Skip to main content

Presha ya kuweka/toa info zako vs Ukarimu....


...enzi za DHB, Yahoo/MSN chatrooms (heeey Maajuza wenzangu hihihihi) ilikuwa ni kawaida kuulizawa upo wapi na unafanya nini au umefikaje huko uliko, wengine wanapitiliza mpaka kwenye unakuja lini Bongo n.k. Kwa baadhi yetu ilikuwa sio big deal kwasababu info hazikuwa muhimu kivile(kabla ya Google haijatufanya Kijiji) kuorodhesha Nasoma, mwaka wa pili  na huwa narudi Home kila Christmas.




Jisni siku zilivyozidi kwenda na Maendeleo kuongezeka  na watu wengi kuwa na wasaa wa kufikia Mitandao na hivyo kuweka mengi kuliko wanavyohitajika. Siku hizi imefikia mahali wewe mwenyewe kwa hiyari yako unahisi kusema/share kila kitu, ikitokea mtu kauliza basi unajimwaga kwa uhuru kabisa, which is okay maana info ni zako bwana. Tatizo  ni kwamba wengi mnatoa mengi kuliko mnavyohitajika na matokeo yake baada ya muda wale wale mliowaambia wanatumia hayo kukuumiza au kukudharau.





Hakika kila mtu ana haki ya kusema atakacho kuhusu maisha yake Halisi  au ya Kimtandaoni  ili tu awemo anapotaka kuwemo,,...hali ambayo inaweza kukupa Presha ku-keep up au ku-maintain Mtindo huo wa Maisha uliojitengenezea Online au ule ulioaminisha watu. Hali inayoweza kukusababishia dharau ikiwa  wale "uliowaaminisha" wakukute unaishi vinginevyo(wapate  kujua ukweli).





Pamoja na kuwa ni uamuzi wako na  ni haki yako kusema/share kila jambo lako, kumbuka kuwa sio lazima. hulazimiki by Law kufanya hivyo, kwahiyo zingatia nini hasa unataka kuweka wazi na nini kibaki kwa ajili ya watu wako wa Karibu na Marafiki(kama unao) waaminifu.




Kwasababu tu wengi ulionao kwenye maisha yako ya Mtandaoni(kwenye Sosho Midia) hasa maCeleb wanaweka kila kitu(wapo kazini na wanalipwa kufanya wafanyavyo) haina maana na wewe pia ufanye hivyo.




Ku-share kupita kiasi huenda mpaka nje ya Mitandao/Sosho Midia. Mfano baadhi yetu huwa na tabia ya Ukarimu eeh Watanzania sie ni ndugu. Jamaa kutoka Serikalini anakuja Ughaibuni kwa mfano, anataka kutunza Pesa alizopewa kwa ajili ya Hotel.....anatafuta connection ya mtu mwenye nyumba kubwa ampe Chumba ili a-save anunulie familia ya Mazawadi ya UK au akajenge huko Bongo baada ya Semina.





Unapomkaribisha mtu kwako(akae bure au achangie sehemu ya Bill) na kuishi nae kwa muda wa siku 3 au zaidi hakika atakuwa amekusanya Info za kutosha bila wewe kukusudia kuzitoa na matokeo yake anazitumia hizo kujumuisha Watanzania waishio Nje na hapo ndio Dharau inapoanza.




Kuanzia sasa Muache kukaribisha Wabongo kwa kisingizio cha Ukarimu/sisi Ndugu majumbani mwenu wanapokuja kwa ajili ya Semina, waacheni wakakae Hotelini huko. Hao mnaowafanyia Wema ndio hao hao wanaokwenda kuwaumiza na matokeo yake wote tunaonekana tunaishi maisha ya Kishenzi mnayoishi nyie......duh! hii sijui imetoka wapi.



Naheshimu na kuthamini Muda wako hapa, Ahsante kwa kuichagua Blog hii.

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao