Skip to main content

Posts

Showing posts with the label uchaguziTZ

Presha ya kuweka/toa info zako vs Ukarimu....

...enzi za DHB, Yahoo/MSN chatrooms (heeey Maajuza wenzangu hihihihi) ilikuwa ni kawaida kuulizawa upo wapi na unafanya nini au umefikaje huko uliko, wengine wanapitiliza mpaka kwenye unakuja lini Bongo n.k. Kwa baadhi yetu ilikuwa sio big deal kwasababu info hazikuwa muhimu kivile(kabla ya Google haijatufanya Kijiji) kuorodhesha Nasoma, mwaka wa pili  na huwa narudi Home kila Christmas. Jisni siku zilivyozidi kwenda na Maendeleo kuongezeka  na watu wengi kuwa na wasaa wa kufikia Mitandao na hivyo kuweka mengi kuliko wanavyohitajika. Siku hizi imefikia mahali wewe mwenyewe kwa hiyari yako unahisi kusema/share kila kitu, ikitokea mtu kauliza basi unajimwaga kwa uhuru kabisa, which is okay maana info ni zako bwana. Tatizo  ni kwamba wengi mnatoa mengi kuliko mnavyohitajika na matokeo yake baada ya muda wale wale mliowaambia wanatumia hayo kukuumiza au kukudharau. Hakika kila mtu ana haki ya kusema atakacho kuhusu maisha yake Halisi  au ya Kimtandaoni  ili tu awemo anapotaka

Scandals: Binti ajiua kisa B'friend+...Miaka 20 Tangu Secondary!

Hello tena, karibu  tuendelee na "series" sehemu ya maisha yangu ya Shule. Baada ya Muda si watu wakaanza ku-date bana.....unasikia tu gossip kuwa fulani anatoka na fulani, tulipotoka wao walienda kujibanza kwenye ma-bin na kufanya yao. Unaangalia Darasani(wa Asubuhi na Mchana) huoni hata Kijana wa kutoka nae(hakuna anaekuvutia(well mie nilikuwa mdogo Sec, 1st Bf alikuja nilipomaliza Kidatoo cha Nne huko mbele....Team Wasiona haraka. Achana na hili! Kanisa la Mtakatifu Joseph Wanafunzi wa nyuma yangu walikuwa Mapepe sana, na wengi walitokea palepale (Forodhani Msingi) hivyo walikuwa na Mahusiano na Wakaka wa Vidato vya juu  na mmoja wao aliekuwa akipiganisha Wadada wa kila Shule pale Mjini. Aliitwa JJ (sitasema alipokuwa akiishi wala alivyofanana)....alikuwa Mbele yangu Kidato. Huyu jamaa alikuwa napiganisha sana Mabinti wa Msingi na Wale wa Secondari(si unajua kuwa Foronda kuna Msingi na Sekondari eeh). Mwaka wao hawa akina JJ kulikuwa na wakaka "fresh"

Mke anafanyiwa mapenzi, sio the other way around!

Umewahi kusikia au kusoma mahali Wanaume wakisimulia namna wanavyowafanyia Wake zao na kuapia kuwa Mwanamke nahaitaji kufanyiwa mapenzi zaidi kuliko wao Wanaume, halafu uka-wish kimoyo-moyo Mumeo aje mahali hapo asome na ajifunze?!! Kama ilivyokuwa Dinahicious Blog, kwamba kuna baadhi ya Wanaume walikuwa wakitaka Wake zao wasome Baadhi ya Makala zangu ili wajifunze. Nakumbuka wapo walioniandikia wakisema huwa wanaacha Blog wazi kwenye Simu/Laptops kwa Makusudi tu ili Mke/Mpenzi apitie. Ni muhimu kumfanya Mumeo/Mpenzi wako ajihisi  kuwa ni Mfalme hapo nyumbani kwenu na unaweza kufanya ajisikie hivyo kwa namna nyingine  nyingi na sio kwenye Kufanya mapenzi kila anapokuhitaji/mnapohitajiana/unapomhitaji(siku hazifanani si unajua Homono nini  na nini).....Mwanamke huwezi kufanya yote, mengine mwachie na yeye! Imekuwa ni kawaida kwetu sisi wakimama kutafuta Mbinu za kumfurahisha Mwanaume Kingono zaidi kuliko wao.....wao wakibaba ni kama vile wametulia tu yaani wanasubiri k

Siku ya kwanza Kidatoni...Miaka 20 tangu Secondary!

Mwaka huu November inatimia Miaka 20, sasa sio mbaya kama nikiweka kumbukumbu zangu za safari yangu ya Shule kuanzia Msingi mpaka Secondari(intro hiyo hihihihi). Siku ya kwanza naingia kama Mwanafunzi wa Kidato cha kwanza ili kuwa ngumu maana hakukuwa na mtu nilietoka nae Msingi. Wengi walikuwa wanajigawa kwa makundi kwasababu wanajuana kwa kutoka shule moja ya msingi ama shule zao zilikuwa jirani. Kulikuwa na Wanafunzi kibao kutoka Mlimani Shule ya Msingi, Olympio na Upanga(wajuajiii, mabishoo, Kiingereza kingii). Ikabidi nitafute namna ya kujiunga nao, maana kati yao watakuwa na mimi Darasa moja.....nikaanza kutumia Tiketi ya Kuiba (naongea Kiingereza kwa Nyimbo hihihihihi). Nilikuwa najua nyimbo nyingi ahsante  "Double Compact something Cassete Music system".....unaweka Compact yako halafu unasimamisha ili kuandika mstari wa Wimbo husika. Nilikuwa na "book" full of nyimbo za RnB. Baba(Mungu amrehemu) alikuwa anatununulia hizo eti tujifunze Kiinger

Kipindi cha Baridi ndio unahisi kuwa Stylish....

Jambo! Nimeamua kuipenda Autum/Winter sasa, sio tu kuwa Kipindi hiki ndio najihisi kuwa stailishi bali pia napata nafasi ya kutumia(vaa) kila aina ya nguo niliyonayo kwa Kujiamini zaidi kwasababu hakuna  ile "presha" ya Kunyoa Kwapa wala Miguu na Mikono.....(well naficha chini ya Tights, Jaketi au Koti). Halafu Majira haya ni Marefu kuliko hizo siku 3 za Kiangazi. September Mpaka June ni total Baridi. mekosa Pic ya Mweusi ambae ana-stayle kama yangu (ubaguzi kando) Halafu pia Wivu wa hali ya hewa unakuwa hauumi sana kwa walio  Nchi za joto, unajua kuna muda unaangalia Fashinblogs za Tz halafu unapata Wivu wa hali ya hewa.....wanavalia nguo nyepesi na wanafurahia Kiangazi kwa Muda mrefu zaidi yako. Kipindi cha Kiangazi huku kinadumu kwa Mwezi mmoja, tena sio Mwezi Mzima mnapata Jua la maana bali mara mbili au tatu kwa Wiki ndani ya Miezi 3! Sasa kuna ulazima gani ya kuipenda Summer(Kiangazi)? Halafu huku tulikohamia Mwaka huu Kiangazi kilijitokeza kwa Si

Maharage Mabichi kutoka Tz yauzwa ASDA-UK

Unajua ile furaha unayipata unapokula kitu kutoka kwenu ambacho hujawahi kukila ulipokuwa kwenu? Kwamba unakula kwasababu tu unahisi unampa sapoti Mkulima wa kwenu. Hii ni mara ya tatu nanunua bidhaa hii  kutoka Asda kwasababu kuu mbili. Moja ni ya kijani(sababu za kiafya na kutunza mwili) na pili ni kwasababu yanatoka Bongo. Jinsi ninavyotengeneza: (kama upo interested)... Kula na/kwa Wali kama mboga: Nayachemsha kwa sekunde kiasi kisha namimina Tui la nazi (well unga wa nazi uliochanganywa na maji ya moto). Ongezea utamu kwa mlo wako kwa kuweka Embe mbivu au Ndizi mbivu. Kula na Samaki bila Wanga: Nayachemsha  pamoja ya "maua ya coli" na "brocoli" kisha  nanyunyizia pilipili Manga na Chumvi kisha namwagia "Fish sauce" kama uonavyo picha na tuvipande twa  Samaki. Kama ni mpenzi wa Rost pia zinakwenda vema hakikisha una Gravy. Unaweza kuchanganya hizo na Kisamvu (kuungwa na Karang