Skip to main content

Posts

Showing posts from August 10, 2014

Mama wa Nyumbani...

Kwa mwaka mmoja na nusu (au tuseme miwili maana nilianza likizo ya Uzazi nikiwa na Mimba ya Miezi 5) nimekuwa Mama wa Nyumbani. Mie kuwa Mama wa nyumbani ilikuwa choice kutokana na moja ya Misimamo yangu ya kimaisha ambayo wengi hushindwa kunielewa....kwamba miaka 3 ya mwanzo ya wanangu ni lazima niifaidi (as in kuona wanavyobadilika kila siku, kuwafunza manners n.k kabla hawajaanza shule rasmi). Pia ile hali ya mimi kutoamini mtu mwingine kuangalia wanangu, nahisi kuwa hawatawapa huduma, upendo na attention inavyotakiwa, na wao hawataniambia kwani bado wadogo. Hiyo ilikuja baada ya kujifungua mtoto wa Pili, yule wa kwanza bado nilikuwa na ile "lazima nirudi kazini, am financially independent working Mum" hivyo Babuu akawa Day care akiwa bado mchanga. Back to Mama wa kunyumba! Heeeeeeee! Nawaheshimu wote, kazi yenu ni ngumu, Kuzaa is nothing compared to Mama wa Nyumbani na anashatili malipo ya juu ambayo ni zaidi ya £60,000 kwa mwaka....well sio wote bali wale ambao hawana

Maghorofa-2

Siku nimekatiza mahali nkasikia sauti ya Kike kwa Lafudhi ya Kipemba "Bwana Dullah wee panda basi mwenzio nipo hoi".....nkajisemea eh watu na shughuli zao asubuhi-asubuhi. Wacha mawazo machafu! Bwana Dulla alikuwa Chini ya Ghorofa akitaka Bibie amfuate kwani aogopa panda Lift-ini peke yake! Sasa Glasgow-Scotigo kama nilivyogusia jana ni Jiji (lililozubaa) lakini linamajengo Marefu mengi kuliko Majiji mengine ndani ya UK. Pamoja na sifa hiyo wataalam wanadai hayakujengwa vema na mbaya zaidi yana reputation mbaya ya "Komando Yoso" Vijana wakorofi na familia mbazo ni masikini(wanaotegemea Benefit). Wananchi wakaanza kuzikimbia nyumba za Maghorofani na kukimbia maeneo ambayo kuna majengo hayo Marefu kwa kuhofia "status" zao na kuibiwa au kuuwawa. Baada ya Muda Serikali(almashauri ya Jiji husika) wakaamua kuyabomoa yale ambayo waliona ni ghali sana kuyatengeneza na Mengine kuyagawa(kuyauza) kwa Mashirika

Majengo marefu(Maghorofa)!

Kuna yale yaliyojengwa kati ya Miaka ya 40s na 70s ( I guess) Ilala, na yale pale kati ya Mnazi Mmoja na Stesheni, Posta, Kariakoo, Tandika, Keko, Upanga, Ostabei. Halafu kuna yale ya Miaka ya 80-90 maeneo ya Tabata, Mbezi Beach.....tulia, nazungumzia Maghorofa ya NHC na ya Kampuni kubwa kama vile TTCL, PPF na kadhalika sio yake binafsi. Ninayoyataka hapa ni yale ya 40s-70s, ambayo hayakujengwa katika mfumo mzuri wa Maji safi na Maji taka, Nyaya za umeme zimekaa kihatari-hatari na Juu ya Ghorofa ya Mwisho kuna uwazi kwa ajili ya eer "kupunga hewa" " kufurahia the view"?!!! in which kwa nchi yenye watu wenye ma-stress na ma-depression kama UK ingekuwa rahisi kujipoteza (kujirusha ili kufa).....mbona tungewa-sue NHC mpaka wangekoma. Pamoja na hasi hizo bado majengo yale yana sifa ya kujengwa kwa kutumia Malighafi Imara ukilinganisha na Maghorofa yanayojengwa Karne hii. Magorofa hayo yakikarabatiwa mmmh itakuwa gharama kuu na pengine kulipuliwa na yaanza kuanguka labd