Skip to main content

Kijinyama/Ngozi kutoka K-ini...


...pengine hujawahi kuambiwa kuhusu hili la "kijinyama", "Kijingozi" lakini lipo na huwatokea wanawake wengi tu, tatizo ni kuwa wengi hawapendi kulizungumzia.....Uanake ni zaidi ya Makeup, Matiti na Kuvaa Magauni na Blauzi.




Umewahi kujiswafi na ukakutana na kitu cha ajabu ukaanza kuogopa n a kudhani Kizazi kimetoka(hahahaha) au Mimba imeharibika bilakujua kama ulikuwa  nayo au ukadhani Umelogwa ili upate Hedhi ya Manyama badala ya Damu?




Mara nyingi hii hutokea mara tu baada ya Kumaliza Hedhi na kufanya Mapenzi, au pengine umefanya Mapenzi na Mwenza akaenda "mbali" na baada ya kumaliza ukaona Damu na baada ya kujiswafi ukatoa "kijinyama" ambacho hakiterezi kama Ute Mzito au Damu nzito......usiogope hasa kama Umeruka Hedhi.


Mfumo wa Uzazi wa Mwanamke



Ukuta wa Mji wa Uzazi(Uterus/Womb) hujijenga kila baada ya siku 23 na baada ya hapo  hung'oka na kuteremka sambamba na Damu pale unapokuwa Hedhini....sasa ikiwa umepitiliza au kuruka Hedhi moja au mbili, Ukuta ule ambao  ni ngozi/kijinyama huwa mnene zaidi na hivyo kugoma/kwamba wakati una-Hedhi-ka kile kijingozi hakiteremki  moja kwa moja Ukeni(Vagina) na matokeo yake hubaki ndani  pale pembeni mwa  Mlango wa Uzazi (Cervix).





Wakati mwingine huwa imeng'ang'ania na hivyo baada ya Uume kuingia na kufanya Uume ufanyavyo  "best" kile kijinyama hujiachia  na hivyo kuwa tayari kutoka kwa msaada wa kidole chako na Maji. Kama huna utaratibu wa Kujiswafi Ukeni ni wazi kuwa kitakaa huko na baadae kusababisha maambukizo au kutoa "ute" wa rangi ya ajabu (kahawia) na harufu mbaya.




Huenda hujawahi kutwa na hili hasa kama Mzunguuko wako sio wa Kuruka(unaenda Kila Mwezi) na haujawahi Kuzaa na Kunyonyesha.  Kama nilivyogusia hapo juu, kuwa kila baada ya Hedhi Ukuta wa Mji wa Mimba hujijenga na hung'oka baada ya muda ikiwa hakuna Yai lililorutubishwa na "ukuta" huo kuteremka sambamba na Damu yako ya Hedhi(Mie sio Daktari usiniulize Maswali).



Sasa ukizaa na ukawa unanyonyesha mara nyingi unapoteza Hedhi(hupati Hedhi mpaka umalize Kunyonyesha sio!), mpaka Hedhi bin Homono vinakuja kutulia baada ya kunyonyesha  ni wazi kuwa utakuwa unaruka-ruka na hivyo "ukuta" wa Mji wa Uzazi wako kuwa Mnene na hivyo kutoka kama nilivyoelezea hapo awali.



Pamoja na kuwa nimekutoa hofu bado ni Muhimu kwako kwenda Kumuona Daktari wa Magonjwa ya Kike na umuelezee hali halisi, jitahidi kuweka kumbukumbu ya Tarehe na aina/ukubwa/udogo wa "kijinyama" hicho ili Daktari aweze kukuelewa zaidi nahivyo kufanyiwa Vipimo yakinifu kuangalia kama Mfumo wako wa Uzazi upo na afya njema.


Naheshimu na kuthamini muda wako hapa, ahsante kwa kuichagua Blog hii.

Babai.

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao