Skip to main content

Majengo marefu(Maghorofa)!

Kuna yale yaliyojengwa kati ya Miaka ya 40s na 70s ( I guess) Ilala, na yale pale kati ya Mnazi Mmoja na Stesheni, Posta, Kariakoo, Tandika, Keko, Upanga, Ostabei.


Halafu kuna yale ya Miaka ya 80-90 maeneo ya Tabata, Mbezi Beach.....tulia, nazungumzia Maghorofa ya NHC na ya Kampuni kubwa kama vile TTCL, PPF na kadhalika sio yake binafsi.

Ninayoyataka hapa ni yale ya 40s-70s, ambayo hayakujengwa katika mfumo mzuri wa Maji safi na Maji taka, Nyaya za umeme zimekaa kihatari-hatari na Juu ya Ghorofa ya Mwisho kuna uwazi kwa ajili ya eer "kupunga hewa" " kufurahia the view"?!!! in which kwa nchi yenye watu wenye ma-stress na ma-depression kama UK ingekuwa rahisi kujipoteza (kujirusha ili kufa).....mbona tungewa-sue NHC mpaka wangekoma.


Pamoja na hasi hizo bado majengo yale yana sifa ya kujengwa kwa kutumia Malighafi Imara ukilinganisha na Maghorofa yanayojengwa Karne hii.


Magorofa hayo yakikarabatiwa mmmh itakuwa gharama kuu na pengine kulipuliwa na yaanza kuanguka labda yapewe "cosmetic" tu....kubadili mfumo wa Maji safi na taka(choo incl) na umeme(yale manyaya bana khaaaa)!!

Majengo hayo ndio yanalifanya Jiji la Dar es Salam kupendeza na nadhani kuwa Jiji la kwanza lenye Majengo Marefu is it East Africa au Tz tu?(Hata sijui)!!....hupendeza sana mida ya Usiku (kama kuna Umeme).


Watu wanaokaa kwenye Maghorofa (Makabati hihihiihihi) hayo huwa na "status" tofauti na wale wanaokaa nyumba za Chini.....wanajidaaaaaai

Pale chini kuna Mitaro isiyorasmi inamwaga mimaji michafu na hapo pembeni kuna Mfumo wa Maji safi(what a mixture)....Karo zinafurika Vinyesi alafu watu hawana habari wala nini....full maringo! Nimekulia Maghorofani enzi zileeeeee hivyo najua ninachokizungumzia.

Kinachonisikitisha ni Maghorofa hayo kutelekezwa na ama watu Binafsi waliyoyanunua au Wamiliki kama vile NHC(kwa kisingizio wapangaji hawalipi Kodi kwa wakati).

Na pengine itafikia mahali watayabomoa na hivyo kupoteza Historia.

Kwanini nakuambia haya? Ni kutokana na uzoefu nilioupata Jijini Scotland. Kumbuka Scotigo ni wenye Majengo marefu Mengi kuliko Nchi nyingine ndani ya UK. Nitakuelezea sehemu ya pili. Very Interesting, usikose!


Babai.
Mapendo tele kwako...

Comments

Unknown said…
Mi nakupenda tu Dina kwa yote. Uandishi wako, your sense of humour, na ushauri na jinsi ulivvyo mtambuka (cross-cutting)

Deeply niko kama wewe ila nimevurugwa tu maishani so sometimes vipaji, karama na endowment nilizo nazo zinashindwa kuwa manifested na kunifanya most of the time kuwa mtu niliyejaa huzuni.
Nikipata nguvu siku nyingine nita share nawe a brief or unbrief version of my life, utajua namna ya kuitumia either kwa kuitohoa kidogo ili kunipa veil ya identity au kuitoa tu kama ilivyo iwe mafunzo wa watu wengine.

Nimependa tu kukuambia kuwa ni mfuasi wako kwenye blog zote mbili na naipenda hii maana iko 'valuvalu' na haitabiriki kuwa leo topic itakuwaje though na ile ya kule ndio ilikuwa zinduzi ya mie kukufahamu na kujua umebarikiwa mno kiuandishi na udadavuzi na unajua namna ya ku communicate na hadhira yako.

Be blessed na salimia BI (Barack na Iman)
MwanaMalundi
KKMie said…
Ah! MwanaMalundi nashukuru sana! Nimefurahi kufahamu kuwa nina "pacha" hehehehe. Usiuzunike, kumbuka kila kitu kina wakati wake. Ukifika utajimwaya tu kama ifuatavyo....

Salamu zimefika, ahsante kwa kujali. Ubaki salama.

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao