Skip to main content

Posts

Showing posts with the label wazazi

Imani ya Dini ni Msingi mzuri kulea watoto....

  Pamoja na kusema hivyo haina maana kuwa Dini ndio kimbilio kwasababu ukizidisha huko Dinini pia unaweza kuongeza viungo kwenye matatizo yako ya akili au kuongezea mengine. Unapokuwa unafuata Imani ya Dini (Traditional Churches na Uislamu, hao matawi ya ukristo wa kisasa aka MATAPELI mie siwatambui) inakusaidia kuishi kwa heshima na kufuata princimples zake, unajua nini chakufanya(unamkimbilia Mungu) unapopata matatizo   mfano kupoteza kazi, migogoro kwenye urafiki, wazazi, ndoa, ndugu au hata pale unapoyumba kiimani.   Sio tu kwamba unakuwa na kimbilio (Mungu) bali pia unakuwa na Community kutokana na Asilia yako(Kabila) ambayo kwa kiasi kikubwa mnakuwa mnajadili masuala mbali mbali ya kimaisha na mnakuwa na activities hata kama ni mara moja kwa Mwaka, mnakuwa karibu kwavile mnamisingi inayofanana, mnaiheshimu na hivyo inakuwa rahisi kuepuka “Drama” ambazo ni chachu ya matatizo ya Akili.     Kutokana na muibuko wa social media, kumekuwa na watu wakipeana mioyo au kufundishana

Mtoto wa kambo(part 1)...

Mtoto wa kambo sehemu ya kwanza.... Kambo maana yake nini? Ikiwa mtoto alizaliwa nje au kabla ya ndoa nae anaitwa mtoto wa kambo? au ni kwa wale waliozaliwa ndoani halafu  ndoa ikafeli au mzazi mmoja kafariki halafu  baba/mama kaoa/olewa tena?  Mnaona mlivyo haribu/changanya mambo baada ya kuua umuhimu wa ndoa na kujenga familia? Mtoto kabla na nje ya ndoa (Wanaharamu) huwa hawajulikani/hawana umuhimu(kwa Waislamu hii bado imesimama). Nimekukwaza? ndio ukubwa huo.😁 Mama/baba wa kambo inatumika zaidi Mikoani, huku kwetu Pwani tunatumia sana Mtoto wa kufikia(kwamba umefika   kimapenzi kwa mwanamke/mwanaume ukamkuta mtoto kutoka ndoa iliyopita?)…sina uhakia. Nitatumia maneno mtoto na watoto interchangeably. Nani alipitisha sheria ya kulazimisha watu wawapende watoto waliowakuta kwa watu waliowadondokea kimapenzi? Yaani ukionyesha huna habari na uzao wa mwanamke/mwanaume kabla yako basi unaitwa Mwanga, unaroho mbaya n.k. Utapendaje mtu wala humjui na hana faida kwako?  Natambua kuna msemo

Jinsi ya kujenga/kuza“character” ya mtoto wako.

Jambo wewe, Kulea Watoto Ughaibuni ambako kuna Kacha tofauti na Kacha tuliokulia nazo inaweza kuwa a bit confused, hasa kama umetoka zako Afrika (bongo as in Tz ikiwepo) na Kacha ya U-marekani mweusi. Unazaa Watoto na hujui uwalee katika kacha gani, nap engine unajiuliza hivi huku ulipo wanao wana kacha yeyote au wafuate kacha ya watu wanaofanana nao(Weusi wenzao aka Black Culture)? Unasahau kuwa kila mweusi wa Ulaya ana kacha yake aliokuzwa nao kulingana kabila lake na wapi anatokea Afrika.     Kwa kifupi nchi kama UK hakuna Black culture (wanalazimisha kuuingiza U-black Amarekan) bali kuna Culture za Afrika na Caribbean ila kwa wale wazazi waliokuja na U-black amerika kutoka Afrika basi huamini kuwa Culture ya Black amerika ndio Black culture Dunia nzima na hivyo kuindeleza. Hizo kacha   zetu za Afrika na Caribbean hazidumishwi na Taifa zaima la UK isipokuwa jamii husika ni kama ambavyo jamii nyingine ya wazungu kutodumisha Kacha zao Kitaifa kwasababu UK ina mataifa mengi hivyo k

Wenye Ndoa, tuache kuwabadilisha Waume Zetu.

Sasa kabla hatujaanza kumsimamnga Wifi kambadilisha Kaka yetu, tuangalie kwanza Wifi alikuwa nani kwao, na je uamuzi wa Wifi kupumzika ki-career baada ya Kuzaa ni kum-support Kaka yenu(Mumewe) ki-career au ni njia tu ya yeye kula Mahela ya Kaka yenu? Je ndugu zake waliokuwa wakimtegemea hawateseki kwa kukosa "kipato" kutoka kwa Dada/Mwana wao? Kwenye era hii ya Sosho Midia inabidi uwe makini sana maana info ni za kumwaga(tofauti na 2007 nilipoanza  kublog), ni kweli baadhi zinasaidia hasa zile za Medical kutoka kwenye Site za Shirika la Ugojwa husika au Shirika la Afya Duniani. Lakini linapokuja suala la Ndoa au mahusiano, ongeza umakini kwasababu Ndoa hazina Kanuni Moja na watu hatufanani hata kama tulikaa tumbo Moja Miezi 9 na kuzaliwa kupitia Njia mooja na siku Moja bado tutatofautiana kwa kiasi fulani. Maisha magumu, kila mtu anatafuta views na clicks siku hizi, mara zote(kama Wanasiasa) watu huamua kuongea au kuandika mambo ambayo wanajua watu watakuja mbio ku

Akisema "tafuta mwingine, mie siwezi/nimechoka"....

...hamaanishi kwamba ukatafute  kweli mwingine, anachomaanisha ni kuwa "nibembeleze na unihakikishie kuwa utanivumilia" mpaka nitakapo kaa sawa Kihomono au kupona(kama alikuwa anaumwa)....Za Miezi Miwili/Mitatu? hello, jambo jambo!! Kwa kawaida Mume anapopatwa na tatizo kubwa litakalomfanya ashindwe kutekeleza Majukumu yake kama Baba na Mume, Mwanamke atavumilia na kumuuguza, kumpa Moyo na Matumaini. Lakini Mwanamke akijifungua(zaa) achilia mbali kuugua....katoa Uhai wa Mtu salama baada ya Miezi 9 kukaa na kulala kwa tabu. Mara zote kipindi hiki huwa Kigumu sana japokuwa kasumba ya Jamii "kukuharakisha" upone haraka huficha ukweli kuwa Mwanamke anapojifungua hukabiliana na mambo mengi Kiafya(kimwili, kihisia na kiakili). Hali ambayo hufanya baadhi ya Wanaume kuamini kuwa Mimba na kuzaa ni "cha mtoto" tu, sio kazi(kama alivyo pizi ndani ya dakika zake 3 kwa utambu uliodumu kwa sekunde 90)....hakuna ugumu wowote, fyatueni tu. Kwa kawaida(uzoefu wa

Kubishana/Fokeana Mbele ya Watoto...

....kuna Ubaya? Baadhi ya watu wanasema SIO vema kwa Watoto wenu kuwaona mkigombana iwe ni Ugomvi Mkubwa(Pesa za Savings acc zimenda wapi?) au ule mdogo(kwa makusudi hujasafisha Bafu). Nyie huwa hamgombani? Kama hamgombani basi mmoja wenu anaishi "kisiri", ulie nae sio yeye...au mmoja wenu anamuogopa mwenzie. Mie ni that Woman ambae nina Sauti kali/ya juu which is a shame kwasababu huwezi kujua kama ninafoka au ninaongea kawaida, sasa ukitaka kuongea kama mimi ni wazi kuwa Utakuwa unanifokea kitu ambacho kitanikera na hapo moto kuwaka...umeona? hihihihihi nataia!! Wazazi wengi hujizuia  kuanzisha "Mabishano" mapema na hivyo, husubiri mpaka Watoto watakapokwenda Kulala ndio wanaanza kubisha/fokeana. Nakumbuka wakati nakua Baba na Mama walikuwa wakifokeana Chumbani kwao(wakiamini tumelala) kumbe some of us (Mie) tulikuwa tunaenda kusimama Mlangoni na kuwasikilia ili tujue kama wanabishana/gombana au wanaongea kawaida tu na kama wanagombana, wanagombania n

Mzazi Mkali Vs Mpole....

Hello! Utakoma na Post za Wazazi na Watoto mahali hapa, ni maisha niishiyo sasa na sio mbaya kama nikichangia uzoefu wangu ambao pengine unafanana na wako na hivyo kukufanya kujisikia nafuu kuwa haupo peke yako au ukanishangaa. Vilevile inawezekana kabisa ukajifunza jambo! Hofu yangu kuu ni Waanangu kuwa na Tabia mbaya chini ya uangalizi wangu, kutokuwa na Heshima kwetu Wazazi wao na Watu wengine. Hofu hii ndio iliyochangia mimi kujitolea Mhanga na kuwa Mama wa nyumbani kwa Miaka 3.  Sikutaka Wanangu waje na tabia za "Nursery assistant".....Babuu alianza Nursery akiwa Mchanga as bado nilikuwa na ile " I can do all, independent woman".....untill Mwanangu alipoanza kunikataa na kulia kwa Uchungu kila nilipokuwa naenda kumchukua! Vilevile alipofikisha Miezi 8 akawa na "vijitabia" ambavyo siku pendezwa navyo.....Solution? nikapunguza Masaa ya Kazi na Nursery(so kutoka full time akawa anaenda kwa 5hrs). Niliamini(bado naamini) kuwa Mtoto anahitaji

Kulazimisha Mtoto awe na Mawazo....

Pengine ni ngumu kujua tofauti ya ku-share information kwa nia ya kuwafanya watambue "Asili" yao, wajifunze kuhusu Upande wa pili(kwa wale waishio Ughaibuni) na kuwapa watoto mawazo. Natambua kuwa kila Mzazi ana namna yake ya kulea na kufunza wanae, na kamwe sitokufundisha namna ya kulea wanao tangu mie mwenyewe  najifunza kila siku. Lakini tukumbuke kuwa kuna "Common Sense".....huitaji Elimu wala Uzoefu kuitumia. Unakumbuka ulipokuwa Mdogo na Mama au Baba au mtu yeyote wa karibu anaanza Hadithi za "Kaka/Dada" yako aliezaliwa na kufariki.....kisha ukaanza kuwaza ingekuwaje hivi sasa kama angekuwepo? Unawaza huko aliko je anafuraha, ana-toys,? unakuwa na Maswali kibao ambayo hayana Majibu. Mtoto anakosa usingizi kwa Mawazo au Uoga na akilala anamuota "dada/kaka". Wazazi hapa hudhani/amini kuwa Mtoto ana connection na "mwenzie"....lakini ukweli ni kuwa anasumbuka Kiakili na Kihisia. Pia umewahi kutambulishwa kwa Ndugu ya

Kujiamini kwa Mtoto kunaanza lini?

....Watoto wa "Ulaya" wanajiamini sana, je kuna namna ya kulea mtoto ili akikua ajiamini kama wa Ulaya? Mkaka mmoja aliniuliza. Nadhani wengi wetu tumeaminishwa Mengi ya Ughaibuni ni Mazuri/Mema....lakini katika hali halisi sivyo. Kuna soko zuri sana la Vitabu/Vipindi vya TV vinavyofunza Wazazi namna ya kulea watoto wenye Kujiamini. Ni tatizo la Wazazi husika ambao walilelewa "Kimaendeleo" na hivyo kuhofia kuwa watoto wao watakuwa kama wao. Hofu hiyo inawafanya wazazi kuwa-overprotect watoto. Nahisi tu sina uhakika. Kujiamini kunategemea zaidi na Malezi(nakubali) lakini sehemu kuwa ya Mtu/Mtoto kujiamini inatokana na yeye mwenyewe alivyoumbwa. Niliwahi kugusia Bloguni hapa kuwa kuna baadhi tumezaliwa hivyo(tunajiamini) lakini pia wapo ambao hawajiamini mpaka wafunzwe/himizwa/pewa Moyo/saidiwa kujiamini. Naamini Watoto wa Afrika(well Tanzania wa kizazi kileeee) tunajiamini kwasababu tulitumia muda mwingi kujifunza kimwili na sio kihisia kama watoto

Wanawake hatupendani....usimbee awe Jaji sasa!

Sina hakika kama hii ni Imani tu au ni kweli, Naturally Wanawake hawanipendi mie binafsi(imagine ningekuwa mzuri sasa!) ila Wanaume wanananipenda(napatana zaidi na Wakibaba kuliko Wakimama). Kuna siku Mfanyakazi mwenzangu akanijia kwenye Dawati langu akanambia "dinah unajua nakuchukia".....mie nkacheka halafu nikamwambia "sio peke yako, nimezoea kuchukiwa na wanawake"....wewe ungesema is because i am Black! Sasa, hii "wanawake hawapendani" ipo kila Nchi Duniani.....kila mtu anaibuka na sababu yake kwanini hasa hatupendani. Baadhi wanadai ni Wivu wa kike(umbile/kupendeza/mafanikio/kuwa na easylife) na wengine wanasema ni mambo ya Homono tu. Mie sio kwamba nachukia wanawake bali sipendenzwi na tabia ya baadhi ya wanawake wanaofanya maamuzi ya Kipumbavu, kama vile kutojikinga dhidi ya Mimba, au kujitegeshea kushika Mimba ili tu waolewe au wapate sehemu ya Kipato ya Mwanaume husika. Sipendi mwanamke ajishushe ili kuonewa kirahisi. Vilevile

Marehemu....

Mungu aendelee kuwapa Mwanga wa Milele, Amina......hebu ngoja kwanza!! Wameenda wakiwa "wamelala" sasa mwanga wanini wakati wamelala? Ile kasumba ambayo mimi naona ni ubinafsi au kutafuta/taka kuonewa "huruma".....yaani marehebu baba blablabla....Marehemu sijui nani blablabla. Marehemu Baba wa Taifa anatuangalia na kugalauka Kaburini......yaani aache kufanya yaliyomuhimu huko aliko abaki kutuangalia sisi huku na kugalauka kutokana na ujinga au makosa na shida zetu! Sidhani kama hao marehemu huwa hata wanatuombe tulio hai tuendelee kupata "kiza" cha milele ili tusiamke na kukabiliana na shida za Dunia. Mtu akienda, ameenda na huna budi kukubali kuwa kaenda na anaendelea na maisha mengine bila wewe....dizaini ukifa unasahau all bout Dunia na watu wake.....Mambo ya new start...new life. Si wanasema unakuwa "declared dead only" kama Ubonko (Ubongo) haufanyi kazi, sasa kama Ubonko haufanyi kazi kumbukumbu za ya Duniani watazitoa wapi? (In my