Skip to main content

Posts

Showing posts from June 8, 2014

Ugumu wa Masomo...

Hisabati....Hisabati....Hisabati! Sikufanya Mtihani wa Mwisho kwasababu nilijua nitapata LieFu.....sikulitaka Li-F kwenye Cheti changu. Nikapiga Mahesabu ya namna ya kuepuka F kwenye Cheti changu cha Fom Foo....nikapata jibu deshi-deshi, ila mie nilitaka Deshi moja tu so siku ya Mtihani sikutokea.....nikajipatia Mathematics-!! Nilifurahiiiiiii. Nazipenda Hesabu (kuhesabu hela na Pea za viatu tu) ila kama somo hapana, sio kwamba nilikuwa siziwezi la hasha! Nilikumbuka Kanuni zote, nilifuata na kupatia njia ili kupata jibu. Tatizo lilikuja Muda napoteza muda mwingi kuhakiki jawabu matokeo yake najikuta nimefanya Maswali 5 out of 25=Efu...SIPENDI Somo la Hisabati sababu speed ya akili yangu ni a bit slow. Hakuna kitu kinachoniudhi kama kuishiwa Muda wakati wa Mtihani......Baba (Merehemu) alikuwa ananiambia "ukitaka akili yako iwe "sharp" na kuongeza uwezo wa ku-focus kwenye hesabu, fanya Mzoezi ya Hesabu mahali ambapo kuna k