Skip to main content

Kujiamini kwa Mtoto kunaanza lini?

....Watoto wa "Ulaya" wanajiamini sana, je kuna namna ya kulea mtoto ili akikua ajiamini kama wa Ulaya? Mkaka mmoja aliniuliza. Nadhani wengi wetu tumeaminishwa Mengi ya Ughaibuni ni Mazuri/Mema....lakini katika hali halisi sivyo.



Kuna soko zuri sana la Vitabu/Vipindi vya TV vinavyofunza Wazazi namna ya kulea watoto wenye Kujiamini. Ni tatizo la Wazazi husika ambao walilelewa "Kimaendeleo" na hivyo kuhofia kuwa watoto wao watakuwa kama wao. Hofu hiyo inawafanya wazazi kuwa-overprotect watoto. Nahisi tu sina uhakika.





Kujiamini kunategemea zaidi na Malezi(nakubali) lakini sehemu kuwa ya Mtu/Mtoto kujiamini inatokana na yeye mwenyewe alivyoumbwa. Niliwahi kugusia Bloguni hapa kuwa kuna baadhi tumezaliwa hivyo(tunajiamini) lakini pia wapo ambao hawajiamini mpaka wafunzwe/himizwa/pewa Moyo/saidiwa kujiamini.






Naamini Watoto wa Afrika(well Tanzania wa kizazi kileeee) tunajiamini kwasababu tulitumia muda mwingi kujifunza kimwili na sio kihisia kama watoto wetu wa leo. Tulianguka kwenye Mchanga/kokoto, tulipigana, tulijikwaa kwenye Mawe na Misumali, tulianguka kutoka juu ya Miti na Milima.....yote haya yalitokea tukiwa peke yetu, hakukuwa na Mama/Baba akisisitiza...."usipande mti utaanguka".






Watotoo wa siku hizi hawapati nafasi hiyo kwa  kwasababu  nyingi tu ila kuu ni Uovu, Maendeleo/Uzungu, tunawaachia watumie(chezee) Simu/Tablets/PC/TV zaidi kuliko kucheza na "nature"  wakiwa na watoto wenzao(wajifunze bila mwalimu/Mzazi.





Watoto ambao wamekuwa/lelewa wakidekezwa kwamba Mama/Baba anawapigania ikiwa wamegombana na rafiki zao (watoto wenzao) au pengine kuonewa......badala ya kumuelekeza namana ya kujitetea na kuwa Imara ili asionewe wewe Mama/Baba unamkingia kifua.





Akiwa anacheza Park(kwa sie wa huku) basi unamfuatilia ili asianguke na kuumia, akikimbia unamwambia "kimbia taratibu usijikwae", akirukaruka na wenzie unasisitiza "kuwa mwangalifu, usijiumize/umiza wenzio".....yaani mtoto  hapati nafasi ya kuwa Mtoto na kujifunza mwenyewe.





Sasa mtoto kama huyu akiwa mtu mzima hatokuwa akijua namna ya kujitetea/pigania haki yake na hivyo atakuwa akionewa na kupoteza Kujiamini. Natambua kuwa ni ngumu(kama mzazi) lakini ni vema na ni muhimu kumuacha mtoto ajifunze(ukimfunza) kupigania haki yake ila sio kwa kutumia Nguvu/Ugomvi wa Maungoni.





Unakumbuka enzi...(well inaezekana na kwetu tu), ukienda kwa Mama/Baba kushitaki huku unalia kuwa "Mona" kakuumiza/piga au chukulia kitu chako.....Mama/Baba anakukurupusha na kukuambia nenda kamwambie "Mona" akurudishie kitu chao.....kama kakupiga basi unaambiwa "siku nyingine akikupiga, mrudishie na ukarudi hapa unalia nakuongezea(unapigwa)".




Siku zikipita hujapeleka Mashitaka, Mama/Baba anauliza wewe na Mona/rafiki zako mnacheza vizuri au bado mnagombana(hapa Mzazi anataka kujua kama unaonewa au ni mambo ya watoto), ikiwa unaonewa(wanaku-bully) then issue inahamishiwa kwa Walimu/Wazazi wa Mtoto ambae ni Muonevu.





Hiyo ni kwa Watoto wakubwa, unamfundishaje mtoto ambae ni chini ya Miaka 5 ambae yupo Shule(ya kucheza)....sikufunzi namna ya kulea mwanao lakini nitakupa uzoefu wangu since nina vitoto viwili vya umri huo.




Stori Time(sijazifanya hizi Kitambo eh): Mwanangu Babuu ni Mvulana ambae hana aibu na anapenda kujieleza(akianza kuongea hamalizi) alipoanza Shule(Vidudu) kila mtu akawa anamfurahia.....lakini kuna ile mitoto Migomvi na Mikubwa(vidudu watoto wenye  miaka Miwili na Nusu Mpaka Mitano) na wawili kati yao walikuwa wanamsumbua Mwanangu. Kila siku akirudi anashtaki kuwa mmoja wa hao wenzie wamemchokoza,





Roho ilikuwa inaniuma sana(niliapa ikitokea mtu anamuone mwanangu napigana) lakini nikamwambia tu kuwa kesho wakikuchokoza tena waambie "stop doing that, it is not nice" na wakiendelea nenda kamwambie "Mwalimu"......mashtaka yakaisha. Term nyingine ikaja na mashtaka yakaanza tena, mara hii nikaenda kuripoti kwa Mwalimu wake, so Walimu wakaanza kufuatilia na kutoa time out kwa Wachokozi. The wachokozi wamekuwa Marafiki zake....sort of.





Siku moja Toto la Kinaijeria(you know how i feel about these watu).....likaanza kumuita mwanangu(mbele yangu)....."Babuu you are so silly".....mwanangu akajibu...."no am not silly, dont call me silly".....lile toto likawa linaendelea huku linacheka(mama yake kimyaaa)....nikamwambia yule mtoto "B kasema usimuite Silly, can you stop please"! Mama yake akasema...."no he didn't call him silly"....and i was excuse me? akarudia tena.....si nikamlipukia nikianzia na "You Naigerians and lies....(kwenye kuongea hunipati, ila  sijui Kukunja Ngumi  Mzaramo mie hihihihihi).....Mama wa Kipopo ananiogopa huyo!

theeeee End,

Ahsante kwa kuichagua Blog hii.

Babai.

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao