweke wa hali ya juu. Inaweza kukupa ushawishi kwa ku-check na Ex au hata kutamani kutafuta kipoozeo. Hivyo kusababisha mtikisiko kwenye Ndoa/Uhusiano wenu ikiwa hakuna Mawasiliano au hamjuani(hamjasomana tabia, kwamba bado ni Wapenzi wap

Rudisha Heshima ya Ndoa: Jinsi ya kuepuka Ulalamishi/Kosoaji too Much.

Kama wewe ni Mkosoaji, hii inakuhusu zaidi, Karibu. Ndoa kama Ndoa ni ngumu na inahitaji  kufanyiwa kazi kila Siku kutoka pande zote mbili. Ndoa  ni ya wawili sio jukumu la Mke tu au Mume tu, bali  nyote kwa pamoja. -Angalia yaliyo Chanya zaidi ya Hasi. -Kubali kuwa Makosa yako kimaisha kabla yake(Mwenza wako) hayamuhusu....kwamba kutotimiza Ndoto zako ni Makosa yako wewe na yeye hausiki. Kwa pamoja  manaweza  kukamilisha Ndoto mpya kama Mke na Mume kwa Ushirikiano na Support bila Kumlazimisha afanye yale utakayo wewe kufidia uliyofeli kabla hajakutana. -Tambua kuwa unaweza kuwa unamjua Mkeo/Mumeo vema sana baada ya kumsoma lakini bado huwezi kamwe kusoma Akili yake. Epuka kusema "najua unachofikiria" "najua unachokitafuta", "najua kwanini unafanya hivyo" n.k....jifunze kutumia maneno "wakati mwingine unanifanya nadhani blah blah blah"...if anything. -Kubali kuwa wewe haujakamilika, kwasababu mwenza wako hakukosoi au halalamiki haina m

Rudisha Heshima Ya Ndoa: Mwenza hana Jema, kila siku Kukosoa...

Kukosoana ni jambo jema na muhimu ili kusaidia kurekebisha Tabia ndogo-ndogo ambazo ni mbaya lakini kumkosoa  Mwenza wako mara kwa mara (kupitiliza) bila wewe mwenyewe kujali kuwa unakasoro zako ambazo anazivumilia ni wazi utakuwa Mnyanyasaji. Unyanyasaji huo utamfanya mwenzio kujisikia vibaya na hivyo kusababisha:- -Maumivu ya Hisia na Akili. -Kumfanya Mwenzio ajione hana thamani au Umuhimu kwenye Ndoa yenu. -Uoga/Hofu  kwenye Ndoa yenu -Kuondoa Furaha na hivyo kujitenga kihisia -Kukosa Amani -Msongo wa Mawazo Kwasababu Mwenza wako sio Mlalamishi au Mkosoaji wa mara kwa mara haina maana kuwa wewe ni Mungu na hukosei, kwamba wewe ni next to perfect(hakuna binadamu asie na Kasoro) ndio maana Mkeo/Mumeo hajawahi kukukosoa au kulalamika. Ukweli ni kuwa, baadhi ya Weza huwa "wanakurekebisha" kwa vitendo, kwamba anafanya exactly vile unapaswa kufanya au kwa kukupa "hints" bila kuumiza Hisia zako wala kusababisha ujisikie vibaya. Asipo pata matokeo ndio ana