Skip to main content

Posts

Showing posts with the label ughaibuni

Kurekebisha/Komesha Tabia online, inawezekana?

Habariyo! Mengi kama sio karibu yote siku hizi yanawezekana Online, lakini kurekebisha Tabia ya mtu au watu Online? mie Mshamba hivyo sidhani kama inawezekama. Huwezi kumfunza mtu tabia njema ikiwa hakufunzwa hivyo na Wazazi/Walezi wake! Utakachokifanya ni kufanya watu wakuogope au Waogope kuwa karibu na wewe (unless ufiche Utambulisho wako). Inaaminika kuwa ni vigumu sana kwa Mtu kubadilika Kitabia akisha vuka Umri wa Miaka 25, atajaribu "kuacha" tabia yake ikiwa tu  kaamua iwe hivyo na kuna mtu wa karibu yake pembeni anamsaidia, lakini "msaidizi" akiondoka maishani mwake basi Mhusika hurudia tabia yake/zake Mbaya. Vilevile, ikiwa Mhusika mwenye Tabia mbaya amejenga Familia na Mtu ambae ana-support au kuelewa au samehe tabia yake mbaya, basi ugumu wa mhusika kubadilika huongezeka, kwasababu ana "support system"kutoka kwa Mke/Mumewe ambae ni Muhimu kuliko watu wengine wote wa online included. Kitambo hivi, kuna jamaa Walipatw

"Sheria" ya wa Ughaibuni kuwaletea Zawadi/kuwalisha Bata...

....nani aliiweka? au ndio mambo ya Mgeni karibu wenyeji tupone? Nakubali upatikanaji wa vitu ni rahisi zaidi huku kuliko Tanzania, lakini hiyo haina maana kuwa ukusanyaji(ununuzi na utunzaji) wa  makorokocho(vitu) na kusafirisha ni Rahisi pia! Ukiachilia mbali hilo, pia badhi yetu tunapokuja Nyumbani ni kwa ajili ya mambo  mengine na sio kulishana Bata kwenye sehemu mbalimbali za Kisasa hapo Nchini. Tandika Sokoni Eti wanataka ujisikie kama "upo nyumbani" kwa kukupeleka/tembeza meneo ya "Kisasa" ambako wanauza mavyakula(sumu) na vinywaji kama vya huko utokakao. Ukweli hapa sio wewe, bali wao ndio wantaka kenda kufanya watakayo kwa kutumia Vihela vyako vya huko utokako. Stori time: Nimerudi zangu Bongo na Mwanangu wa kwanza, tena akiwa mchanga(miezi 8). Kiutamaduni ndugu na jamaa hakuna kumshika mtoto "mikono" mitupu si ndio? heeee! Mwanangu kashikwa na Mikoni Milioni na hakuna hata mmoja aliemshikisha "Senti"....well isipokuw

Kukosoa na Kumcheka mtu ni "interest" yako?

Nakuona! Wengi huamini kuwa ukiwa na tabia ya kukosoa au kucheka watu wengine basi wewe utakuwa na Matatizo kwenye Maisha yako, maisha yakoo hayana furaha na yamejawa na Huzuni na hivyo kukosoa na kucheka watu ndio njia pekee ya kujipatia "furaha". Nakubali kwa kiasi fulani, kwa baadhi kuwa Hasi kwenye kila kitu  ni tatizo na linaathiri maisha yao ya kila siku. wengine huamua kuwa Hasi kama sehemu ya kupata "attetion" au "Trafic" na "Views" popote walipo kwenye Sosho Midia. Kwa wale wa Ughaibuni, Maisha mitaa hii yanaweza kuwa ya Upweke sana na hivyo kumfanya mtu kutumia muda wake mwingi kwenye kutafuta "furaha" kwa kuwa Negative towards watu wengine. Upweke wa huku unatokana na utofauti wa Kitamaduni, Utaratibu wa kazi za "shift",  Majira ya Mwaka(Kiza kuingia mapema) vilevile kutumia muda mwingi kusafiri to na from work....by the time unafika nyumbani upo hoi, tayari ni Giza hivyo  hakuna muda wa kutoka au kukarib

Presha ya kuweka/toa info zako vs Ukarimu....

...enzi za DHB, Yahoo/MSN chatrooms (heeey Maajuza wenzangu hihihihi) ilikuwa ni kawaida kuulizawa upo wapi na unafanya nini au umefikaje huko uliko, wengine wanapitiliza mpaka kwenye unakuja lini Bongo n.k. Kwa baadhi yetu ilikuwa sio big deal kwasababu info hazikuwa muhimu kivile(kabla ya Google haijatufanya Kijiji) kuorodhesha Nasoma, mwaka wa pili  na huwa narudi Home kila Christmas. Jisni siku zilivyozidi kwenda na Maendeleo kuongezeka  na watu wengi kuwa na wasaa wa kufikia Mitandao na hivyo kuweka mengi kuliko wanavyohitajika. Siku hizi imefikia mahali wewe mwenyewe kwa hiyari yako unahisi kusema/share kila kitu, ikitokea mtu kauliza basi unajimwaga kwa uhuru kabisa, which is okay maana info ni zako bwana. Tatizo  ni kwamba wengi mnatoa mengi kuliko mnavyohitajika na matokeo yake baada ya muda wale wale mliowaambia wanatumia hayo kukuumiza au kukudharau. Hakika kila mtu ana haki ya kusema atakacho kuhusu maisha yake Halisi  au ya Kimtandaoni  ili tu awemo anapotaka

Kujiamini kwa Mtoto kunaanza lini?

....Watoto wa "Ulaya" wanajiamini sana, je kuna namna ya kulea mtoto ili akikua ajiamini kama wa Ulaya? Mkaka mmoja aliniuliza. Nadhani wengi wetu tumeaminishwa Mengi ya Ughaibuni ni Mazuri/Mema....lakini katika hali halisi sivyo. Kuna soko zuri sana la Vitabu/Vipindi vya TV vinavyofunza Wazazi namna ya kulea watoto wenye Kujiamini. Ni tatizo la Wazazi husika ambao walilelewa "Kimaendeleo" na hivyo kuhofia kuwa watoto wao watakuwa kama wao. Hofu hiyo inawafanya wazazi kuwa-overprotect watoto. Nahisi tu sina uhakika. Kujiamini kunategemea zaidi na Malezi(nakubali) lakini sehemu kuwa ya Mtu/Mtoto kujiamini inatokana na yeye mwenyewe alivyoumbwa. Niliwahi kugusia Bloguni hapa kuwa kuna baadhi tumezaliwa hivyo(tunajiamini) lakini pia wapo ambao hawajiamini mpaka wafunzwe/himizwa/pewa Moyo/saidiwa kujiamini. Naamini Watoto wa Afrika(well Tanzania wa kizazi kileeee) tunajiamini kwasababu tulitumia muda mwingi kujifunza kimwili na sio kihisia kama watoto

Urijali/Uanaume Kamili/wa Kweli!

.....hapa lazma nivabe! Lakini kwasababu napenda kuchangia "knowledge" sio mbaya nikikuelezea nilichojifunza. Inawezekana kabisa hukubaliani na ninachotaka kuandika, basi angalau nipe nafasi na unisikilize(soma na share....ahsante). Unajua pale unaanzisha Topic halafu watu wanaivamia na kuaanza Malumbano (ya busara) halafu wewe upo pembeni unafurahia huku  unachukua "Material", basi ndivyo ilivyokuwa. Wengi tunaamini(mie mmoja wao mpaka Wiki Majuzi) kuwa Mwanume Rijal/Kamilii ni yule mwenye Uwezo wa Kusimamisha Uume kwa muda Mrefu au mwenye uwezo wa Kusimama na kufanya mapenzi na kufanikiwa kummimba mwanamke. Baadhi hudhani kuwa Wasenge sio Marijali kwasababu hawapendi wanawake aka hawawezi kuingia ukeni sababu hawawezi kuinuka(Hanithi).....kama Kusimamisha kwa muda mrefu ni Urijali basi hawa  majamaa ni MARIJALI haswa!! Achana na hili. Sehemu ndogo wanaamini kuwa kama Mwanaume  ni Rijali mwanamke mmoja hamtoshi....daah! Ujinga Mzigo. Hawa wan

Maisha ya sasa ni kusaidiana...

When it suits them.... Sina uhakika na wenzetu wa Nyumbani ila wengi wetu wa Ughaibuni (wanawake) tunalaliwa na Wanaume tunaoishi nao aka Wenza/Waume. Maisha ya Ughaibuni ni Magumu sana japokuwa upatikanaji wa vitu basic ni rahisi.....kwamba huwezi kuvaa nguo/viatu vilevile au kutumia Friji/Jiko/Kochi lilelile kwa miaka mitatu. Lazima kutakuwa na hitaji la kununua vipya(ni kwasababu ubora wake ni wa chini) lengo la Makampuni mengi nikuwawezesha Wananchi "wa kawaida" kumudu vitu ambavyo vinafanya maisha yao kuwa rahisi(kurahisisha maisha). Au tuseme ni "kiwango cha ubora wa maisha" kwa kila mwananchi kilichowekwa na Serikali.......sasa ukiamua kuibuka na Sumsang Fridge sababu unamudu hakika utakuwa nayo kwa miaka 10 zaidi. Turudi kwenye Kichwa cha Habari; Ughaibuni sote tunafanya kazi (mimi bado ni Temp Mama wa kunyumba)na tuna-share majukumu Kiuchumi  lakini linapokuja suala la majukumu ya kuangalia/kulea watoto tunaambia ni "jukumu la mama". Kwamba

Sio wote Ughaibuni tulifika kwa Ndege....

Mabaharia.....I see ya! Mambo vipi lakini(i sound like a male)? Ahsante kwa kuichagua Blog hii. Ujue huku nje ya Tanzania kila mtu anauchungu wa maisha kivyake kutokana na sababu zilizomleta....sio mnatujaji kwa kutujumuisha bana. Kuna wale walikuja kuongeza Elimu ili wakirudi waitumie ilimu yao ya kwa ajili ya Maendeleo ya Nchi yao Tukufu Tanzania. Halafu wapo waliochukia maisha yao yalivyokuwa Bongo na kwa hasira kutaka kwenda kujaribu au kuanza upya huko kwingine.....hawa kurudi sio chee(as in rahisi). Wengine walipelekwa na Wazazi wao baada ya kuanza tabia mbaya na zenye kutia aibu Wadhifu....sasa ili Wazazi waendelee ku-keep Status.....er ya Uchungaji wa Kanisa, Ukuu wa Jeshi au Uwaziri n.k so unapelekwa Nje ukafanye Umalaya wako kwa nafasi. Pia kuna akina sie tulioletwa huku kama Mtaji au Urithi.....kwamba Wazazi wanatumia Akiba ya familia ili ukasome na ukimaliza na kuanza kazi ama ulipe Deni na Riba au uwasaidie Nduguzo ambao technically umetumia Mgao wao wa Urithi

Wale akina bila "mimi" usingekuwa hapo!

Unawajua? Kwanza haujambo? Anhsante sana kwa kuichagua Blog hii. Kwa sie wa Ughaibuni (tuishio nje ya Tanzania)au wale tulioitwa Mjini kusoma au kufanya Kazi pia sisi wa Mtaani tuliamua kujaribu Fani na tukaipatia na tumefanikiwa kimtindo ndio huwa tunabeba hili limzigo. Sawa pengine bila wewe kweli asingekuwa hapo lakini ulifanyanini hasa kwenye mafanikio yake aliyonayo hivi sasa......zaidi ya kuwa njia tu ya yeye kufika hapo na actually ukajaribu kuharibu bila mafanikio? Kwa kawaida sisi wa Ughaibuni tukikaa sawa huwa tunapenda kusaidia wengine waje kujaribu maisha huku. Wanafikia kwako na unawasaidia kutafuta Kazi  na baada ya hapo nauli kwa miezi kadhaa halafu wanaanza kujitegemea. Kutokana na Ughali wa Maisha Ughaibuni well UK + "kikacha" unapaswa kuchangia sehemu ya Bills.....hakuna cha bure na hakuna "nakaa kwa Anti hapa" lipa bill dadaaa au nakutimua.....hapa sio Tanzania. Anyway.....maisha yanakuwa magumu kwa upande wako so unaongeza bidii kwenye kus