Skip to main content

Wasichana tuliokulia miaka ya 90...


....ndio tulipokea kwa nguvu zote suala la Haki za Mwanamke au Usawa aka U-Beijin. Waliopigana vita ni Mama zetu ambao hawakutaka sisi tuonewe kama ambavyo wao walionewa. Baadhi ya Mama zetu hao walikuwa na Hasira na Wanaume kutokana na "treatment" walizopatiwa na Wanaume kama Wenza wako, Wafanya kazi wenzao, Wakubwa wao kwenye Familia na Maboss wao.




Ujumbe na maana na nia ya "Ubeijing" ilikuwa nzuri na bado ni nzuri, lakini kwa baahati mbaya kwa baadhi ya akina Mama zetu hao waliziwakilisha kwetu, wasichana ambao tulizaliwa mwishoni mwa miaka ya 70s na 80s ambao ndio tumekulia era ya "Ubeijing" au niseme Miaka ya 90.




Heka heka za kupigania Haki/Usawa kwa wanawake imeanza  miaka ya 60s kwa nchi niliyopo na mafanikio makubwa yalikuwa ni kutambuliwa kwa "haki" ya mwanamke kufurahia tendo la kufanya Mapenzi, kwamba tendo hili sio kwa ajili ya kumfurahisha mwanaume. Baada ya hapo ikaja suala la kutumia Kinda Dhidi ya Mimba(Kidonge).




Mkutano wa Nne wa wanawake uliofanyika Ubeijing mie nilikuwa  ndio namalizia Shule ya Secondary. Nilikuwa najivunia sana ile Hotuba ya yule Mama wa Kitanzania (nimesahau jina lake na sina mpango wa kuGugo....soma Picha hihihihi) niliona kuwa ni Mwanamke Msomi(academically smart), Shupavu na Imara.




Sasa, sisi Wasichana wa Era hiyo ndio tulikuwa wa kwanza kuweka "Ubeijing" kwenye actions kwa nguvu zote.....tulikuwa kwenye "presha" bila kujijua, tulihakikisha tunabaki shule kwa muda mrefu (sio kukimbilia kuolewa) na kuipata hiyo Elimu kama Wanaume, Era hiyo wengi  wetu tulichukua Masomo ya  "Magumu" kama vile Sayansi(nili drop katikati though usicheke), tunafanya kazi za Ufundi,Uinjinia, Urubani,Ukandarasi n.k.




Wasichana wengi tulifaulu Mitihani, hatukuwa wa kati wala mwisho tena. Tuliongoza Darasa na Mikondo. Dhamira yetu ya kujitegemea na kuongoza na kuelimisha Jamii iliendelea kukua tulipopatiwa Mawaziri wa Kike na kuona Wakurugenzi(akina Ms Mhavile and co) wakifanya mambo.




Fast Foward:...kwa Wasichana wa leo(waliozaliwa 90s wamekulia 2000s) ambao wengi wanaumri kama ule wetu miaka  ya 90, ni teens au wapo early 20s.....hawa are so relaxed! Wanajua haki zao, wanajua wanapaswa kujitegemea na how.....yaani kila kitu kipo wazi kwao hivyo hawapigani ile sanaa kama sisi miaka ya 90s.




Ni kama vile wameona "Ubeijing" haujafanikiwa kama tulivyotegemea(well tangu 1965 bado Wanawake hatujafanikiwa...safari ni ndefu). Wengi wa Era hii(2000s) wapo tayari kufanya kazi nusu siku ili wapate muda wa kuwa  na Familia zao na kuachia Jukumu la Mume kubaki palepale. "Ubeijing" umefanya Baadhi ya Wanaume kuwa tegemezi na matokeo yake mwanamke anafanya Jukumu la Baba na Majukumu yake kama Mama. Wasichana wa 2000s wanachangamoto ya  kubadilisha hili.




Wasichana wa 2000s(wanaokulia Era hii) wameanikiwa(wekea wazi) kila kitu na wao wana-choose and pick, tofauti na sisi  ambao hatukupewa Option kwasababu tulikuwa hatujui lolote kuhusu nafasi ya Mwanamke kwenye jamii ambayo ni zaidi ya Kuzaa na Kulea watoto.




Natambua wanawake wengi walikuwa wakijituma na kuongeza Kipato kwenye familia kabla ya miaka ya 90(Ubeijing era) lakini bado hawakuwa na sauti au nguvu kwenye Vipato vyao, so ni kama walikuwa "watumwa" wa Wenza wao.


Naheshimu na kuthamini Muda wako hapa, Ahsante kwa kuichagua Blog hii.

Babai.

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao