Skip to main content

The why's!

Nilijua siku nikizaa mmoja kati ya wanangu (au wote) watakuwa waongeaji sana kama errr Mimi?!!





Well, najua kuwa napenda kuongea (labda kwa vile sinywi pombe au sina nguvu ya kupigana) lakini sio muongeaji kihiiivyo.





Nakumbuka Marehemu Baba alikuwa anawaambia watu "aah kuwa makini, binti yangu huyu anamaneno sana".





Kiukweli kabisa na admit mimi ni Mbishi sana....nope! wala sina asili na watu wa Kibondo, Kigoma! Labda kwa vile sina Nguvu za kupigana lakini wakati huohuo sipendi kuonewa, sipendi kudanganywa na siamni katika "kubali yaishe" BS na wala sio "ndio bwana"....sasa nikiwa na uhakika na ninachokisema nitakubishia mpaka kesho muda kama huu.






Turudi kwenye uongeaji ambapo ndipo Babuu(my 1st born) anapokuja sasa....Laaaa! Mwanangu anaongea jamaniiiii....akianza stori zake....halafu ana "why's" za kutosha.





Maana nilikuwa nahofia Hisabati akianza shule, sasa nina shughuli ya kujibu why's.....wakati mwingine mtu hujui hata jibu halafu huwezi kumdanganya, basi unabaki bikozi izi eh...I will google, I mean tell you when we get home!!!




Mbaya zaidi why's zake wakati mwingine ni ngumu(halafu mbele za watu)....hivi hapo ulipo bila kufikiria unaweza niambia kwanini tunapata Kwikwi (....toa jibu la Kibaiolojia kwa Kiinglishi)!





Ujue swali Why kwa Kiswahili ni gumu hivyo watoto wengi huwa waongeaji lakini huchelewa kuuliza ze "kwaniniZi"!




Mtoto anaweza kumlilia baba yake anapokwenda kazini halafu ukamwambia tu...baba kaenda kazini na atarudi jioni kesi ikaisha sio!




Huyu wangu bana lazma upate "why dad has to go to work everyday?".....na usipojibu swali litaimbwa mpaka utoe jibu lenye because....Hata sijui kwanini Asali wa Moyo anaenda kazi kila siku....eer in English that is!






Na ukitoa jibu fupi kama "dad has to work so that we can pay bills"....unapewa "why do we have to pay bills" aiiii kazi ya Ualimu nayo ni £24,000+ kwa mwaka.



Nikuache kwa sasa!
Mapendo tele kwako...

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao