Skip to main content

Jinsi ya kujenga/kuza“character” ya mtoto wako.

Jambo wewe,

Kulea Watoto Ughaibuni ambako kuna Kacha tofauti na Kacha tuliokulia nazo inaweza kuwa a bit confused, hasa kama umetoka zako Afrika (bongo as in Tz ikiwepo) na Kacha ya U-marekani mweusi. Unazaa Watoto na hujui uwalee katika kacha gani, nap engine unajiuliza hivi huku ulipo wanao wana kacha yeyote au wafuate kacha ya watu wanaofanana nao(Weusi wenzao aka Black Culture)? Unasahau kuwa kila mweusi wa Ulaya ana kacha yake aliokuzwa nao kulingana kabila lake na wapi anatokea Afrika.

 

 Kwa kifupi nchi kama UK hakuna Black culture (wanalazimisha kuuingiza U-black Amarekan) bali kuna Culture za Afrika na Caribbean ila kwa wale wazazi waliokuja na U-black amerika kutoka Afrika basi huamini kuwa Culture ya Black amerika ndio Black culture Dunia nzima na hivyo kuindeleza. Hizo kacha  zetu za Afrika na Caribbean hazidumishwi na Taifa zaima la UK isipokuwa jamii husika ni kama ambavyo jamii nyingine ya wazungu kutodumisha Kacha zao Kitaifa kwasababu UK ina mataifa mengi hivyo kinder sio sahihi(hii ni topic ya kisiasa zaidi sitaki Kwenda huko).



Sasa, kulea Watoto kwakufuata mkondo wa ulioishi wewe kwa kufuata Kacha yako bila wao kuishi kwenye mazingira husika binafsi naona sio sahihi, kulea watoto katika miongozo ya tabia njema na kufuata maadili/values za Dini(sio za makanisa ya kisasa ones) ni muhimu. Pamoja na hayo pia ni vema kama wazazi kuweka nguvu ya ziada kwenye kujenga “character” zao….na hii ndio topic ya leo.

 

Unajengaje character/tabia ya Watoto wako ili wakawe na mwanzo mwema out there?

Kwa kawaida unaanza mapema sana, kabla mtoto hajafikisha miaka 3, unamfunza kusalimia, kuomba, kusema ahsante na kusema samahani. Jinsi anavyokuwa unaendelea kumfunza na kurudia mara zote unahisi kuwa  ni muhimu…unajua jinsi inavyokua.

 

 Kila hatua mtoto anafika unarudia (mara kibao, kwa sababu huwa wanasahau) na wakati huo huo unaongeza vitu vingine mfano kusafisha kila anapomaliza kucheza, kula, kuonga, kucheza pamoja na ndugu/watoto wengine, kusalimia watu baki, kuchangia sanamu…unamfunza kwa vitendo(mnafanya kila jambo pamoja).

 

 Sasa kafika Miaka 6(yupo darasa la 2/3) Pamoja na masomo ya shuleni pia unatakiwa kuanza kumfunza wapi ni kawaida na salama kushikwa/shika, bila kujali jinsia. Hakikisha anajua kuwa hakuna mtu anapaswa kumshika makalio, sehemu ya mbele na kamwe hakuna kuvua nguo zake kwa mtu yeyote ambae sio Mama/baba yake, na ikitokea mtu kamgusa aje kukuambia(hakuna siri)….natambua hii inategemea na mazingira, kama mnaishi na watu wengi au anaenda kukaa na watu  baki  wewe ukiwa kazini basi ni vema kuanza mapema.

 

 -Kujiheshimu na kuheshimu watu wengine(bilakujali jinisia): Hii inanzia mapema ikiwa wapo Zaidi ya 2. Wao kwa wao wanatakiwa kuheshimiana kabla hawajaenda kuheshimu Watoto wengine nje ya kwao….mf, Kaka mtu anataka mdogo wake aende kucheza nae, Mdogo mtu akisema sitaki kucheza, kaka mtu anapaswa kuheshimu uamuzi wa mdogo wake. Au wanachokozana na mmoja anasema Hapana, mchokozi anatakiwa kuheshimu Hapana ya mwezie.

 

-Majukumu: Mfunze na msaidie ajue majukumu yake na namna ya kuyatimiza, mf kwa kuanzia ni lazima aoge, alainishe ngozi, achane/tengeneze nywele, avae vizuri(we presentable), asafike chumba chake n.k.(zingatia umri).

 

-Kukubali makosa na kuomba radhi (ndio Accountability?): Hii ndani kwetu imeanza mapema sana kwasababu tulichagua kuwa Watoto humu ndani wana haki kama wanadamu na kwamba wao sio bidhaa zetu, kwamba hata tukikosea kama wazazi bado tupo sahihi na hakuna kuomba radhi. Mtoto akija kwako na kulalamika kuwa umemkosea na unajua kabisa umemkosea, omba radhi. Na mfunze mwanao hivyo, rahisi ikiwa ana wadogo zake.

 

-Ushirikiano: Kufanya kazi kama timu ili kufikia lengo, iwe shuleni au nyumbani katika kusafisha nyumba, kuandaa/tenga  meza/mkeka/jamvi kwa ajili ya chakula, kucheza na wakati mwingine kusaidia kazi nyingine pale inapobidi.

 

-Shukurani: Ajue kushukuru  sio tu kwavile mnamnunulia vitu atakavyo, bali pia kwa sababu kaamka akiwa salama, ana afya njema ana wazazi wote wawili na wadogo/wakubwa wake ambao wanampenda na vitu vingine alivyo navyo kwa wakati husika.

 

Msimamo: Asimamie anacho kijua na kuamini (inategemea na Imani yenu ya Dini na mambo mengine mnayomfunza kulingana na uzoefu wenu)ambacho ni kizuri/chema sio kwake tu bali kwa jamii nzima inayokuzunguka.


-Utu: Mfunze mwanao aweke mbele utu, kwa kukumbuka watu wengine katika maombi na atoe Sadaka kwa kusaidia wengine wenye uhitaji(hii inafunzwa zaidi Kanisani)awe mwenye huruma lakini asivuke mipaka.

 

-Kujizuia:Ajue kujizuia linapokuja suala la kukabiliana  hasira, frustrations hii hujitokeza pale unapomfunza mf Hisabati halafu hapatii, kila akirudia bado anakosea….hapa ndio pa kuanzia kumfunza self-control. Itachukua muda lakini ataweza. Hii pia itamsaidia kujua how to pale wewe mzazi nay eye mkifikia kwenye suala la kukabiliana na Hisia mbali mbali.

 

 Mtoto akiyajua hayo na kuyafuata/tekeleza ndio atakuwa amejenga tabia nzuri na itamrahisishia kwenye kuikuza as anaendelea kukua, kumbuka kila umri mtoto anafikia anakutana na changamoto tofauti ambazo hawajawahi kukutana nazo na hivyo hajui namna ya kukabiliana nazo. Ila mtoto akiwa na msingi mzuri kama nilivyotaja hapo awali inawasaidia sana kupambana na Maisha. Hayo yote yatajirudia lakini kwa namna tofauti akifikia umri wa ku-date na hatimae kujenga mahusino ya  baadae Ndoa.

 

Sote tunajua Maisha ni magumu, tujitahidi kuwasaidia Watoto wetu ili wawe na Maisha mepezi kiasi sio  kiuchumu tu, bali kitabia pia. Pole kwa kusoma neno “Kacha” mara 820 😐.

 Babaiiii.

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao