Skip to main content

Posts

Showing posts from 2015

Ndugu anaposema "ndugu" yake fulani ni attractive....

.....ni kwamba yupo attracted nae. Yaani anavutiwa nae na uwezekano wa yeye kuwa na "wivu" wa Kimapenzi au Kumtaka kimapenzi ni mkubwa. Hawa watu wapo kwenye Jamii na nina uhakika inagusa watu wengi ikiwemo mimi mwenyewe na ndio maana Daima huwa nasema Mjomba/Binamu/Mpwa sio Ndugu wa damu kwasababu hatuchangii Damu kwa asilimia 50 au zaidi(hii haina Usayansi). Kamakawaida nitakupa Mifano au "story" ili kukuburudisha na wakati huohuo kukusaidia unielewe ninaposimamia. Nina wajomba kama most of you, but nilikuwa na Mjomba mmoja(wa mwisho kwa kina Mama) ambae nilimpenda na tulielewana nahisi kwa sababu kiumri tuliendana, kwamba mie nilipokuwa Kidato cha Tatu, Yeye alikuwa Chuoni Mwaka wa Pili. Tulikuwa tunapatana na kwangu mie alikuwa kama "Kaka" mkubwa kabla ya Kaka yangu (wa damu)ambae ndio Kifungua Mimba wetu. Alikuwa akinifunza Hisabati (unajua mie na Hesabu tulivyo) na pia alikuwa akinisimulia Hadithi za Shida, Kuli, Thing fall a part etc(mi

Kristmas mwaka huu ni tofauti....

Yeboyebo hihihihi bado mnatumia hili neno? Wasukuma wa Shinyanga (enzi za Usichana) walikuwa wakisema Yebaaa as in Yeah....."Wananchi Mpo?" "tupo tupo kabisa kwa Jeuri ya Chama yee yee yeebaa". Twende kwenye Krismas sasa. Kwa kawaida mie huwa siandiki kuendana na Nyakati lakini Mwaka huu ni tofauti kwa sababu Waanangu has huyu Mkubwa kanifanya nianze kuipenda na kuifurahia Krismas tena. Miaka 3 nyuma alikuwa Mdogo so hakujali mapambo wala Santa, Mwaka huu anakaribia  miaka 5 na yupo Shule ambako wanafunzwa kama sehemu ya Utamaduni. Babuu akaandika(makorokocho) Barua yake kwa Santa akiorodhesha zawadi aitakayo na akatengeneza na Bahasha kisha kuiweka na kumpa Baba yake akaipost(which he did, huruma kwa postman mkusanya barua hihihi). Sasa kila leo anamzungumzia Santa na kudai atakuwa extra nice na kunisaidia kusafisha(anaacha toys kila kahali) ili Santa asibadili mawazo na hivyo yeye kukosa Zawadi siku ya Krismasi. Walipoanza kupamba Shuleni kwako akaja

Kupoteza Nywele baada ya Kujifungua Update (Bidhaa)....

Natumaini Post hii itakukuta ukiwa Mzima wa afya. Kama nilivyoahidi, leo nitakuelezea utaratibu wangu uliosababisha nywele(Relaxed) zangu kurudia Afya yake baada ya kuzipoteza na kupata "upara" wa muda. Jikoni kuna mwanga asilia, sihifadhi Bidhaa hizi Jikoni....hihihi! Ukiachilia mbali kuongeza aina ya Mboga iitwayo Kale kwenye Mlo wangu wa kila siku na kula Mayai 2-3 kila asubuhi. Bidhaa hizi zimechangia kwa kiasi kikubwa kuzuia Nywele zangu kuendelea kung'oka/anguka baada ya Kujifungua. Utaratibu wangu Rahisi. Kila Siku: Napaka Cantu Shea Butter kila siku asubuhi na Jioni na baada ya kupaka Cantu huwa na-"seal" na Mafuta asilia ya Sweet Almond. Kila Wiki: Huosha na Deep Condition Nywele zangu mara Moja (kila Ijumaa/JumaMosi) na huwa natumia Cream of Nature shampoo. Baada ya hapo nafanya deep condition kwa kutumia Vitale Mayonaise ambayo huwa nachanganya na Hello hydration (haipo pichani) na aina 2 za Mafuta asilia ambayo

Tumezaliwa ili tuzae....

....ndio Asali wa Moyo anaamini hivyo, which is Sad really.....but hey mepata topic! Wazazi wako walipoamua kuanza familia nadhani ilikuwa ni maana ya Ndoa, kwamba mtafanya Tendo hilo ili kuzaliana. Nia na dhumuni la Tendo la Ngono ni kuzaliana, kama hutaki kuzaa basi tumia Kinga (usiolewe/usioe) si ndio?!! Kwasisi wa kileo ambao tunabaki Shule kwa muda mrefu, Muda wa kufanya Tendo kwa "haki" (kuzaliana) huwa  sio muhimu, lakini pia sio wote tunaweza kuvumilia mpaka muda ufike...hivyo tunaanza Ngono kabla ya Ndoa nakujikinga "Kizungu" Dhidi ya "kuzaliana". Wazazi kutuzaa sisi ilikuwa uamuzi wao, haikuwa lazima na hakuna aliewalazimisha, sasa kwasababu tu nilizaliwa haina maana na mimi ni lazima nizae. Suala la kuzaa sio rahisi (kwa mwanamke ambae ndio anaezaa)kama ambavyo wengi wanafikiria. Mwili wa Mwanamke ni wa ajabu in a good way, Ukiachilia mbali Athari na Mabadiliko makuu(mengine yanahatarisha uhai) kwa Mwanamke kwa ndani baad

Hii ndio sababu ya mawifi/Mama wake kutuchukia?

Usinielewe vibaya, mie pia ni Wifi "mkubwa", lakini  tofauti ni...sio  kwamba nawachukia(hawajawahi kunikosea) au nawapenda(sijawahi kuishi nao).....nawachukulia kama walivyo na kuwaheshimu kama wanavyoniheshimu. Kamwe sijawahi/siwezi kujaji lolote kuhusu wao kwasababu siwajui kama ambavyo Kaka zangu wanawajua Wake zao. Sijawahi kuhoji kwenye  kufanana kwao na watoto wao. Huwa nasema tu mnawatoto wazuri, wapwa wangu wanapendeza n.k. Ikiwa Kaka zangu hawakuwa Makini na wanalea watoto wa wenzao, hiyo ni issue yao, sio yangu. Sasa, kuna siku nilikuwa nazungumza na Asali wa Moyo wangu kuhusu mambo ya Kijamii na tukagusia Chuki ya Wanawake kutoka Upande wa Mwanaume, akaniuliza hivi ni kwanini? Nkamwambia mie pia ni Wifi(mwanamke kutoka upande wa Kaka zangu) lakini sina Chuki na wala sifuatilii mambo yao na familia zao! Tukaenda ndani (deep)kidogo, nikagundua kuwa, chuki hii inaweza kusababishwa na moja9au yote) kati ya haya yafuatayo;- *Mwanamke anajua kuwa yeye ni

Kutunza Siri ni Wajibu wako....

...well, inategemea na unachokifanya for a living sio! Si unajua ile Kuapa au kuweka sahihi kuwa kamwe hutotoa siri (ujuayo) ya Kampuni/Mgonjwa/Mteja n.k. isipokuwa tu ikiwa Serikali na Mahakama itahitaji. Hello, natumaini Post hii imekukuta ukiwa na afya njema. Mie binafsi naamini kuwa kutunza "siri" ya mtu au watu ni wajibu wako. Kutokana na kile nilichokuwa nikifanya Miaka 8 iliyopita baadhi ya watu walijenga Uaminifu kwangu, kwamba walikuwa huru kuniambia mengi  kuhusu wao na maisha yao. Kwa maana hiyo nafahamu mengi ya watu wengi ambao hatufahamiani. Ile ilikuwa "kazi" ya kujitolea, sijasomea nilichokuwa n akifanua isipokuwa nilitumia uelewa wangu na uzoefu wangu(natambua unalijua hilo), hivyo sikula Kiapo na wala sikutia saini kuwa nitabaki na "siri" za watu Milele(haina maana nitazitoa). Pamoja na kuwa hakuwa "Kazi" bado nilichukulia na ninaendelea kuchukulia kuwa ni wajibu wangu kuto-share chochote kuhusu watu wote walion

Kupoteza Nywele baada ya Kujifungua....update!

Ni Mwaka na Miezi kadhaa tangu nikusimulie kuhusu Nywele zangu za kichwani ambazo ni Relaxed(bila shaka). Sasa, tangu tunamaliza Mwaka nimeona sio mbaya kama niki-share safari yangu ya kuwa na Nywele  tena zenye urefu wa kutosha kutengeneza mitindo na pia zenye afya. Halafu sio mbaya kama nikikutajia/nikionyesha Bidhaa ambazo zimenisaidia kufika hapa nilipofikia. Vilevile nitakuambia ni Bidhaa gani natumia lini na kwa nini(kwenye post nyingine) na nitaambatanisha Picha. Pamoja na kusema hayo ni vema utambue kuwa Bidhaa hizi hazikuhakikishii matokeo kama yangu, inaweza kuwa bora zaidi yangu au usione mabadiliko yeyote. Baadhi ya Bidhaa hizi nilikuwa natumia kitambo, baada ya kuhangaika na kujaribu aina nyingine na kutofanikiwa nikaamua kurudi kwenye bidhaa kutoka Vitale, Nikaamua kutumia "Steamer" na "Blow dryer". Awali nilikuwa situmii Heat kabisa kama nilivyoshauriwa na Gurus. Baadae nikagundua kuwa Nywele zangu zinapenda Heat so nikarudia utaratibu w

Single Mum/Loner Parent, Mzazi Mmoja=no Help

Hi! Sitojifanya mjuaji kwenye hili, tangu sijawahi kuwa "single mother" iwe kwa kutaka (wale wanaoamua kushika Mimba bila kuwa na hitaji la mwanaume husika) au kwa bahati mbaya, kwamba kutofautiana kwenu kumefanya mmoja wenu abaki na mtoto/Watoto(hapa siwazungumzii Wajane au wale waliobakwa, hii ni issue nyingine). Ninaowagusia hapa ni wale ambao kuwa "single mother" ni Mtindo wa Maisha,Sifa, chanzo cha kuonekana Imara/Unaweza! Wengi hapa ni wale Wasichana waliokulia miaka ya 90s na wale wa early 2000s. Ule msukumo wa kutaka kujitegemea ukikuwa na "impact" kubwa kwetu kiasi cha kuhisi hatuhitaji Wanaume ili kuwa na Familia. Tuliamini kuwa tunaweza kufanya yetu kama Wanawake na tunaweza kufanya ya Wanaume pia, "ikiwa mwanaume anaweza hata mimi naweza" sort of Imani....hakika hakuna afanyacho Mwanaume ambachoo sisi hatuwezi kufanya, lakini kuna mambo ambayo hatuwezi kuyafanya kama Wanawake kwenye malezi ya Mtoto au watoto(h

Kukosoa na Kumcheka mtu ni "interest" yako?

Nakuona! Wengi huamini kuwa ukiwa na tabia ya kukosoa au kucheka watu wengine basi wewe utakuwa na Matatizo kwenye Maisha yako, maisha yakoo hayana furaha na yamejawa na Huzuni na hivyo kukosoa na kucheka watu ndio njia pekee ya kujipatia "furaha". Nakubali kwa kiasi fulani, kwa baadhi kuwa Hasi kwenye kila kitu  ni tatizo na linaathiri maisha yao ya kila siku. wengine huamua kuwa Hasi kama sehemu ya kupata "attetion" au "Trafic" na "Views" popote walipo kwenye Sosho Midia. Kwa wale wa Ughaibuni, Maisha mitaa hii yanaweza kuwa ya Upweke sana na hivyo kumfanya mtu kutumia muda wake mwingi kwenye kutafuta "furaha" kwa kuwa Negative towards watu wengine. Upweke wa huku unatokana na utofauti wa Kitamaduni, Utaratibu wa kazi za "shift",  Majira ya Mwaka(Kiza kuingia mapema) vilevile kutumia muda mwingi kusafiri to na from work....by the time unafika nyumbani upo hoi, tayari ni Giza hivyo  hakuna muda wa kutoka au kukarib

Mzunguuko wa Ngono kwa Mwanamke...

Jambo! Kama unakumbuka niliahidi kuwa nikipata muda nitaandika kuhusu Mzunguuko wa Hedhi ambao unaendana na Mzunguuko wa Kufanya Ngono/Mapenzi kwa Mwanamke. Nilielezea kuwa Mwanamke sio kama Mwanaume, kwamba tunakabiliana na mambo mengi ukiachilia mbali Homono(Pengine ni Homono tu). Kuna siku Mwanamke analianzisha, inaweza kuwa mara moja au tatu kwa mwezi. Pia kuna siku mwanamke anataka kuwa Juu sio kwasababu wewe Mkibaba unataka bali mwili wake unamtuma kutaka kuwa in-control na hii inaweza kutokea mara kadhaa ndani ya mwezi lakini sio kila siku. Hali kadhalika zipo siku(ambazo ni nyingi) mwanamke anataka kuhisi kupendwa  na kujaaliwa kwa vitendo(kitandani)......vinginevyo Tendo halitokuwa na maana na halitokuwa la kufurahia. Wale Wanawake na Wanaume mabingwa wa kuwalaumu wanawake kuwa ndio sababu ya Waume zao kutereza nje ni ama hawaujui Mwili wa Mwanamke, kwamba mwanaume ataka na kutegemea Mwanamke awe in control kila siku......au kungojea Mwanamke alianzishe ili afurahi

Kulazimisha Mtoto awe na Mawazo....

Pengine ni ngumu kujua tofauti ya ku-share information kwa nia ya kuwafanya watambue "Asili" yao, wajifunze kuhusu Upande wa pili(kwa wale waishio Ughaibuni) na kuwapa watoto mawazo. Natambua kuwa kila Mzazi ana namna yake ya kulea na kufunza wanae, na kamwe sitokufundisha namna ya kulea wanao tangu mie mwenyewe  najifunza kila siku. Lakini tukumbuke kuwa kuna "Common Sense".....huitaji Elimu wala Uzoefu kuitumia. Unakumbuka ulipokuwa Mdogo na Mama au Baba au mtu yeyote wa karibu anaanza Hadithi za "Kaka/Dada" yako aliezaliwa na kufariki.....kisha ukaanza kuwaza ingekuwaje hivi sasa kama angekuwepo? Unawaza huko aliko je anafuraha, ana-toys,? unakuwa na Maswali kibao ambayo hayana Majibu. Mtoto anakosa usingizi kwa Mawazo au Uoga na akilala anamuota "dada/kaka". Wazazi hapa hudhani/amini kuwa Mtoto ana connection na "mwenzie"....lakini ukweli ni kuwa anasumbuka Kiakili na Kihisia. Pia umewahi kutambulishwa kwa Ndugu ya

Era ya Kulazimishana ku-react!

Heiyaaa! Mtu una-react kutokana na Uzito au Wepesi wa Hisia  unazopata kutokana na Tukio au Jambo fulani. Kuguswa kwako kunaweza kutokana na Upendo au Chuki au Kutojali, Kutoona umuhimu wa jambo hilo lililotokea n.k. Kama unakumbuka Rais aliyepita alikuwa mzuri sana/Maarufu kwenye kushiriki Masuala/Matukio ya Kijamii. Naamini kufanya kwake huko kulitokana zaidi na kuguswa kwake yeye kama Mwanadamu na sio kama Kiongozi wa Nchi. Kwamba anapojitokeza Mahali, haendi kuwakilisha Taifa basi yeye na pengine Familia yake. Reaction yake kwenye Misiba ilichukuliwa kivingine....achana na Siasa(Msimamo wangu kwa JK bado ni ule ule hihihihi), ni mfano wa karibu ili unielewe. Sasa kwenye Era hii ya Sosho Media imekuwa ngumu na pengine haikubaliki kwa baadhi yetu kuweka wazi hisia zetu kwa kuhofia kuonekana "tuna roho mbaya", "hatujali", "tunachagua matukio yapi ya kusikitika/kufurahia", n.k. Imefikia mahali wale "Magwiji" sijui "Wakongwe&

Wasichana tuliokulia miaka ya 90...

....ndio tulipokea kwa nguvu zote suala la Haki za Mwanamke au Usawa aka U-Beijin. Waliopigana vita ni Mama zetu ambao hawakutaka sisi tuonewe kama ambavyo wao walionewa. Baadhi ya Mama zetu hao walikuwa na Hasira na Wanaume kutokana na "treatment" walizopatiwa na Wanaume kama Wenza wako, Wafanya kazi wenzao, Wakubwa wao kwenye Familia na Maboss wao. Ujumbe na maana na nia ya "Ubeijing" ilikuwa nzuri na bado ni nzuri, lakini kwa baahati mbaya kwa baadhi ya akina Mama zetu hao waliziwakilisha kwetu, wasichana ambao tulizaliwa mwishoni mwa miaka ya 70s na 80s ambao ndio tumekulia era ya "Ubeijing" au niseme Miaka ya 90. Heka heka za kupigania Haki/Usawa kwa wanawake imeanza  miaka ya 60s kwa nchi niliyopo na mafanikio makubwa yalikuwa ni kutambuliwa kwa "haki" ya mwanamke kufurahia tendo la kufanya Mapenzi, kwamba tendo hili sio kwa ajili ya kumfurahisha mwanaume. Baada ya hapo ikaja suala la kutumia Kinda Dhidi ya Mimba(Kidonge).

Mzazi kukupenda zaidi ya wenzio...

Habari ya sasa! Kwa kawaida Mtoto wa Kwanza na yule wa Mwisho kwenye Familia nyingi hutokea kupendwa zaidi na wazazi au Mzazi......wakati mwingine wadogo/wakubwa zake. Sababu ya kuwa "favourite" angalau kwa muda hapa ipo wazi. Mtoto wa kwanza ndio kifungua Familia na huwa peke yake kwa muda mrefu au ikitokea kuna mdogo wake kaja fasta basi ile "huruma" huwafanya Wazazi waongeze attention kwa yule wa kwanza. Mtoto wa mwisho ni mdogo kuliko wote hivyo Wazazi na dada/kaka huwa over protected. Pamoja ya kupendelewa au kupendwa zaidi bado Wazazi wengi huwa hawaonyeshi hilo kwa uwazi ili kuepusha ugomvi au kuwafanya watoto wengine kujiona hawapendwi kwa kiwango sawa. Lakini mnapofikia umri mkubwa unaweza kuona kabisa kuwa Baba na Mama wanampendelea fulani zaidi na hivyo kuanza kujenga chuki au ushindani dhidi ya mwenzenu ambae mnahisi kuwa anapendelewa. Hali hufikia pabaya, mpaka anaependelewa kuanza kujidai na kutumia kupendwa zaidi na Waza

Bora alama ya Mstari kuliko F.....Miaka 20 Tangu Secondary

Mambo! Ijumaa Mpya(ya Kwanza Mwezi huu) na Maalum kabisa kwani ni Wiki ya Kwanza tangu kuanza kwa Mitihani ya Kumaliza Kidato cha Nne Tanzania, na ndio Mwanzo wa Mwisho wa Series hii(inaonekana kupedwa/somwa zaidi), inapendeza! Utakuwa unajua by now kuwa Mie na Hisabati sio marafiki, Biology niliipenda kwenye kuandika Essay kuhusu Maambukizo au Magonjwa(niliyajua haya kutokana na Somo la Sayansikimu kutoka Msingi), mengineyo nilikuwa sielewi(nilikuwa nasinzia). Mwalimu wetu wa Biology Kidato cha Tatu-Nne alikuwa a bit Boring au alikuwa  na Mapepo(hihihi). Yule mama alipokuwa akiingia na kufungua Mdomo "Good afternoon" mie yuleeeee Uzaramoni.....yaani macho yanakuwa mazito halafu nalala ule usingizi Mzito m paka Udenda! Nikaona aah isiwe shida bana, nikawa siingii kwenye Kipindi chake unless kuna Essay hehehehe. Sikufanya Mitihani Miwili  nayo Hisabati na Biology, kwasababu nilijua wazi sitofanikiwa kufanya vizuri na matokeo yake nikaamua ni Bora nipate alam

Kuzuia Mimba au Kupoteza Hamu?

Habari ya sasa! Utasema hee Dinah mbona umeshupalia Topic hizi? Well....ninachoandika hakitobadilisha Maisha ya watu na kuwa Bora zaidi ya yalivyo sasa, lakini naweza kusaidia mtu mmoja kuelewa kwa kiasi kidogo....yule ambae ame-google "kupoteza hamu" kwa mwanamke si eti! Kuna ulalamishi kuwa Dawa za kuzia Mimba(pamoja na matatizo mengine kwa baadhi) husababisha Mwanamke kupoteza hali ya kutaka/tamani Ngono. Hakuma chunguzi ambayo ina-support hili ila Wanawake wengi hulalamikia kuwa Hamu hupungua au hutoweka kabisa mara tu baada ya kuanza kutumia Njia za kuzuia mimba Zenye Homono(hata zisizo na Homono huingilia "hamu" ya mwanamke"). Do I look like I am busy? Ukweli ni kwamba kama hali ya kutaka  Ngono ilikuwa juu au chini basi haitobadilika......isipokuwa utaratibu wa Mwili wako ndio utabadilika na hivyo wewe Mkimama kulazimika kuanza kujifunza upya(wengi huwa hawalijui hili) namna mwili wako unafanya kazi. Tena sio Dawa za kuzuia m

Umuhimu wa Furaha ya Mke....

....wengi huchukulia suala hili juu juu tu, labda hushindwa kuelewa kwasababu Jamii (ikiongozwa na wanawake wenyewe) huwa  hailizungumzii sana kama wazungumziavyo Furaha ya Mume. Furaha ni hitaji la wote lakini nadhani kwa mwanamke ni muhimu zaidi kwasababu bila furaha kwake ni wazi watoto  na baba mtu hatokuwa na furaha. Pia furaha kwa mwanamke inahusika sana kwenye masuala ya kufanya mapenzi.....kama mwanamke hana furaha ni ama hakutakuwa na Tendo au Tendo halitokuwa la kufurahia na badala yake litakuwa ni la kumaliza haja tu kwa Mwanaume(maliza nilale arrg hihihihi). Wanaume wachache ambao wameshuhudia baba zao wakihakikisha Mama zao wanafuraha mara zote iwezekenavyo, hujitahidi na kuwa hivyo au zaidi kwa wake zao. Hawa hujua namna ya kujali  na kuheshimu hisia za mwanamke. Kwabahati mbaya sehemu kubwa ya Wanaume wamelelewa kwenye Mazingira ya kumuona Mama  ni mtu mmoja mvumilivu, mpole na muelevu.....wakati Baba Mkali na Bingwa wa kudharau. Kwamba Mama anapochoshwa n

Kufutiwa Matokeo Kidato cha 2.....Miaka 20 Tangu Secondary!

Ni Ijumaa nyingine tena ambapo tunaendelea na "Series" yetu. Unakumbuka nilikuambia kuwa pale Shuleni kwangu kwa zamani kulikuwa na Watoto wa watu Wazito na wale wa Mabalozi wa Tz Nje(waliokuwa wanasubiri kupewa Ofisi).....Tulipokuwa Kidato cha Pili kikaja kimtoto kina miaka Nane kilikuwa kinatokea Nchi gani sijui huko. Kilikuwa kinashuka mahisabati kwa Kiingereza hicho hihihihihihi. Aliondoka baada ya Wiki 6. anyway. Kusoma na watoto wa watu wazito ni raha, unapata kujua mambo mengi sana kuhusu maisha yao na(sio muhimu kivile lakini ndio hivyo), unakula maCandy na Majuisi ya Ulaya bana.....hasara yake inakuja kwenye Mitihani, sio siku ya Mitihani bali kwenye Matokeo. Kama unakumbuka mwaka wetu(piga mahisabati mwenyewe) baada ya Matokeo kufutwa(sote tukafaulu) ndio Mtihani wa Taifa wa Kidato cha pili ukafutwa, sababu zilikuwa nyingi kwanini hakukuwa  na umuhimu wa Kukaa Mtihani wa Kidato cha Pili. Nakumbuka siku tunaenda kuangalia Matokeo(ilikuwa siku ya s

Sababu Kuu ya Kumchukia Ex wake...

.....wengi hudhani kuwa ni Wivu au Hofu kwamba Mwanaume anaweza kurudi alikotoka au kukuacha kama alivyomuacha yule ila tofauti ni kuwa anakwenda kwa Ex wake sio Mwanamke mpya. Yote ni  sababu common lakini ile kuu ambayo wanawake wengi hutusumbua na hata kujenga dislike(nikisema hate inakuwa too strong) huenda ni hii hapa chini. Umewahi kutaka kumjua kama Mpenzi wako ana type? na pengine kwenda ndani na kutaka kumuona Ex wa Mpenzi wako kabla yako na hata kutaka kukutana nae? sio ili muwe marafiki bali ni kutaka kuona kama alikuwa Hot au Not....(hihihihihihi). Ikiwa Mpenzi wako ana type na aliempitia kabla yako alikuwa Hot basi unafurahi kuwa na wewe ni hot (pengine wala sio that hot) na kwabahati mbaya kama ex alikuwa Not basi hapo ndio hasira huja. Kila ukimfikiria/kumbuka yule Ex alivyo unamchukia vibaya sana hehehehehe huku unajisemea "am not that ugly" na kujiuliza "am I that ugly?". Yaani sio kwamba unachukia alivyo (kuwa ugly is okay but....) ba

Presha ya kuweka/toa info zako vs Ukarimu....

...enzi za DHB, Yahoo/MSN chatrooms (heeey Maajuza wenzangu hihihihi) ilikuwa ni kawaida kuulizawa upo wapi na unafanya nini au umefikaje huko uliko, wengine wanapitiliza mpaka kwenye unakuja lini Bongo n.k. Kwa baadhi yetu ilikuwa sio big deal kwasababu info hazikuwa muhimu kivile(kabla ya Google haijatufanya Kijiji) kuorodhesha Nasoma, mwaka wa pili  na huwa narudi Home kila Christmas. Jisni siku zilivyozidi kwenda na Maendeleo kuongezeka  na watu wengi kuwa na wasaa wa kufikia Mitandao na hivyo kuweka mengi kuliko wanavyohitajika. Siku hizi imefikia mahali wewe mwenyewe kwa hiyari yako unahisi kusema/share kila kitu, ikitokea mtu kauliza basi unajimwaga kwa uhuru kabisa, which is okay maana info ni zako bwana. Tatizo  ni kwamba wengi mnatoa mengi kuliko mnavyohitajika na matokeo yake baada ya muda wale wale mliowaambia wanatumia hayo kukuumiza au kukudharau. Hakika kila mtu ana haki ya kusema atakacho kuhusu maisha yake Halisi  au ya Kimtandaoni  ili tu awemo anapotaka

Scandals: Binti ajiua kisa B'friend+...Miaka 20 Tangu Secondary!

Hello tena, karibu  tuendelee na "series" sehemu ya maisha yangu ya Shule. Baada ya Muda si watu wakaanza ku-date bana.....unasikia tu gossip kuwa fulani anatoka na fulani, tulipotoka wao walienda kujibanza kwenye ma-bin na kufanya yao. Unaangalia Darasani(wa Asubuhi na Mchana) huoni hata Kijana wa kutoka nae(hakuna anaekuvutia(well mie nilikuwa mdogo Sec, 1st Bf alikuja nilipomaliza Kidatoo cha Nne huko mbele....Team Wasiona haraka. Achana na hili! Kanisa la Mtakatifu Joseph Wanafunzi wa nyuma yangu walikuwa Mapepe sana, na wengi walitokea palepale (Forodhani Msingi) hivyo walikuwa na Mahusiano na Wakaka wa Vidato vya juu  na mmoja wao aliekuwa akipiganisha Wadada wa kila Shule pale Mjini. Aliitwa JJ (sitasema alipokuwa akiishi wala alivyofanana)....alikuwa Mbele yangu Kidato. Huyu jamaa alikuwa napiganisha sana Mabinti wa Msingi na Wale wa Secondari(si unajua kuwa Foronda kuna Msingi na Sekondari eeh). Mwaka wao hawa akina JJ kulikuwa na wakaka "fresh"

Kijinyama/Ngozi kutoka K-ini...

...pengine hujawahi kuambiwa kuhusu hili la "kijinyama", "Kijingozi" lakini lipo na huwatokea wanawake wengi tu, tatizo ni kuwa wengi hawapendi kulizungumzia.....Uanake ni zaidi ya Makeup, Matiti na Kuvaa Magauni na Blauzi. Umewahi kujiswafi na ukakutana na kitu cha ajabu ukaanza kuogopa n a kudhani Kizazi kimetoka(hahahaha) au Mimba imeharibika bilakujua kama ulikuwa  nayo au ukadhani Umelogwa ili upate Hedhi ya Manyama badala ya Damu? Mara nyingi hii hutokea mara tu baada ya Kumaliza Hedhi na kufanya Mapenzi, au pengine umefanya Mapenzi na Mwenza akaenda "mbali" na baada ya kumaliza ukaona Damu na baada ya kujiswafi ukatoa "kijinyama" ambacho hakiterezi kama Ute Mzito au Damu nzito......usiogope hasa kama Umeruka Hedhi. Mfumo wa Uzazi wa Mwanamke Ukuta wa Mji wa Uzazi(Uterus/Womb) hujijenga kila baada ya siku 23 na baada ya hapo  hung'oka na kuteremka sambamba na Damu pale unapokuwa Hedhini....sasa ikiwa umepitiliza au