Na haraka zao!! Yaani wapo mbio-mbio tu japo mbio zao zinatofautiana.....kuna wale wa starehe(Now) na wa maisha yajayo(Future)!!
Mdogo wangu wa Mwisho anatarajia kufunga ndoa hivi karibuni. Nilipopata habari za yeye Kuposwa nilipata hasira za ajabu!
Nikabaki nalalamika "yaani mdogo wangu mdogo hivi anaolewa"...."Vipi huyo mwanaume akienda kumtesa"? "Kwanini asisubiri kidogo jamani akue (huku nalia) bado mdogoooooooo" she's 23yrs!
Mama akaniuliza(Simuni), ningekupa taarifa kuwa anamimba au kazaa ugelia kiasi gani?!! Kabla sijajibu!! Asali wa Moyo nae akauliza swali hilo hilo(live).....nikasema but she's my little sister....can she just wait another 2yrs?!!!
Anyway, ilinichukua mwezi Mzima kukubali kuwa my baby little sister-o anaenda kuolewa!!
Sasa leo naongea nae, ananiambia "nipo site dada" Nkauliza Site ya maandalizi ya Ndoa? Akanijibu "Hapana Da Dinah, tunajenga"!!
...