Skip to main content

Umuhimu wa Furaha ya Mke....


....wengi huchukulia suala hili juu juu tu, labda hushindwa kuelewa kwasababu Jamii (ikiongozwa na wanawake wenyewe) huwa  hailizungumzii sana kama wazungumziavyo Furaha ya Mume. Furaha ni hitaji la wote lakini nadhani kwa mwanamke ni muhimu zaidi kwasababu bila furaha kwake ni wazi watoto  na baba mtu hatokuwa na furaha.




Pia furaha kwa mwanamke inahusika sana kwenye masuala ya kufanya mapenzi.....kama mwanamke hana furaha ni ama hakutakuwa na Tendo au Tendo halitokuwa la kufurahia na badala yake litakuwa ni la kumaliza haja tu kwa Mwanaume(maliza nilale arrg hihihihi).




Wanaume wachache ambao wameshuhudia baba zao wakihakikisha Mama zao wanafuraha mara zote iwezekenavyo, hujitahidi na kuwa hivyo au zaidi kwa wake zao. Hawa hujua namna ya kujali  na kuheshimu hisia za mwanamke.



Kwabahati mbaya sehemu kubwa ya Wanaume wamelelewa kwenye Mazingira ya kumuona Mama  ni mtu mmoja mvumilivu, mpole na muelevu.....wakati Baba Mkali na Bingwa wa kudharau. Kwamba Mama anapochoshwa na labda maudhi ya Baba na hivyo kuweka hisia zake wazi kwa "ukali".....baba hupata hasira kwanini "mwanamke" amwambie nini cha kufanya....yeye mwanaume na hivyo kuamua kukaa kimya(kumdharau Mkewe) ili yaishe.



Kwasababu najua akimjibu mkewe ni wazi Ugomvi utakuwa Mkubwa kwa maana Baba hato-back down na huenda akaishia Kumpiga Mama....ili kuepusha hilo Baba anajifanya anamsikiliza Mkewe(mama) lakini ukweli ni kuwa hakuna kinachoingia akilini na hakuna atakachofanyia kazi.



Sasa kwa Kijana aliekulia kwenye Mazingira kama hayo(kama nilivyogusia hapo juu) inakuwa ngumu kujua umuhimu wa furaha ya Mmwanamke kwenye Uhusiano wao. Furaha ya "mke" itakuwa na maana nyingine kabisa ambayo mimi na wewe(wanawake kama wanawake tunavyoifahamu).



Kwasisi Wanawake baadhi hukua kwenye Mzingira kama hayo pia lakini tofauti ni kuwa pembeni huwa tunafunzwa namna  Mwanamke anapaswa kuwa "treated" na namna gani Mwanaume anapaswa kuwa "treated". Wanaotoa mafunzo huwa ni Watu wazima ambao tayari wamepita kwenye maisha hayo na husisitiza kuwa Waume zao  hakuwa hivyo lakini hawakuwa  na jinsi kutokana na Jamii ilivyokuwa (kipindi hicho cha nyuma)alipaswa kuolewa kwa wakati ule ambapo aliolewa(hakuwa na option).




Sasa kutokana na kukosa Option, inakuwa kama vile wanajutia na hawataki sisi Wanawake wasasa(tunaofundwa) kuishi maisha walioishi wao.....kudharauliwa, kutosikilizwa, furaha zao kutotiliwa maanani n.k.



Je utamfurahishaje Mwanamke(Mke)?
Inategemea na Mwanamke husika lakini kuna yale ya Jumla ambayo kila mwanamke anahitaji ili kuwa na furaha na hivyo kuwa na Ndoa/Uhusiano mzuri:-


-Msikilize(najua tunaongea sana) lakini ni muhimu kuonyesha unamsikiliza na kumuelewa.

-Mshukuru(sio kwa kufanya Mapenzi) bali kwa lolote ambalo anakufanyia nje ya Kitanda, hata kama ni kidogo kama kukuletea Chai au kukutoa tongotongo.



-Muulize kabla ya kumkosoa(wewe sio Baba yake, hajifunzi kutoka kwako) hivyo ni vema kujua kwanini jambo limefanyika badala ya kukimbilia kumkosoa.



-Zika habari za Ex.....hakikisha huleti habari ambazo unajua zitasumbua akili yake(wale Funs wa kuzungumzia past lives zao kila Mgeni anapowatembelea au kila mnapokutana na watu wapya). Wote mna Past, kwanini udhani yako ni muhimu sana kujulikana kwa kila mtu?!!


-Hakikisha unajua tofauti kati ya Wajibu na Mapenzi, yupo na wewe kwasababu anakupenda......kukupenda sio Wajibu.

-Msaidie kwenye Malezi ya watoto(kama mmejaaliwa kuwa  nao), watoto wenu ni Wajibu wenu kama Baba na Mama, sio Wajibu wa Mama pekee.


-Mnunulie Zawadi once in a while hata kama ana kazi na mshahara Mkubwa kuliko wako.


Hey! Naheshimu na kuthamini Muda wako hapa, ahsante kwa kuichagua Blog hii.

Babai.

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao