Skip to main content

Wale akina bila "mimi" usingekuwa hapo!

Unawajua?
Kwanza haujambo? Anhsante sana kwa kuichagua Blog hii.



Kwa sie wa Ughaibuni (tuishio nje ya Tanzania)au wale tulioitwa Mjini kusoma au kufanya Kazi pia sisi wa Mtaani tuliamua kujaribu Fani na tukaipatia na tumefanikiwa kimtindo ndio huwa tunabeba hili limzigo.




Sawa pengine bila wewe kweli asingekuwa hapo lakini ulifanyanini hasa kwenye mafanikio yake aliyonayo hivi sasa......zaidi ya kuwa njia tu ya yeye kufika hapo na actually ukajaribu kuharibu bila mafanikio?




Kwa kawaida sisi wa Ughaibuni tukikaa sawa huwa tunapenda kusaidia wengine waje kujaribu maisha huku.




Wanafikia kwako na unawasaidia kutafuta Kazi  na baada ya hapo nauli kwa miezi kadhaa halafu wanaanza kujitegemea.




Kutokana na Ughali wa Maisha Ughaibuni well UK + "kikacha" unapaswa kuchangia sehemu ya Bills.....hakuna cha bure na hakuna "nakaa kwa Anti hapa" lipa bill dadaaa au nakutimua.....hapa sio Tanzania.




Anyway.....maisha yanakuwa magumu kwa upande wako so unaongeza bidii kwenye kusoma na kufanya kazi 3 ili uweze kumudu Ada ya Chuo cha Uhakika(sio kile cha Kinaijeria alichokuombea  Dada yako) £12,000 kwa mwaka sio lelemama.....unajigawa vipi.....utajijua mwenyewe.




Mpaka hapo aliekuleta hana mchango kwenye kuhama Chuo wala Ada bali wewe mwenyewe.....isitoshe kaisha kufukuza kwake na amegoma kukupa Udhamini (wa Maandishi) baada ya kuona umekuwa "kitisho" kwamba unampiku (ujanja wa kusaka mahela)......




.......wenye Nchi nao wanagoma kukuongozea Kibali kwasababu "Mdhamini" aliekuleta amegoma kukudhamini kwa Maandishi ili uendelee kusoma na hivyo kulazimika kurudi kwenu Tanzania. Na huu ndio mwisho wa "bila mimi usingekuwa hapo" kwani techically umerudi Bongo.





Haya.....unapiga mahesabu urudi kwenu mahesabu hayaleti Jawabu. Umebakiza Mwaka uvute Degirii ya Muingereza halafu upate replacement ambayo itakusaidia kupata ajira ya Kudumu(ukifanya vema).





Unachukua Risk na unabaki Nchini kwa watu bila Kibali ili umalizie Masomo.....unaishi kwa hofu na wasiwasi. Kila ukiona au kukutana na Askari unahisi wanajua huna Karatasi....mtu akibisha hodi unakimbilia auvunguni......ukiona mtu kaja kazini na amevaa kiofisa unaenda jificha Chooni....basi ni karaa tu.





Mungu anabariki unapata replacement baada ya Muda unamaliza Shule halafu KABOOM Kampuni uliyofanya nayo replacement inakudhamini na kukuombea Kibali kama Mfanya kazi wao.





Siku unarudi Tanzania baada ya miaka Tano. Hakuna anaejua uliyopitia huko utokako na kwanini hukutudi likizo.....wanakupa siku tatu uzoee halafu kila mtu anakuja na tatizo lake.....wanakuona Mkombozi....usipotoa msada kwa kiwango watakacho basi unakumbushwa "bila nanilihu usingekuwa hapo".



Najua nimekugusa au nimekusaidia uelewe upande wa pili wa Hadithi ya "bila mimi usingekuwa hapo"......

Babai.

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao