Skip to main content

Kurekebisha/Komesha Tabia online, inawezekana?

Habariyo!

Mengi kama sio karibu yote siku hizi yanawezekana Online, lakini kurekebisha Tabia ya mtu au watu Online? mie Mshamba hivyo sidhani kama inawezekama. Huwezi kumfunza mtu tabia njema ikiwa hakufunzwa hivyo na Wazazi/Walezi wake! Utakachokifanya ni kufanya watu wakuogope au Waogope kuwa karibu na wewe (unless ufiche Utambulisho wako).



Inaaminika kuwa ni vigumu sana kwa Mtu kubadilika Kitabia akisha vuka Umri wa Miaka 25, atajaribu "kuacha" tabia yake ikiwa tu  kaamua iwe hivyo na kuna mtu wa karibu yake pembeni anamsaidia, lakini "msaidizi" akiondoka maishani mwake basi Mhusika hurudia tabia yake/zake Mbaya.



Vilevile, ikiwa Mhusika mwenye Tabia mbaya amejenga Familia na Mtu ambae ana-support au kuelewa au samehe tabia yake mbaya, basi ugumu wa mhusika kubadilika huongezeka, kwasababu ana "support system"kutoka kwa Mke/Mumewe ambae ni Muhimu kuliko watu wengine wote wa online included.



Kitambo hivi, kuna jamaa Walipatwa na Msiba. Sasa jamaa walikuwa wakiishi kivyao-vyao(hawana habari)na hawakujichanganya na Watz wenzao huko waliko Ughaibuni. Inasemekana walikuwa hawashiriki "Sosho events" za watu soooo walipofikwa na hiyo "life situation". Watu wakaamua kuwafunza "adabu Online".




Mie nilipoambiwa nikawashangaa watoa Adabu. Kwanini mtumie Maumivu ya watu kuwadhalilisha.....sawa nyie ni Watz zaidi yao(Wafiwa wanaishi Kizungu) basi toeni Adabu kiTz, Kijadi. Unakumbuka Utani Msibani? yep watu bado wanafanya haya na tulipofiwa na Mzee(Baba RIP) watani walitutania na kumuigiza marehemu Baba, baadhi unacheka na mengine yanakuongezea Uchungu zaidi.



Watani hutumiwa Misibani kufikisha Ujumbe/Funzo/Tia Adabu  "live" uliochanganyikana na Utani, sasa kama alietangulia alikuwa wa kujidai-Pua juu ndio mtajuzwa siku hiyo, Kutokana na Utu Washiriki watakuja Msibai lakini watafanya kwa "utani" vile ambavyo ulikuwa ukifanya kwenye matukio kama hayo kwa wenzako na mwisho kususia "Shughuli" ili kuwafunza  Adabu Waliobaki. Baada ya tukuio kupita utaanza kuona Wanafamilia wakianza "kubadilika" na kuanza kushiriki Matukio ya Kimaisha ya Jamii inayowazunguuka.



Hili haliwezi kuhamishiwa Online, unachokifanya Online ni kuiaibisha Familia ya mwenzio kwa kisingizio cha Kufunza tabia. Asilimia 99.9 wahusika hawatosoma/ona na wengi watakaosoma sio wahusika uliowakusudia. Kwa maana nyingine wale uliowakusudia wataendelea na "Uzungu wao" kama kawaida.



Mie binafsi sio Mtu ninaependa Mikusanyiko lakini huwa nashiriki kwenye Matukio ambayo nahisi kuwa ni Muhimu kama vile Msiba au Michango kwa ajili kusaidia Matibabu. Kwenye sherehe-sherehe hunikuti.


Ninachojaribu kusema hapa ni kuwa ni sawa kabisa  kujitenga(kutokuwa mtu wa mikusanyiko) lakini mtu unaemfahamu anapopatwa na Shida ni vema kutafuta muda na kushiriki. Natambua maisha ya Ughaibuni yanabana sana linapokuja suala la Muda(nafasi), Ugumu huongezeka mnapokuwa na Watoto.



Lakini ni muhimu kujigawa, hii ita-sound kizungu pia hihihihihihi tupo Uzunguni babu wee hehehehe. Kama ambavyo tunajigawa kwenye maswala mengine ya kimaisha kama vile bills, shopping....mjigawe, nani atakuwa anawakilisha Familia kwenye "life situation" kwenye jamii inayokuzunguuka iwe ni ya Wabongo wenzako au mchanganyiko.


Wakati mwingine sio rahisi kuwepo "live" kwenye tukio kutokana na Umbali wa Jimbo to Jimbo, Mkoa toMkoa, kwa UK ni Nchi na Nchi, basi tumia Simu eeh, shiriki ki-Digital.


Nashukuru na kuthamini Muda wako hapa, ahsante kwa kuichagua Blog hii.

Babai.

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao